Hadiyth Ya 10 Mwenye Kufanya Amali Isiyokuwa Kwa Ajili Yangu Nitaikanusha



Hadiyth Ya 10



Mwenye Kufanya Amali Isiyokuwa Kwa Ajili Yangu Nitaikanusha



عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ (( قَالَ اللَّهُ تَبَارَكَ وَتَعَالَى أَنَا أَغْنَى الشُّرَكَاءِ عَنْ الشِّرْكِ مَنْ عَمِلَ عَمَلًا أَشْرَكَ فِيهِ مَعِي غَيْرِي تَرَكْتُهُ وَشِرْكَهُ)) مسلم و ابن ماجه


Kutoka kwa Abu Huraryah رضي الله عنه ambaye amesema: Mtume صلى الله عليه وسلم amesema: ((Allaah  تَبَارَكَ وَتَعَالَىAmesema: Mimi mkamilifu [kabisa kabisa mwenye kukamilika kwa kila kitu] Sihitaji mshirika. Kwa hiyo, yule anayefanya amali kwa ajili ya mwengine isiyokuwa kwa ajili Yangu, Nitaikanusha pamoja mshirika wake)) [Muslim na Ibn Maajah]