Madrasa Chigugu yachangamka kwa kasi ikiwa ni mwitiko wa kipekee baada kukosekana kwa kitambo kirefu

Miaka takribani Sita sasa kumekosekana  madrasa yenye uhakika kutokana na kuhamishwa Sheykh aliyekuwa akifundisha wakati huo kutokana chuki za vigogo wa kijiji cha Chigugu. Sheykh Abillah  mwenye kipaji cha ufundishaji wa Elimu ya dini ya Kiislam, ujuzi wa kuwavuta watu wenye rika tofauti tofauti kuwa na ari ya kusoma dini alijikuta akinyanyasika, kutukanwa na kufukuzwa kwa kashifa, kutokana na Nuru aliyokuwa akiieneza katika jamii hiyo ilyo totoro na Ushirikina, Ulevi, Zinaa na Uislamu wa kurithishana.

Mafanikio yaliokuwa yakipanda kwa kasi, na juhudi za wazi za Sheykh Abillah na wenzake walioamua kuikomboa jamii yao iliyokithiri katika ujinga yakadhoofishwa na na Mamwenye wachache wa mji na kusababisha kizuri kuwa kibovu. Waliyeshuhudia tukio la kufedheheshwa Sheykh walilaumu hatua iliyofikia ya kumwagiwa Pombe mahala pa Kuswalia, na matusi kejeli za Usuni n.k. Tunamuomba Allah (Subhaanahu wa Ta'ala) amjaalie subira.

Baada ya kipindi hicho chote Chigugu yaanza madrasa kwa watoto, watu wazima wake kwa waume baada ya kituo kimoja cha Kisunnah kung'amua tatizo hilo na kuamua kulivalia njuga kwa hali na mali.Imam wa Masjid Al -Ansaar Chigugu Sheykh Hamisi Nachembe amehakikisha ya kwamba awamu hii madrasa itasimamiwa vizuri. Kwa upande wake mwalimu wa mmoja kati yao Ustaadh Juma  naye ameamua kujitoa kweli kweli katika jambo hili kwa kusema hii ni sehemu ya fadhila na Mas'ul kwa Allah (Subhaanahu wa Ta'ala).

Allah (S.W) awatilie wepesi walewaliojitoa kwa ajili ya kuitafuta fardhi hii ya elimu na wengine wengi wawe wenye kujitokeza. Aamiin!