Hadiyth Ya 40Mambo Yaliyozungushiwa Pepo Na Moto



عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ عَنْ رَسُولِ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((لَمَّا خَلَقَ اللَّهُ الْجَنَّةَ وَالنَّارَ أَرْسَلَ جِبْرِيلَ إِلَى الْجَنَّةِ فَقَال: انْظُرْ إِلَيْهَا وَإِلَى مَا أَعْدَدْتُ لِأَهْلِهَا فِيهَاز  قَالَ:  فَجَاءَهَا وَنَظَرَ إِلَيْهَا وَإِلَى مَا أَعَدَّ اللَّهُ لِأَهْلِهَا فِيهَا.  قَالَ:  فَرَجَعَ إِلَيْهِ قَالَ: فَوَعِزَّتِكَ لَا يَسْمَعُ بِهَا أَحَدٌ إِلَّا دَخَلَهَا. فَأَمَرَ بِهَا فَحُفَّتْ بِالْمَكَارِهِ. فَقَالَ: ارْجِعْ إِلَيْهَا فَانْظُرْ إِلَى مَا أَعْدَدْتُ لِأَهْلِهَا فِيهَاز  قَالَ: فَرَجَعَ إِلَيْهَا فَإِذَا هِيَ قَدْ حُفَّتْ بِالْمَكَارِهِز  فَرَجَعَ إِلَيْهِ فَقَالَ: وَعِزَّتِكَ لَقَدْ خِفْتُ أَنْ لَا يَدْخُلَهَا أَحَدٌ. قَالَ: اذْهَبْ إِلَى النَّارِ فَانْظُرْ إِلَيْهَا وَإِلَى مَا أَعْدَدْتُ لِأَهْلِهَا فِيهَا.  فَإِذَا هِيَ يَرْكَبُ بَعْضُهَا بَعْضًا.  فَرَجَعَ إِلَيْهِ فَقَالَ: وَعِزَّتِكَ لَا يَسْمَعُ بِهَا أَحَدٌ فَيَدْخُلَهَا. فَأَمَرَ بِهَا فَحُفَّتْ بِالشَّهَوَاتِ فَقَالَ: ارْجِعْ إِلَيْهَا فَرَجَعَ إِلَيْهَا فَقَالَ: وَعِزَّتِكَ لَقَدْ خَشِيتُ أَنْ لَا يَنْجُوَ مِنْهَا أَحَدٌ إِلَّا دَخَلَهَا)) الترمذي و قال حديث حسن صحيح – ابو داود والنسائي

Kutoka kwa Abu Hurayrahرضي الله عنه   kwamba Mtume صلى الله عليه وسلم amesema: ((Allaah Alipoumba Pepo na moto, Alimtuma Jibriyl Peponi Akimwambia: Iangalie na angalia matayarisho Nliyoyatayarisha kwa ajili ya wakaazi wake. Akasema (Mtume صلى الله عليه وسلم) Kwa hivyo alikuja kuiangalia na kuangalia matayarisho Allaah Aliyofanya kwa ajili ya wakaazi wake. Akasema: Akarejea kwa Allaah na kusema: Kwa Utukufu Wako, hakuna atakayesikia (habari yake) ila tu ataingia (Peponi). Kisha Akaamrisha izungushwe (ihusishwe) mambo magumu watu wasiyoyapenda, Akasema: Rejea na angalia yale Niliyoyatayarisha kwa ajili ya wakaazi wake. Akasema: Kisha akarejea na akakuta imezungukwa na mambo magumu watu wasiyoyapenda. Hapo alirejea kwa Allaah na akasema: Kwa utukufu Wako, nina khofu hakuna hata mtu mmoja atakayeingia. Akasema: Nenda motoni ukauangalie na uangalie matayarisho Yangu kwa ajili ya wakaazi wake. Akaona ulikuwa na matabaka moja juu ya tabaka jengine. Akarejea kwa Allaah na akamuambia: Kwa Utukufu Wako hakuna hata mmoja ausikiae (sifa zake) atakayeingia. Kisha Allaah Aliamrisha Uhusishwe na shahawa (matamanio ya nafsi). Kisha Allaah Akamuambia: Rejea tena (motoni). Alirejea tena na akasema: Kwa Utukufu, wako nakhofia kuwa hapatakuwa na yeyote atakayenusurika nao)) [At-Tirmidhiy akasema ni Hadiyth hasan, na Abu Daawuud na An-Nasaaiy]