سُورَةُ الْقِيَامَة
Al-Qiyaamah (75)
بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ
لَا أُقْسِمُ بِيَوْمِ الْقِيَامَةِ ﴿١﴾
|
1. Naapa kwa siku ya Qiyaamah. |
وَلَا أُقْسِمُ بِالنَّفْسِ اللَّوَّامَةِ ﴿٢﴾
|
2. Na Naapa kwa nafsi inayojilaumu. |
أَيَحْسَبُ الْإِنسَانُ أَلَّن نَّجْمَعَ عِظَامَهُ ﴿٣﴾
|
3. Je, anadhani insani kwamba Hatutoikusanya mifupa yake? |
بَلَىٰ قَادِرِينَ عَلَىٰ أَن نُّسَوِّيَ بَنَانَهُ ﴿٤﴾
|
4. Ndio! Tuna uwezo wa (hata) kusawazisha ncha za vidole vyake (zikiwemo alama zake). |
بَلْ يُرِيدُ الْإِنسَانُ لِيَفْجُرَ أَمَامَهُ ﴿٥﴾
|
5. Bali anataka insani aendelee kutenda dhambi mbele yake. |
يَسْأَلُ أَيَّانَ يَوْمُ الْقِيَامَةِ ﴿٦﴾
|
6. Anauliza (kwa istihzai) ni lini (hiyo) siku ya Qiyaamah? |
فَإِذَا بَرِقَ الْبَصَرُ ﴿٧﴾
|
7. Basi jicho litakapoduwaa. |
وَخَسَفَ الْقَمَرُ ﴿٨﴾
|
8. Na mwezi utakapopatwa. |
وَجُمِعَ الشَّمْسُ وَالْقَمَرُ ﴿٩﴾
|
9. Na itakapojumuishwa jua na mwezi. |
يَقُولُ الْإِنسَانُ يَوْمَئِذٍ أَيْنَ الْمَفَرُّ ﴿١٠﴾
|
10. Atasema insani siku hiyo: “Wapi pa kukimbilia?” |
كَلَّا لَا وَزَرَ ﴿١١﴾
|
11. Hasha! Hapana mahali pa kukimbilia. |
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوْمَئِذٍ الْمُسْتَقَرُّ ﴿١٢﴾
|
12. Kwa Rabb (Mola) wako siku hiyo ndio makazi ya kustakiri. |
يُنَبَّأُ الْإِنسَانُ يَوْمَئِذٍ بِمَا قَدَّمَ وَأَخَّرَ ﴿١٣﴾
|
13. Siku hiyo insani atajulishwa yale aliyoyakadimisha na aliyoyaakhirisha. |
بَلِ الْإِنسَانُ عَلَىٰ نَفْسِهِ بَصِيرَةٌ ﴿١٤﴾
|
14. Bali insani (atakuwa) shahidi dhidi ya nafsi yake. |
وَلَوْ أَلْقَىٰ مَعَاذِيرَهُ ﴿١٥﴾
|
15. Japo akitoa nyudhuru. |
لَا تُحَرِّكْ بِهِ لِسَانَكَ لِتَعْجَلَ بِهِ ﴿١٦﴾
|
16. Usitikise lisani yako ili kuiharakiza (Qur-aan ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم). |
إِنَّ عَلَيْنَا جَمْعَهُ وَقُرْآنَهُ ﴿١٧﴾
|
17. Hakika ni juu Yetu kuikusanya (moyoni mwako), na (kuiwezesha) kuisoma kwake. |
فَإِذَا قَرَأْنَاهُ فَاتَّبِعْ قُرْآنَهُ ﴿١٨﴾
|
18. Basi Tunapoisoma (kupitia Jibriyl), fuata kusomwa kwake. |
ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا بَيَانَهُ ﴿١٩﴾
|
19. Kisha ni juu Yetu kuibainisha (kwako). |
كَلَّا بَلْ تُحِبُّونَ الْعَاجِلَةَ ﴿٢٠﴾
|
20. Sivyo katu! Bali mnapenda (uhai wa dunia) unaopita haraka kwa muda tu. |
وَتَذَرُونَ الْآخِرَةَ ﴿٢١﴾
|
21. Na mnaiacha Aakhirah (yenye kudumu abadi). |
وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ نَّاضِرَةٌ ﴿٢٢﴾
|
22. (Baadhi ya) Nyuso siku hiyo zitanawiri. |
إِلَىٰ رَبِّهَا نَاظِرَةٌ ﴿٢٣﴾
|
23. Zikimtazama Rabb (Mola) wake. |
وَوُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ بَاسِرَةٌ ﴿٢٤﴾
|
24. Na (baadhi ya) nyuso siku hiyo zitakunjana (kwa kusononeka). |
تَظُنُّ أَن يُفْعَلَ بِهَا فَاقِرَةٌ ﴿٢٥﴾
|
25. Zitaelewa yakini kuwa zitafikiwa na msiba unaovunja uti wa mgongo. |
كَلَّا إِذَا بَلَغَتِ التَّرَاقِيَ ﴿٢٦﴾
321
|
26. Hasha! Itakapofika (roho) mafupa ya koo. |
وَقِيلَ مَنْ ۜ رَاقٍ ﴿٢٧﴾
|
27. Na itasemwa: “Ni nani wa kumzingua (kumtibu)?” |
وَظَنَّ أَنَّهُ الْفِرَاقُ ﴿٢٨﴾
|
28. Na ataelewa yakini kwamba ni (wakati wa) kufariki. |
وَالْتَفَّتِ السَّاقُ بِالسَّاقِ ﴿٢٩﴾
|
29. Na utakapoambatanishwa muundi kwa muundi. |
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوْمَئِذٍ الْمَسَاقُ ﴿٣٠﴾
|
30. Siku hiyo kwa Rabb (Mola) wako ndio kuendeshwa (kupelekwa huko). |
فَلَا صَدَّقَ وَلَا صَلَّىٰ ﴿٣١﴾
|
31. (Kwani) Hakusadikisha (hii Qur-aan) na wala hakuswali. |
وَلَـٰكِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ ﴿٣٢﴾
|
32. Lakini (badala yake) alikadhibisha na akakengeuka. |
ثُمَّ ذَهَبَ إِلَىٰ أَهْلِهِ يَتَمَطَّىٰ ﴿٣٣﴾
|
33. Kisha akaenda kwa watu wake akijigamba. |
أَوْلَىٰ لَكَ فَأَوْلَىٰ ﴿٣٤﴾
|
34. Ole kwako! Ole kwako (ewe kafiri)! |
ثُمَّ أَوْلَىٰ لَكَ فَأَوْلَىٰ ﴿٣٥﴾
|
35. Kisha ole kwako! Tena ole kwako! |
أَيَحْسَبُ الْإِنسَانُ أَن يُتْرَكَ سُدًى ﴿٣٦﴾
|
36. Je, anadhani insani ataachwa bila ya lengo (bure)? |
أَلَمْ يَكُ نُطْفَةً مِّن مَّنِيٍّ يُمْنَىٰ ﴿٣٧﴾
|
37. Kwani hakuwa tone kutokana na manii lilotonwa? |
ثُمَّ كَانَ عَلَقَةً فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ ﴿٣٨﴾
|
38. Kisha akawa pande la damu, (Allaah) Akamuumba na Akamsawazisha? |
فَجَعَلَ مِنْهُ الزَّوْجَيْنِ الذَّكَرَ وَالْأُنثَىٰ ﴿٣٩﴾
|
39. Akamjaalia jozi; dume na jike. |
أَلَيْسَ ذَٰلِكَ بِقَادِرٍ عَلَىٰ أَن يُحْيِيَ الْمَوْتَىٰ ﴿٤٠﴾
|
40. Je, hivyo Hakuwa (Huyo Muumbaji) Qaadir (Muweza) wa kuhuisha wafu?
Ukitaka kusoma Sura nyengine Rejeauliko toka
Ukiwa una shauri au maelezo juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii falhaqqiy@gmail.com |