Hiki
ni kisa kinachosimuliwa na Shaqiyq Al Bakhliy ambae siku moja alimwambia
Haatim, mwanafunzi wake, kama kilivyotajwa katika kitabu cha Minhaaj
Qaasidiin cha Ibnu Qudaamah/25 kwamba:
“Tumekuwa
pamoja kwa muda sasa . Umejifunza nini kutoka kwangu?
Haatim
akasema: “mambo manane”.
La
Kwanza:
Hakika
mimi kila nikiwaangalia viumbe nnamuona kila kiumbe ana mpenzi/kipenzi. Hata
hivyo afikapo kaburini mpenzi hufarikiana nae. Hivyo nikayajaalia matendo
yangu mema ndio kipenzi changu ili yawe nami ndani ya kaburi.
La
Pili
Nikiitazama
kauli ya Allah Subhaanahu Wata'ala katika Annazia’at/40
وَنَهَى النَّفْسَ عَنِ الْهَوَى
Na akaikataza nafsi na matamanio
Basi nikamua kupigana jihadi na nafsi yangu ili itulie katika
kumtii Allah Subhaanahu Wata’ala.
La Tatu
Nimeona kila mwenye kitu chake cha thamani hukitunza na
kukihifadhi vizuri. Nikaiangalia kauli ya Allah Subhaanahu Wata’ala katika
Annahl/96
مَا عِندَكُمْ يَنفَدُ وَمَا عِندَ اللّهِ بَاقٍ
Mlivyo navyo vitakwisha na vilivyoko kwa Allah ndivyo
vitakavyobakia.
Hivyo
kila nikijaaliwa kupata kitu chochote cha thamani hukielekeza kwake Allah
subhaanahu Wata’ala ili kibakie huko.
La
Nne
Nimeona
watu hufungamana zaidi na mali, nasaba na sharafu nikaiangalia kauli ya Allah
Subhaanahu Wata’ala Al Hujuraat/13
إِنَّ أَكْرَمَكُمْ عِندَ اللَّهِ أَتْقَاكُمْ
Hakika aliye mtukufu zaidi kati yenu kwa Allah ni huyo aliye
mchamungu zaidi katika nyinyi
Hivyo
nikajifunga zaidi na taqwa – uchamungu ili niwe karimu kwake Allah Subhaanahu
Wata’ala.
La
Tano
Nimeona
watu wanapenda husuda na kuhusudiana wao kwa wao. Nikaiangalia kauli ya Allah
Subhaanahu Wata’ala Azzukhruf/32
نَحْنُ قَسَمْنَا
بَيْنَهُم مَّعِيشَتَهُمْ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا
Sisi tumewagawanyia baina yao maisha yao katika uhai wa duniani
Basi
hapo hapo nikaacha kuhusudu.
La
Sita
Nimeona
watu wanafanyiana uadui wenyewe kwa wenyewe nikaangalia kauli ya Allah
Subhaanahu Wata’ala Faatir/6
إِنَّ الشَّيْطَانَ لَكُمْ عَدُوٌّ فَاتَّخِذُوهُ
عَدُوًّا
Hakika Shetani ni adui yenu, basi mfanyeni kuwa ni adui
Hivyo
nikaacha kuwafanya watu kuwa maadui na kuwa na adui mmoja tu – shetani.
La
Saba
Nimeona
jinsi watu wanavyojidhalilisha katika kutafuta rizki Nikaiangalia kauli ya
Allah Subhaanahu Wata’ala Huud/6
وَمَا مِن دَآبَّةٍ فِي
الأَرْضِ إِلاَّ عَلَى اللّهِ رِزْقُهَا
Na hakuna mnyama yoyote katika ardhi ila riziki yake iko kwa
Allah.
Nikajishughulisha
zaidi na yale yaliyokuwa wajibu kwangu kwake Allah na nikaiacha mali
yangu kwake
La
Nane
Nimeona
watu muda wao mwingi wanategemea biashara zao, viwanda vyao na afya ya miili
yao hivyo mimi nikawacha yote hayo na kumtegemea Allah Subhaanahu Wata’ala
pekee.
Wabillahi
Attawfiyq
|
Tujifunze Kutoka kwa Waliofahamu Kujifunza
Subscribe to:
Posts (Atom)