Hadiyth Ya 8 Nitamsibu Mja Wangu Kwa Homa Duniani Nimpunguzie Moto Wa Akhera



Hadiyth Ya 8



Nitamsibu Mja Wangu Kwa Homa Duniani Nimpunguzie Moto Wa Akhera



عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ عَنْ رَسُولِ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أَنَّهُ عَادَ مَرِيضًا وَمَعَهُ أَبُو هُرَيْرَةَ مِنْ وَعْكٍ كَانَ بِهِ فَقَالَ لَهُ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:  ((أَبْشِرْ.  إِنَّ اللَّهَ عَزَّ وَجَلَّ يَقُولُ: نَارِي أُسَلِّطُهَا عَلَى عَبْدِي الْمُؤْمِنِ فِي الدُّنْيَا لِتَكُونَ حَظَّهُ مِنْ النَّارِ فِي الْآخِرَةِ)) أحمد وابن ماجه والترمذي – حديث حسن

Kutoka kwa Abu Hurayrahرضي الله عنه  kwamba Mtume  صلى الله عليه وسلم alimtembelea mgonjwa aliyekuwa na homa pamoja naye akamwambia mgonjwa: ((Bishara njema (Furahi) kutoka kwa Allaah Anasema: Nitamsibu mja Wangu duniani kwa kwa moto (homa) Wangu ili aepukane na sehemu ya moto wa Akhera)) [Ahmad, Ibn Maajah, At-Tirmidhiy- Hadiyth Hasan]