سُورَةُ الْفَلَقْ
Al-Falaq (113)
(Imeteremka Makka)
Sura hii inamtaka Nabii s.a.w. amwendee Mola wake Mlezi atake ulinzi kwake
kujilinda na shari ya kila mwenye shari, ya viumbe vyake, na shari za usiku
linapo ingia giza, yanayo yasibu nafsi katika hali ya upweke, na madhara
ambayo mtu hawezi kujikinga nayo, na shari za mafisadi wanao pita kuharibu
makhusiano na mawasiliano yalio baina ya watu, na shari za hasidi anaye
tamani kuondoa neema alizo wapa Mwenyezi Mungu waja wake.
قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ الْفَلَقِ ﴿١﴾
|
1. Sema: “Najikinga na Rabb (Mola) wa mapambazuko. |
مِن شَرِّ مَا خَلَقَ ﴿٢﴾
|
2. “Kutokana na shari ya Alivyoviumba. |
وَمِن شَرِّ غَاسِقٍ إِذَا وَقَبَ ﴿٣﴾
|
3. “Na kutokana na shari ya giza linapoingia. |
وَمِن شَرِّ النَّفَّاثَاتِ فِي الْعُقَدِ ﴿٤﴾
|
4. “Na kutokana na shari ya wanaopuliza mafundoni. |
وَمِن شَرِّ حَاسِدٍ إِذَا حَسَدَ ﴿٥﴾
|
5. Na kutokana na shari ya hasidi anapohusudu.
Ukitaka kusoma Sura nyengine Rejeauliko toka
Ukiwa una shauri au maelezo juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii falhaqqiy@gmail.com |