Hadiyth Ya 27 - Wapendanao Kwa Ajili Ya Allaah Wapate Kivuli Chake


عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:  ((إِنَّ اللَّهَ يَقُولُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ أَيْنَ الْمُتَحَابُّونَ بِجَلَالِي الْيَوْمَ أُظِلُّهُمْ فِي ظِلِّي يَوْمَ لَا ظِلَّ إِلَّا ظِلِّي)) البخاري ومالك

Kutoka kwa Abu Hurayrahرضي الله عنه  ambaye amesema kwamba Mtume صلى الله عليه وسلم  amesema: ((Allaah Atasema siku ya Qiyaamah: Wako wapi wale wapendanao kwa (ajili ya) utukufu Wangu? Leo Nitawaweka kwenye kivuli Changu siku ambayo hakuna kivuli isipokuwa kivuli Changu]. [Al-Bukhaariy na Maalik]