Kujipanga Safu Wakisali Wanawake na Wanaume



Jinsi ya Kujipanga Safu Wakisali Wanaume na Wanawake kwa Pamoja.


Watakaposali wanawake na wanaume sala ya jamaa pamoja (na kama kuna na watoto ) ikiwa ni nyumbani au msikitini basi mistari  (safu) za mwanzo zitatakiwa ziwe za wanaume kisha zifuate za watoto wa kiume kama wapo na mwisho zije safu za wanawake.

Kwa mujibu wa hadithi ya Mtume (Salla Allahu ‘Alayhi Wasallam) iliyosimuliwa na Bukhari na Muslim na kupokelewa na Anas bin Malik Allah amuwie radhi kwamba :

Bibi yake anas alimualika Mtume (Salla Allahu ‘Alayhi Wasallam) kwa ajili ya chakula alichomuandalia. Mtume (Salla Allahu ‘Alayhi Wasallam) akala kidogo kisha akasema : simameni nikuongozeni kwenye sala. Anas akasema: Nikaenda kuchukua msala wetu ambao tayari umejaa weusi(kwa kutumika sana) nikauchurizia maji kuusafisha . Kisha Mtume(Salla Allahu ‘Alayhi Wasallam) akasimama na (alikuwepo ) yatima na mimi tukasimama nyuma yake na bibi akasimama nyuma yetu Na Mtume(Salla Allahu ‘Alayhi Wasallam) Akatusalisha rakaa mbili kisha akaondoka.

Na  kwa mujibu wa hadithi nyengine ya Mtume(Salla Allahu ‘Alayhi Wasallam)

  قال صلى الله عليه وآله وسلم (( خَيْرُ صُفُوف الرَّجْلُ أَوَّلُهَا وَشَرُّهَا أَخِرُهَا وَخَيْر صُفُوف النِّسَاء  أَخِرُهَا  وَشَرُّهَا    أَوَّلُهَا )) رواه مسلم
Amesema Mtume (Salla Allahu ‘Alayhi Wasallam)   katika  hadithi iliyosimuliwa na Abu Hurayrah, Allah amuwie radhi:

“Safu iliyo bora kwa wanaume ni ile ya mwanzo na safu iliyo mbaya ni ile ya mwisho, Na bora ya safu (ya sala) kwa mwanamke ni ile ya mwisho na iliyo mbaya ni ile ya mwanzo”
                                               Imesimuliwa na   Muslim

Na ikiwa kama wanawake wanasali na wanaume kwenye sehemu kama msikiti au  kwenye ukumbi (hall) na ukuta au kizuizi ndio kinachowatenganisha lakini wanasali kama bega kwa bega pia sala hii ni sahihi almuradi kuna kitu kinawatenganisha lakini inavyotakikana kiutaratibu safu hizi ziwe nyuma ya safu za wanaume .

Wallahu Aalamu