سُورَةُ الْمُرْسَلاَت
Al-Mursalaat (77)
بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ
وَالْمُرْسَلَاتِ عُرْفًا ﴿١﴾
|
1. Naapa kwa pepo zitumwazo moja baada ya moja. |
فَالْعَاصِفَاتِ عَصْفًا ﴿٢﴾
|
2. Kisha (Naapa) kwa pepo zinazovuma kwa dhoruba. |
وَالنَّاشِرَاتِ نَشْرًا ﴿٣﴾
|
3. Na (Naapa) kwa pepo zinazotawanya (mawingu na mvua) mtawanyiko. |
فَالْفَارِقَاتِ فَرْقًا ﴿٤﴾
|
4. Na (Naapa) kwa (Malaika) wanaopambanua mpambanuo. |
فَالْمُلْقِيَاتِ ذِكْرًا ﴿٥﴾
|
5. Kisha (Naapa) kwa (Malaika) wanaopeleka dhikri (maneno ya Allaah). |
عُذْرًا أَوْ نُذْرًا ﴿٦﴾
|
6. Kwa udhuru au kuonya. |
إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَوَاقِعٌ ﴿٧﴾
|
7. Hakika yale mliyoahidiwa bila shaka yatatokea tu! |
فَإِذَا النُّجُومُ طُمِسَتْ ﴿٨﴾
|
8. Pale nyota zitakapofutwa (mwanga wake). |
وَإِذَا السَّمَاءُ فُرِجَتْ ﴿٩﴾
|
9. Na (pale) mbingu zitakapopasuliwa. |
وَإِذَا الْجِبَالُ نُسِفَتْ ﴿١٠﴾
|
10. Na (pale) majabali yatakapong’olewa. |
وَإِذَا الرُّسُلُ أُقِّتَتْ ﴿١١﴾
|
11. Na (pale) Rasuli watakapopangwa kwa ratiba (wakati wake maalumu). |
لِأَيِّ يَوْمٍ أُجِّلَتْ ﴿١٢﴾
|
12. Kwa siku gani hiyo iliyokawilishwa? |
لِيَوْمِ الْفَصْلِ ﴿١٣﴾
|
13. Kwa ajili ya siku ya hukumu. |
وَمَا أَدْرَاكَ مَا يَوْمُ الْفَصْلِ ﴿١٤﴾
|
14. Na nini kitakachokujulisha siku ya hukumu? |
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ ﴿١٥﴾
|
15. Ole siku hiyo (ya Qiyaamah) kwa wakadhibishaji. |
أَلَمْ نُهْلِكِ الْأَوَّلِينَ ﴿١٦﴾
|
16. Je, kwani Hatukuangamiza (watu wa) awali? |
ثُمَّ نُتْبِعُهُمُ الْآخِرِينَ ﴿١٧﴾
|
17. Kisha Tukawafuatilishia wengineo? |
كَذَٰلِكَ نَفْعَلُ بِالْمُجْرِمِينَ ﴿١٨﴾
|
18. Hivyo ndivyo Tutakavyowafanya wakhalifu. |
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ ﴿١٩﴾
|
19. Ole siku hiyo (ya Qiyaamah) kwa wakadhibishaji. |
أَلَمْ نَخْلُقكُّم مِّن مَّاءٍ مَّهِينٍ ﴿٢٠﴾
|
20. Je, kwani Hatukukuumbeni kwa maji dhalilifu (manii)? |
فَجَعَلْنَاهُ فِي قَرَارٍ مَّكِينٍ ﴿٢١﴾
|
21. Kisha Tukayaweka katika mahali pa utulivu. |
إِلَىٰ قَدَرٍ مَّعْلُومٍ ﴿٢٢﴾
|
22. Mpaka kadirio maalumu. |
فَقَدَرْنَا فَنِعْمَ الْقَادِرُونَ ﴿٢٣﴾
|
23. Tukakadiria, basi ni wazuri walioje (Sisi) Wakadiriaji. |
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ ﴿٢٤﴾
|
24. Ole siku hiyo (ya Qiyaamah) kwa wakadhibishaji. |
أَلَمْ نَجْعَلِ الْأَرْضَ كِفَاتًا ﴿٢٥﴾
|
25. Je, kwani Hatukufanya ardhi kuwa ni chombo cha kukusanya? |
أَحْيَاءً وَأَمْوَاتًا ﴿٢٦﴾
|
26. (Kukusanya) Vilivyo hai na wafu? |
وَجَعَلْنَا فِيهَا رَوَاسِيَ شَامِخَاتٍ وَأَسْقَيْنَاكُم مَّاءً فُرَاتًا ﴿٢٧﴾
|
27. Na Tukaweka humo milima mirefu thabiti, na Tukakunywesheni maji matamu? |
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ ﴿٢٨﴾
|
28. Ole siku hiyo (ya Qiyaamah) kwa wakadhibishaji. |
انطَلِقُوا إِلَىٰ مَا كُنتُم بِهِ تُكَذِّبُونَ ﴿٢٩﴾
|
29. (Wataambiwa): “Nendeni kwenye yale mliyokuwa mkiyakadhibisha. |
انطَلِقُوا إِلَىٰ ظِلٍّ ذِي ثَلَاثِ شُعَبٍ ﴿٣٠﴾
|
30. “Nendeni kwenye kivuli chenye sehemu tatu.” |
لَّا ظَلِيلٍ وَلَا يُغْنِي مِنَ اللَّـهَبِ ﴿٣١﴾
|
31. (Kivuli hicho) hakiwafuniki, na wala hakiwakingi na mwako wa Moto. |
إِنَّهَا تَرْمِي بِشَرَرٍ كَالْقَصْرِ ﴿٣٢﴾
|
32. Hakika (huo Moto) hurusha macheche (makubwa na marefu) kama makasri. |
كَأَنَّهُ جِمَالَتٌ صُفْرٌ ﴿٣٣﴾
|
33. Kama kwamba ngamia wa rangi ya manjano. |
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ ﴿٣٤﴾
|
34. Ole siku hiyo (ya Qiyaamah) kwa wakadhibishaji. |
هَـٰذَا يَوْمُ لَا يَنطِقُونَ ﴿٣٥﴾
|
35. Siku hii hawatotamka. |
وَلَا يُؤْذَنُ لَهُمْ فَيَعْتَذِرُونَ ﴿٣٦﴾
|
36. Na wala hawatopewa idhini, ili watoe nyudhuru. |
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ ﴿٣٧﴾
|
37. Ole siku hiyo (ya Qiyaamah) kwa wakadhibishaji. |
هَـٰذَا يَوْمُ الْفَصْلِ ۖ جَمَعْنَاكُمْ وَالْأَوَّلِينَ ﴿٣٨﴾
|
38. Hii ni siku ya hukumu. Tumekukusanyeni pamoja na (watu) wa awali. |
فَإِن كَانَ لَكُمْ كَيْدٌ فَكِيدُونِ ﴿٣٩﴾
|
39. Ikiwa mnayo njama yoyote ile basi Nifanyieni. |
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ ﴿٤٠﴾
|
40. Ole siku hiyo (ya Qiyaamah) kwa wakadhibishaji. |
إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي ظِلَالٍ وَعُيُونٍ ﴿٤١﴾
|
41. Hakika wenye taqwa wamo katika vivuli na chemchemu. |
وَفَوَاكِهَ مِمَّا يَشْتَهُونَ ﴿٤٢﴾
|
42. Na (kila aina ya) matunda katika yale wanayoyatamani. |
كُلُوا وَاشْرَبُوا هَنِيئًا بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ﴿٤٣﴾
|
43. (Wataambiwa): “Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa sababu ya yale mliyokuwa mkiyatenda.” |
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ ﴿٤٤﴾
|
44. Hakika hivyo ndivyo Tunavyowalipa watendao wema. |
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ ﴿٤٥﴾
|
45. Ole siku hiyo (ya Qiyaamah) kwa wakadhibishaji. |
كُلُوا وَتَمَتَّعُوا قَلِيلًا إِنَّكُم مُّجْرِمُونَ ﴿٤٦﴾
|
46. (Makafiri nao wataambiwa): “Kuleni na stareheni kidogo (hapa duniani), hakika nyinyi ni wahalifu.” |
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ ﴿٤٧﴾
|
47. Ole siku hiyo (ya Qiyaamah) kwa wakadhibishaji. |
وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ ارْكَعُوا لَا يَرْكَعُونَ ﴿٤٨﴾
|
48. Na (walikuwa duniani) wakiambiwa “Rukuuni (Swalini),” hawakuwa wakirukuu. |
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ ﴿٤٩﴾
|
49. Ole siku hiyo (ya Qiyaamah) kwa wakadhibishaji. |
فَبِأَيِّ حَدِيثٍ بَعْدَهُ يُؤْمِنُونَ ﴿٥٠﴾
|
50. Basi hadiyth gani baada ya hii (Qur-aan) wataiamini?
Ukitaka kusoma Sura nyengine Rejeauliko toka
Ukiwa una shauri au maelezo juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii falhaqqiy@gmail.com |