Hadiyth Ya 42 Waja Peponi Watapata Ridhaa Ya Allaah



عَنْ أَبِي سَعِيدٍ الْخُدْرِيِّ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((إِنَّ اللَّهَ تَبَارَكَ وَتَعَالَى يَقُولُ لِأَهْلِ الْجَنَّةِ:  يَا أَهْلَ الْجَنَّةِ.  فَيَقُولُونَ لَبَّيْكَ رَبَّنَا وَسَعْدَيْكَ.  فَيَقُولُ هَلْ رَضِيتُمْ؟  فَيَقُولُونَ وَمَا لَنَا لَا نَرْضَى وَقَدْ أَعْطَيْتَنَا مَا لَمْ تُعْطِ أَحَدًا مِنْ خَلْقِكَز  فَيَقُولُ:  أَنَا أُعْطِيكُمْ أَفْضَلَ مِنْ ذَلِكَ.  قَالُوا: يَا رَبِّ وَأَيُّ شَيْءٍ أَفْضَلُ مِنْ ذَلِكَ؟  فَيَقُولُ: أُحِلُّ عَلَيْكُمْ رِضْوَانِي فَلَا أَسْخَطُ عَلَيْكُمْ بَعْدَهُ أَبَدًا)) البخاري, مسلم و الترمذي



Kutoka kwa Abu Sa’iyd Al-Khudriyyرضي الله عنه  ambaye kwamba Mtume صلى الله عليه وسلم     amesema: ((Allaah تَبَارَكَ وَتَعَالَى Atawaambia watu wa peponi: Enyi watu wa Peponi! Watasema: Labeka Mola wetu tuko kwa ajili ya amri Yako. Kheri yote imo katika mikono Yako. Kisha Atasema: Je, mmeridhika?  Watasema: Vipi tusiridhike na hali Umetupa ambayo Hukumpa yeyote mwengine katika viumbe Vyako? Kisha Atasema:  Nitakupeni kilicho bora kuliko hayo. Watasema: Ee Mola, ni kipi kilicho bora kuliko haya? Atasema: Nitafanya ridhaa (mapenzi) Yangu iwateremkie na baada ya hapo Sitokasirika nanyi tena abadan)) [Al-Bukhaariy, Muslim na At-Tirmidhy