Hadiyth Ya 35
Mja
Aliyewausia Wanawe Wamuunguze Kwa kukhofu Adhabu Ya Allaah
عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّهُ
عَنْهُ عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((كَانَ رَجُلٌ
يُسْرِفُ عَلَى نَفْسِهِ فَلَمَّا حَضَرَهُ الْمَوْتُ قَالَ لِبَنِيهِ إِذَا أَنَا
مُتُّ فَأَحْرِقُونِي ثُمَّ اطْحَنُونِي ثُمَّ ذَرُّونِي فِي الرِّيحِ فَوَاللَّهِ
لَئِنْ قَدَرَ عَلَيَّ رَبِّي لَيُعَذِّبَنِّي عَذَابًا مَا عَذَّبَهُ أَحَدًا
فَلَمَّا مَاتَ فُعِلَ بِهِ ذَلِكَ فَأَمَرَ اللَّهُ الْأَرْضَ فَقَالَ اجْمَعِي
مَا فِيكِ مِنْهُ فَفَعَلَتْ فَإِذَا هُوَ قَائِمٌ فَقَالَ مَا حَمَلَكَ عَلَى مَا
صَنَعْتَ قَالَ يَا رَبِّ خَشْيَتُكَ.
فَغَفَرَ لَهُ)) البخاري, مسلم, النسائي و ابن ماجه
Kutoka kwa
Abu Hurayrahرضي الله عنه kutoka kwa Mtume صلى الله عليه وسلم kwamba amesema: ((Mtu alifanya maasi makubwa na wakati mauti yalipomfikia
aliwausia wanawe akiwaambia: Nitapokufa, nichomeni, munisage na mulitawanye
jivu langu baharini kwani, WaLLaahi, Allaah Atakaponipata, Ataniadhibu adhabu
ambayo hajapata kuadhibiwa mtu mwingine. (Wanawe) walifanya walivyousiwa. Kisha
(Mola) Aliiambia ardhi: Toa kile ulichokichukua. Hapo tena akazuka! Na (Mola) akamuambia: Kitu gani
kilichokufanya ufanye hayo uliyofanya? (Yule mtu) akasema: Ni kukuogopa Wewe Ee
Mola wangu (au alisema: Ni kukukhofu wewe) na kwa sababu hiyo Mola Alimsamehe)) [Al-Bukhaariy, Muslim,
An-Nasaaiy na Ibn Maajah]