Wednesday 6 May 2020

Nguzo za swaumu

Nguzo za swaumu
NGUZO YA KWANZA: Ni kujizuia kufanya mambo yatakayo Haribu swaumu kuanzia kutokeza kwa alfajiri hadi kuzama kwa jua kwa kuingia jioni
Dalili ni kauli yake Mwenyezi Mungu U: {…Na kuleni na kunyweni mpaka ubainike kwenu weupe wa alfajiri katika weusi wa usiku. Kisha timizeni saumu mpaka usiku…} (Al-Baqarah- Aya 187).

NGUZO YA PILI: Ni kutia nia ya Kufunga
Nako ni kukusudia kwa anayefunga saumu ya kwamba huku kujizuia na vitu vinavyofungua saumu ni ibada kwa ajili ya Mwenyezi Mungu Mtukufu; kwa dalili ya kauli ya Mtume (saw): ( Hakika kila jambo analolifanya (mwanadamu) ni kulingamana na nia yake, na hakika kila mtu atalipwa kulingana na alivyonuilia)[Imepokewa na Bukhari na Muslim.] Endelea Kupata Zaidi

Friday 24 April 2020

Fadhila za swaumu

Swaumu ni Nini?
Saumu Katika Lugha
Ni kujizuia na kujiepusha kufanya jambo fulani.
Saumu Kisheria
Ni kufanya ibada kwa ajili ya Mwenyezi Mungu U kwa kujizuia kula, kunywa na kufanya tendo la ndoa kuanzia kutokeza kwa alfajiri hadi kutwa kwa Jua. Endelea Kupata Zaidi

Monday 20 April 2020

Abu Hurayrah-mpokezi wa hadithi

Mamilioni ya waislam tokea mwanzo mwanzo mwa historia ya kiislam hadi hii leo wanaisoma kauli hii ‘kutoka kwa Bwana Abu Hurayrah radhi za Mwenyezi Mungu zimfikie amesema, mjumbe wa Mwenyezi Mungu amesema…….”   Endelea Kupata Zaidi