Hadiyth Ya 4
Binaadamu Amenikana Na Amenitukana
عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّهُ
عَنْهُ عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ ((قَالَ اللَّهُ
كَذَّبَنِي ابْنُ آدَمَ وَلَمْ يَكُنْ لَهُ ذَلِكَ وَشَتَمَنِي وَلَمْ يَكُنْ لَهُ
ذَلِكَ فَأَمَّا تَكْذِيبُهُ إِيَّايَ فَقَوْلُهُ لَنْ يُعِيدَنِي كَمَا بَدَأَنِي
وَلَيْسَ أَوَّلُ الْخَلْقِ بِأَهْوَنَ عَلَيَّ مِنْ إِعَادَتِهِ وَأَمَّا
شَتْمُهُ إِيَّايَ فَقَوْلُهُ اتَّخَذَ اللَّهُ وَلَدًا وَأَنَا الْأَحَدُ
الصَّمَدُ لَمْ أَلِدْ وَلَمْ أُولَدْ وَلَمْ يَكُنْ لِي كُفْئًا أَحَدٌ)) البخاري والنسائ
Kutoka
kwa Abu Hurayrah رضي الله
عنه kwamba
Mtume صلى الله عليه وسلم amesema: ((Allaah Amesema: Binaadamu amenikana na hana haki ya
kufanya hivyo, na amenitukana na hana haki ya kufanya hivyo. Ama kunikana kwake
ni kusema: Hatonirejesha (tena) kama Alivyoniumba (Hatonifufua kama vile
Alivyoniumba). Na kuumba hakukuwa rahisi Kwangu kuliko kumfufua. Ama kunitukana
kwake ni kule kusema: Allaah Ana mtoto wakati Mimi ni Pweke, Mwenye kubaki
Sikuzaa wala Sikuzaliwa na hakuna chochote kinacholingana Nami)) [Al-Bukhaariy
na An-Nasaaiy]