Hadiyth Ya 44
 Ninayempenda Zaidi Ni Lofa, Mwenye Swalah Nyingi, Ananiabudu Kwa Siri, Si Maarufu, Anastahmili Hali Ya Uduni


  عَنْ أَبِي أُمَامَةَ عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ:  ((إِنَّ أَغْبَطَ أَوْلِيَائِي عِنْدِي لَمُؤْمِنٌ خَفِيفُ الْحَاذِ ذُو حَظٍّ مِنْ الصَّلَاةِ أَحْسَنَ عِبَادَةَ رَبِّهِ وَأَطَاعَهُ فِي السِّرِّ وَكَانَ غَامِضًا فِي النَّاسِ لَا يُشَارُ إِلَيْهِ بِالْأَصَابِعِ وَكَانَ رِزْقُهُ كَفَافًا فَصَبَرَ عَلَى ذَلِكَ)) ثُمَّ نَقَرَ بِيَدِهِ فَقَالَ:  ((عُجِّلَتْ مَنِيَّتُهُ قَلَّتْ بَوَاكِيهِ قَلَّ تُرَاثُهُ)) الترمذي (وكذلك  أحمد وابن ماجه ) وإسناده حسن



Kutoka kwa Abu Umaamah رضي الله عنه      kwambe Mtume صلى الله عليه وسلم   amesema: (([Allah Amesema}] Kwa kweli katika wale wanaoniabudu, Ninayempenda zaidi ni yule muuminu lofa, mwenye Swalah nyingi mwenye kujitahidi kumuabudu Mola wake kwa siri (bila ya kujionyesha kwa watu), ambaye si maarufu kwa watu, na wala hatajiki, na ambaye hali yake ya maisha ni duni lakini anaistahamili hali hiyo)) Tena hapo صلى الله عليه وسلم  akasema: ((Kama mauti yangekuwa mapema kwake asingekuwa na watu wengi wa kumlilia, na urithi wake ungelikuwa mdogo sana))  [ At-Tirmidhiy (vilevile Ahmad  na Ibn Maajah) Mapokezi yake ni mazuri]