Al-Maaidah: 5

الْمَائِدَة
Al-Maaidah: 5

(Imeteremka Madina)


Hii Sura ya Madina. Idadi za Aya zake ni 120. Na hii ni katika Sura zilizo shuka karibu na mwisho. Humu umebainishwa waajibu wa kutimiza maagano, sawa yakiwa baina ya mja na Mola wake Mlezi, au baina ya watu wenyewe kwa wenyewe. Na Sura hii imebainisha baadhi ya vyakula vilivyo harimishwa, kama ilivyo bainisha vilivyo halali, na kuhalalisha kuwaoa wanawake wa Ahlil Kitabi, Wakristo na Mayahudi. Zimetajwa pia humu nguzo za udhu na kutayamamu. Kadhaalika imeelezwa kutakikana kufanya uadilifu na adui. Na Sura hii imeashiria neema za Mwenyezi Mungu juu ya Waislamu, na waajibu wao kukihifadhi Kitabu chao, na ikaelezea kuwa Mayahudi wameyatengua maneno kutokana na pahala pake, na Wakristo wakayasahau baadhi ya mambo waliyo kumbushwa, na kwamba wao wamekufuru kwa kusema kwao kuwa Masihi ni mwana wa Mungu. Kadhaalika Sura hii inawakanusha Mayahudi na Wakristo kwa yale madai yao kwamba ati wao ni wana wa Mungu na vipenzi vyake. Kisha tena Sura hii imekusanya baadhi ya khabari za Mayahudi, kama ilivyo kusanya  kisa cha wana wawili wa Adam. Kisa hichi kinathibitisha kuwa uvamizi na kudhulumiana ni katika tabia za kibinaadamu. Tena kuwajibika kumtoza kisasi mwenye kudhulumu ni njia ya kuidhibiti tabia hii mbovu isivuke mpaka! Na Sura Al Maidah imeeleza adhabu ya kumtia adabu mwenye kufanya fiski na wizi. Tena baadae ikarejea kubainisha vipi Mayahudi walivyo pindua hukumu za sharia zilizo kuwamo katika Taurati, na ikabainisha kwamba katika Taurati na Injili ulikuwapo ukweli na haki kabla ya kuchezewa na kugeuzwa geuzwa. Na ikahakikishwa kuwa ni waajibu kuhukumu kwa mujibu alivyo teremsha Mwenyezi Mungu. Sura imeashiria juu ya uadui wa Mayahudi na Wakristo kwa Waumini, na waajibu wa kutowanyenyekea, na kutowaridhia kwa wanayo tenda, na kuwa ni dharura kuwapinga. Na Sura imethibitisha kuwa Wakristo wamekufuru kwa kusema kwao Mwenyezi Mungu ni mmoja wa Watatu! Tena Qur'an katika Sura hii imewasifu baadhi ya Wakristo ambao wameikubali haki na wakaiamini, na ikamkataza Muumini kujiharimishia mwenyewe vitu vizuri, na ikabainisha nini kafara ya kuvunja kiapo. Sura hii kadhaalika imeharimisha ulevi kabisa, na imebainisha ibada za Hija na cheo cha Alkaaba na miezi mitakatifu, na ikaeleza upotovu wa baadhi ya mambo waliyo jiharimishia Waarabu wenyewe kwa wenyewe bila ya hoja wala dalili yoyote, kama ilivyo bainisha wasia wakati wa safari.  Mwishoe Sura hii imekhitimisha kwa kutaja miujiza iliyo tokea kwa Nabii Isa a.s. Na juu ya hiyo miujiza Banu Israili walimkanya. Pia Sura imetaja kuwa Nabii Isa a.s. hana dhambi ya walio potoka wakamuabudu, na imeeleza Ufalme wa Mwenyezi Mungu Subhanahu juu ya mbingu na ardhi, na ukamilifu wa uwezo wake. 



بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ

 يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا أَوْفُوا بِالْعُقُودِ ۚ أُحِلَّتْ لَكُم بَهِيمَةُ الْأَنْعَامِ إِلَّا مَا يُتْلَىٰ عَلَيْكُمْ غَيْرَ مُحِلِّي الصَّيْدِ وَأَنتُمْ حُرُمٌ ۗ إِنَّ اللَّـهَ يَحْكُمُ مَا يُرِيدُ ﴿١﴾
1. Enyi mlioamini! Timizeni mikataba. Imehalalishwa kwenu wanyama wa mifugo wanaopelekwa malishoni, isipokuwa mnaosomewa (humu) - kuwinda imeharamishwa (pia) mkiwa katika Ihraam. Hakika Allaah Anahukumu Atakayo.


يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تُحِلُّوا شَعَائِرَ اللَّـهِ وَلَا الشَّهْرَ الْحَرَامَ وَلَا الْهَدْيَ وَلَا الْقَلَائِدَ وَلَا آمِّينَ الْبَيْتَ الْحَرَامَ يَبْتَغُونَ فَضْلًا مِّن رَّبِّهِمْ وَرِضْوَانًا ۚ وَإِذَا حَلَلْتُمْ فَاصْطَادُوا ۚ وَلَا يَجْرِمَنَّكُمْ شَنَآنُ قَوْمٍ أَن صَدُّوكُمْ عَنِ الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ أَن تَعْتَدُوا ۘ وَتَعَاوَنُوا عَلَى الْبِرِّ وَالتَّقْوَىٰ ۖ وَلَا تَعَاوَنُوا عَلَى الْإِثْمِ وَالْعُدْوَانِ ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ ۖ إِنَّ اللَّـهَ شَدِيدُ الْعِقَابِ ﴿٢﴾
2. Enyi mlioamini!  Msihalifu kaida za Dini (na maharamisho) ya Allaah, wala (taadhima) ya miezi mitukufu wala (kupuuza alama za) wanyama wanaopelekwa kuchinjwa (Makkah), wala vigwe (vyao), wala (kuhalifu amani kwa) wanaoiendea Al-Baytal-Haraam wanatafuta (huko) fadhila kutoka kwa Rabb (Mola) wao na Radhi (Zake). Na mkishatoka kwenye Ihraam windeni (mkitaka). Na wala isikuchocheeni chuki ya watu kwa vile walikuzuieni (kufika) Al-Masjidil-Haraam (kusikupelekeeni) kutaadi. Shirikianeni katika wema na taqwa, na wala msishirikiane katika dhambi na uadui. Na Mcheni Allaah; hakika Allaah ni Mkali wa kuakibu.


حُرِّمَتْ عَلَيْكُمُ الْمَيْتَةُ وَالدَّمُ وَلَحْمُ الْخِنزِيرِ وَمَا أُهِلَّ لِغَيْرِ اللَّـهِ بِهِ وَالْمُنْخَنِقَةُ وَالْمَوْقُوذَةُ وَالْمُتَرَدِّيَةُ وَالنَّطِيحَةُ وَمَا أَكَلَ السَّبُعُ إِلَّا مَا ذَكَّيْتُمْ وَمَا ذُبِحَ عَلَى النُّصُبِ وَأَن تَسْتَقْسِمُوا بِالْأَزْلَامِ ۚ ذَٰلِكُمْ فِسْقٌ ۗ الْيَوْمَ يَئِسَ الَّذِينَ كَفَرُوا مِن دِينِكُمْ فَلَا تَخْشَوْهُمْ وَاخْشَوْنِ ۚ الْيَوْمَ أَكْمَلْتُ لَكُمْ دِينَكُمْ وَأَتْمَمْتُ عَلَيْكُمْ نِعْمَتِي وَرَضِيتُ لَكُمُ الْإِسْلَامَ دِينًا ۚ فَمَنِ اضْطُرَّ فِي مَخْمَصَةٍ غَيْرَ مُتَجَانِفٍ لِّإِثْمٍ ۙ فَإِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ﴿٣﴾
3. Mmeharamishiwa nyamafu (mzoga), na damu, na nyama ya nguruwe, na kilichotajiwa katika kuchinjwa kwake asiyekuwa Allaah. Na (mnyama aliyeuawa) kwa kunyongwa, na (aliyekufa kwa) kupigwa, na (aliyekufa kwa) kuporomoka, na (aliyekufa kwa) kupigwa pembe (na mnyama mwengine), na aliyeliwa na mnyama mwitu (akafa) isipokuwa mliyewahi kumchinja (kihalali kabla ya kufa kwake); na (pia mmeharamishiwa) waliochinjwa kwa ajili ya mizimu, na (pia mmeharamishiwa) kupiga ramli kutokana na mishale. Hayo kwenu ni ufasiki. Leo wamekata tamaa (kabisa) wale waliokufuru katika Dini yenu; basi msiwaogope, na Niogopeni (Mimi). Leo Nimekukamilishieni Dini (yenu), na Nimekutimizieni neema Yangu, na Nimekuridhieni kwenu Uislamu uwe (ndio) Dini yenu. Basi atakayefikwa na dharura na kushurutishwa kutokana na njaa kali (ikampelekea kula vilivyoharamishwa), pasipo kuelekea dhambi; basi hakika Allaah ni Ghafuwrur-Rahiym (Mwingi wa kughufuria - Mwenye kurehemu).

يَسْأَلُونَكَ مَاذَا أُحِلَّ لَهُمْ ۖ قُلْ أُحِلَّ لَكُمُ الطَّيِّبَاتُ ۙ وَمَا عَلَّمْتُم مِّنَ الْجَوَارِحِ مُكَلِّبِينَ تُعَلِّمُونَهُنَّ مِمَّا عَلَّمَكُمُ اللَّـهُ ۖ فَكُلُوا مِمَّا أَمْسَكْنَ عَلَيْكُمْ وَاذْكُرُوا اسْمَ اللَّـهِ عَلَيْهِ ۖ وَاتَّقُوا اللَّـهَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ سَرِيعُ الْحِسَابِ﴿٤﴾
4. Wanakuuliza (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) wamehalalishiwa nini? Sema: “Mmehalalishiwa vizuri na mlichowafunza wanyama (kukiwinda) na ndege wa kuwinda; mnawafunza yale Aliyokufunzeni Allaah. Basi kuleni walichokukamatieni, na mkitajie Jina la Allaah. Na mcheni Allaah; hakika Allaah ni Mwepesi wa kuhesabu.


الْيَوْمَ أُحِلَّ لَكُمُ الطَّيِّبَاتُ ۖ وَطَعَامُ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ حِلٌّ لَّكُمْ وَطَعَامُكُمْ حِلٌّ لَّهُمْ ۖ وَالْمُحْصَنَاتُ مِنَ الْمُؤْمِنَاتِ وَالْمُحْصَنَاتُ مِنَ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ مِن قَبْلِكُمْ إِذَا آتَيْتُمُوهُنَّ أُجُورَهُنَّ مُحْصِنِينَ غَيْرَ مُسَافِحِينَ وَلَا مُتَّخِذِي أَخْدَانٍ ۗ وَمَن يَكْفُرْ بِالْإِيمَانِ فَقَدْ حَبِطَ عَمَلُهُ وَهُوَ فِي الْآخِرَةِ مِنَ الْخَاسِرِينَ﴿٥﴾
5. Leo mmehalalishiwa vizuri. Na chakula cha wale waliopewa Kitabu ni halaal kwenu, na chakula chenu ni halaal kwao. Na (mmehalalishwa kuwaoa) wanawake walioimarisha sitara (wasiozini) miongoni mwa Waumini wanawake na (pia mmehalalishiwa kuwaoa) wanawake walioimarisha sitara (wasiozini) miongoni mwa wale waliopewa Kitabu kabla yenu; mtakapowapa mahari yao mkafunga nao ndoa bila ya kufanya uhasharati wala kuchukua hawara. Na yeyote atakayekufuru iymaan; basi kwa yakini zimebatilika ‘amali zake; naye Aakhirah atakuwa miongoni mwa waliokhasirika.

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا قُمْتُمْ إِلَى الصَّلَاةِ فَاغْسِلُوا وُجُوهَكُمْ وَأَيْدِيَكُمْ إِلَى الْمَرَافِقِ وَامْسَحُوا بِرُءُوسِكُمْ وَأَرْجُلَكُمْ إِلَى الْكَعْبَيْنِ ۚ وَإِن كُنتُمْ جُنُبًا فَاطَّهَّرُوا ۚ وَإِن كُنتُم مَّرْضَىٰ أَوْ عَلَىٰ سَفَرٍ أَوْ جَاءَ أَحَدٌ مِّنكُم مِّنَ الْغَائِطِ أَوْ لَامَسْتُمُ النِّسَاءَ فَلَمْ تَجِدُوا مَاءً فَتَيَمَّمُوا صَعِيدًا طَيِّبًا فَامْسَحُوا بِوُجُوهِكُمْ وَأَيْدِيكُم مِّنْهُ ۚ مَا يُرِيدُ اللَّـهُ لِيَجْعَلَ عَلَيْكُم مِّنْ حَرَجٍ وَلَـٰكِن يُرِيدُ لِيُطَهِّرَكُمْ وَلِيُتِمَّ نِعْمَتَهُ عَلَيْكُمْ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ﴿٦﴾
6. Enyi mlioamini!  Mnaposimama kwa ajili ya Swalaah; osheni nyuso zenu na mikono yenu mpaka kwenye visugudi, na panguseni kwa (kupaka maji) vichwa vyenu na (osheni) miguu yenu hadi vifundoni. Na mkiwa na janaba basi jitwaharisheni. Na mkiwa wagonjwa (maji yanawadhuru) au mko safarini au mmoja wenu akitoka msalani, au mmewagusa (kwa matamanio au mmejamiiana na) wanawake, kisha hamkupata maji; basi mtayammamu (ikusudieni ardhi), panguseni kwayo nyuso zenu na mikono yenu. Allaah Hataki kukufanyieni magumu, lakini Anataka kukutwaharisheni na Akutimizieni neema Yake juu yenu ili mpate kushukuru.


وَاذْكُرُوا نِعْمَةَ اللَّـهِ عَلَيْكُمْ وَمِيثَاقَهُ الَّذِي وَاثَقَكُم بِهِ إِذْ قُلْتُمْ سَمِعْنَا وَأَطَعْنَا ۖ وَاتَّقُوا اللَّـهَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ عَلِيمٌ بِذَاتِ الصُّدُورِ﴿٧﴾
7. Na kumbukeni neema ya Allaah juu yenu na fungamano Lake ambalo Amekufungamanisheni nalo mliposema: “Tumesikia na Tumetii.” Na mcheni Allaah; hakika Allaah ni ‘Aliym (Mjuzi) kwa yaliyomo vifuani.


يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُونُوا قَوَّامِينَ لِلَّـهِ شُهَدَاءَ بِالْقِسْطِ ۖ وَلَا يَجْرِمَنَّكُمْ شَنَآنُ قَوْمٍ عَلَىٰ أَلَّا تَعْدِلُوا ۚ اعْدِلُوا هُوَ أَقْرَبُ لِلتَّقْوَىٰ ۖ وَاتَّقُوا اللَّـهَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ خَبِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ﴿٨﴾
8. Enyi mlioamini!  Kuweni wasimamizi madhubuti kwa ajili ya Allaah mkitoa ushahidi kwa uadilifu. Na wala chuki ya watu isikuchocheeni kutokufanya uadilifu. Fanyeni uadilifu; hivyo ni karibu zaidi na taqwa. Na mcheni Allaah; hakika Allaah Khabiyr (Mjuzi wa yaliyodhahiri na yaliyofichikana) kwa myatendayo.

وَعَدَ اللَّـهُ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ ۙ لَهُم مَّغْفِرَةٌ وَأَجْرٌ عَظِيمٌ﴿٩﴾
9. Allaah Amewaahidi wale walioamini na wakatenda mema; (kwamba) watapata maghfirah na ujira adhimu.

وَالَّذِينَ كَفَرُوا وَكَذَّبُوا بِآيَاتِنَا أُولَـٰئِكَ أَصْحَابُ الْجَحِيمِ﴿١٠﴾
10. Na waliokufuru na wakakadhibisha Aayaat (na ishara, dalili n.k) Zetu, hao ni watu wa (Moto wa) Al-Jahiym.

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اذْكُرُوا نِعْمَتَ اللَّـهِ عَلَيْكُمْ إِذْ هَمَّ قَوْمٌ أَن يَبْسُطُوا إِلَيْكُمْ أَيْدِيَهُمْ فَكَفَّ أَيْدِيَهُمْ عَنكُمْ ۖ وَاتَّقُوا اللَّـهَ ۚ وَعَلَى اللَّـهِ فَلْيَتَوَكَّلِ الْمُؤْمِنُونَ﴿١١﴾
11. Enyi mlioamini! Kumbukeni neema ya Allaah juu yenu, pale walipopania watu kunyosheeni mikono yao (kukushambulieni), kisha Allaah Akazuia mikono yao kutoka kwenu (kukufikieni). Na mcheni Allaah; na kwa Allaah pekee watawakali Waumini.


وَلَقَدْ أَخَذَ اللَّـهُ مِيثَاقَ بَنِي إِسْرَائِيلَ وَبَعَثْنَا مِنْهُمُ اثْنَيْ عَشَرَ نَقِيبًا ۖ وَقَالَ اللَّـهُ إِنِّي مَعَكُمْ ۖ لَئِنْ أَقَمْتُمُ الصَّلَاةَ وَآتَيْتُمُ الزَّكَاةَ وَآمَنتُم بِرُسُلِي وَعَزَّرْتُمُوهُمْ وَأَقْرَضْتُمُ اللَّـهَ قَرْضًا حَسَنًا لَّأُكَفِّرَنَّ عَنكُمْ سَيِّئَاتِكُمْ وَلَأُدْخِلَنَّكُمْ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ ۚ فَمَن كَفَرَ بَعْدَ ذَٰلِكَ مِنكُمْ فَقَدْ ضَلَّ سَوَاءَ السَّبِيلِ﴿١٢﴾
12. Na kwa yakini Allaah Alichukua fungamano la wana wa Israaiyl na Tukawapelekea miongoni mwao wakuu kumi na mbili. Na Allaah Akasema: “Hakika Mimi Niko pamoja nanyi; mtakaposimamisha Swalaah, na kutoa Zakaah, na kuamini Rasuli Wangu, na kuwaunga mkono, na kumkopesha Allaah mkopo mzuri; bila shaka Nitakufutieni maovu yenu, na Nitakuingizeni Jannaat zipitazo chini yake mito. Na yeyote atakayekufuru baada ya hapo miongoni mwenu; basi kwa yakini amepotea njia iliyo sawa.”

فَبِمَا نَقْضِهِم مِّيثَاقَهُمْ لَعَنَّاهُمْ وَجَعَلْنَا قُلُوبَهُمْ قَاسِيَةً ۖ يُحَرِّفُونَ الْكَلِمَ عَن مَّوَاضِعِهِ ۙ وَنَسُوا حَظًّا مِّمَّا ذُكِّرُوا بِهِ ۚ وَلَا تَزَالُ تَطَّلِعُ عَلَىٰ خَائِنَةٍ مِّنْهُمْ إِلَّا قَلِيلًا مِّنْهُمْ ۖ فَاعْفُ عَنْهُمْ وَاصْفَحْ ۚ إِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ الْمُحْسِنِينَ﴿١٣﴾
13. Kwa (sababu ya) kuvunja kwao fungamano lao, Tuliwalaani na Tukazifanya nyoyo zao kuwa ngumu. Wanageuza maneno (ya Allaah) kutoka mahali pake, na wakasahu sehemu ya yale waliyokumbushwa kwayo. Na utaendelea kupata (habari za) khiana kutoka kwao isipokuwa wachache miongoni mwao. Basi wasamehe na achilia mbali (maudhi yao). Hakika Allaah Anapenda wafanyao ihsaan.


وَمِنَ الَّذِينَ قَالُوا إِنَّا نَصَارَىٰ أَخَذْنَا مِيثَاقَهُمْ فَنَسُوا حَظًّا مِّمَّا ذُكِّرُوا بِهِ فَأَغْرَيْنَا بَيْنَهُمُ الْعَدَاوَةَ وَالْبَغْضَاءَ إِلَىٰ يَوْمِ الْقِيَامَةِ ۚ وَسَوْفَ يُنَبِّئُهُمُ اللَّـهُ بِمَا كَانُوا يَصْنَعُونَ﴿١٤﴾
14. Na kwa wale waliosema: “Hakika sisi ni Naswaaraa” Tulichukua fungamano lao, wakasahau sehemu ya yale waliyokumbushwa kwayo. Basi Tukapandikiza baina yao uadui na bughudha mpaka Siku ya Qiyaamah. Na Allaah Atawajulisha waliyokuwa wakiyatenda.

يَا أَهْلَ الْكِتَابِ قَدْ جَاءَكُمْ رَسُولُنَا يُبَيِّنُ لَكُمْ كَثِيرًا مِّمَّا كُنتُمْ تُخْفُونَ مِنَ الْكِتَابِ وَيَعْفُو عَن كَثِيرٍ ۚ قَدْ جَاءَكُم مِّنَ اللَّـهِ نُورٌ وَكِتَابٌ مُّبِينٌ﴿١٥﴾
15. Enyi Ahlal-Kitaab! Hakika amekwishakujieni Rasuli Wetu anayekubainishieni mengi katika yale mliyokuwa mkiyaficha katika Kitabu, na anasamehe mengi. Kwa yakini imekufikieni kutoka kwa Allaah nuru na Kitabu bayana.

يَهْدِي بِهِ اللَّـهُ مَنِ اتَّبَعَ رِضْوَانَهُ سُبُلَ السَّلَامِ وَيُخْرِجُهُم مِّنَ الظُّلُمَاتِ إِلَى النُّورِ بِإِذْنِهِ وَيَهْدِيهِمْ إِلَىٰ صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ﴿١٦﴾
16. Allaah Anamwongoza kwacho yeyote atayefuata Radhi Zake katika njia za salama; na Anawatoa katika viza kuingia katika nuru kwa idhini Yake, na Anawaongoza kuelekea njia iliyonyooka.


لَّقَدْ كَفَرَ الَّذِينَ قَالُوا إِنَّ اللَّـهَ هُوَ الْمَسِيحُ ابْنُ مَرْيَمَ ۚ قُلْ فَمَن يَمْلِكُ مِنَ اللَّـهِ شَيْئًا إِنْ أَرَادَ أَن يُهْلِكَ الْمَسِيحَ ابْنَ مَرْيَمَ وَأُمَّهُ وَمَن فِي الْأَرْضِ جَمِيعًا ۗ وَلِلَّـهِ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا ۚ يَخْلُقُ مَا يَشَاءُ ۚ وَاللَّـهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ﴿١٧﴾
17. Kwa yakini, wamekufuru wale waliosema: “Hakika Allaah Ndiye Al-Masiyh mwana wa Maryam.” Sema: “Nani anayemiliki chochote mbele ya Allaah, Akitaka kumhilikisha Al-Masiyh mwana wa Maryam na mama yake na walioko ardhini wote? Na ufalme ni wa Allaah Pekee wa mbingu na ardhi na vyote vilivyo baina yake, Anaumba Atakacho. Na Allaah juu ya kila kitu ni Qadiyr (Muweza).


وَقَالَتِ الْيَهُودُ وَالنَّصَارَىٰ نَحْنُ أَبْنَاءُ اللَّـهِ وَأَحِبَّاؤُهُ ۚ قُلْ فَلِمَ يُعَذِّبُكُم بِذُنُوبِكُم ۖ بَلْ أَنتُم بَشَرٌ مِّمَّنْ خَلَقَ ۚ يَغْفِرُ لِمَن يَشَاءُ وَيُعَذِّبُ مَن يَشَاءُ ۚ وَلِلَّـهِ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا ۖ وَإِلَيْهِ الْمَصِيرُ﴿١٨﴾
18. Na Mayahudi na Manaswara wamesema: “Sisi ni wana wa Allaah na vipenzi Vyake.” Sema: “Kwa nini basi Anakuadhibuni kwa dhambi zenu? Bali nyinyi ni watu miongoni mwa Alioumba. Anamghufuria Amtakaye na Anamuadhibu Amtakaye. Na ufalme ni wa Allaah Pekee wa mbingu na ardhi na vyote vilivyo baina yake na Kwake Pekee ndio mahali pa kuishia.

يَا أَهْلَ الْكِتَابِ قَدْ جَاءَكُمْ رَسُولُنَا يُبَيِّنُ لَكُمْ عَلَىٰ فَتْرَةٍ مِّنَ الرُّسُلِ أَن تَقُولُوا مَا جَاءَنَا مِن بَشِيرٍ وَلَا نَذِيرٍ ۖ فَقَدْ جَاءَكُم بَشِيرٌ وَنَذِيرٌ ۗ وَاللَّـهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ﴿١٩﴾
19. Enyi Ahlal-Kitaab! Kwa yakini amekwishakujieni Rasuli Wetu anaekubainishieni (Dini) katika kipindi cha kusita (kisichokuwa) na Rasuli. Msije kusema: “Hakutujia mbashiriaji yeyote wala mwonyaji”. Kwa yakini amekujieni mbashiriaji na mwonyaji. Na Allaah juu ya kila kitu ni Qadiyr (Muweza).

وَإِذْ قَالَ مُوسَىٰ لِقَوْمِهِ يَا قَوْمِ اذْكُرُوا نِعْمَةَ اللَّـهِ عَلَيْكُمْ إِذْ جَعَلَ فِيكُمْ أَنبِيَاءَ وَجَعَلَكُم مُّلُوكًا وَآتَاكُم مَّا لَمْ يُؤْتِ أَحَدًا مِّنَ الْعَالَمِينَ﴿٢٠﴾
20. Na (taja ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) pale Muwsaa alipoambia kaumu yake:  “Enyi kaumu yangu!  Kumbukeni neema ya Allaah juu yenu Alipojaalia miongoni mwenu Nabiy, na Akakufanyeni wenye kumiliki (mambo yenu mkawa huru) na Akakupeni yale Asiyowahi kumpa yeyote miongoni mwa walimwengu.” 



يَا قَوْمِ ادْخُلُوا الْأَرْضَ الْمُقَدَّسَةَ الَّتِي كَتَبَ اللَّـهُ لَكُمْ وَلَا تَرْتَدُّوا عَلَىٰ أَدْبَارِكُمْ فَتَنقَلِبُوا خَاسِرِينَ﴿٢١﴾
21. “Enyi kaumu yangu! Ingieni ardhi iliyotakaswa ambayo Amekuandikieni Allaah kwenu, na wala msirudi nyuma kugeuka (kukimbia kupigana katika njia ya Allaah, hivyo) mtageuka kuwa wenye kukhasirika.”

قَالُوا يَا مُوسَىٰ إِنَّ فِيهَا قَوْمًا جَبَّارِينَ وَإِنَّا لَن نَّدْخُلَهَا حَتَّىٰ يَخْرُجُوا مِنْهَا فَإِن يَخْرُجُوا مِنْهَا فَإِنَّا دَاخِلُونَ﴿٢٢﴾
22. Wakasema: “Ee Muwsaa! Hakika humo kuna watu majabari; nasi hatutaingia humo mpaka (majabari) watoke humo; watakapotoka humo; hapo (ndio) sisi tutaingia.”

قَالَ رَجُلَانِ مِنَ الَّذِينَ يَخَافُونَ أَنْعَمَ اللَّـهُ عَلَيْهِمَا ادْخُلُوا عَلَيْهِمُ الْبَابَ فَإِذَا دَخَلْتُمُوهُ فَإِنَّكُمْ غَالِبُونَ ۚ وَعَلَى اللَّـهِ فَتَوَكَّلُوا إِن كُنتُم مُّؤْمِنِينَ﴿٢٣﴾
23. Wakasema watu wawili miongoni mwa wale waliokhofu (kuasi, ambao) Allaah Aliowaneemesha (walisema): “Waingilieni katika mlango;    mkiwaingilia, basi hakika nyinyi mtashinda. Na kwa Allaah Pekee tawakalini ikiwa nyinyi ni Waumini”.

قَالُوا يَا مُوسَىٰ إِنَّا لَن نَّدْخُلَهَا أَبَدًا مَّا دَامُوا فِيهَا ۖ فَاذْهَبْ أَنتَ وَرَبُّكَ فَقَاتِلَا إِنَّا هَاهُنَا قَاعِدُونَ﴿٢٤﴾
24. Wakasema: “Ee Muwsaa!  Hakika sisi hatutoingia humo abadani madamu wamo (hao majabari); basi nenda wewe na Rabb (Mola) wako mkapigane, hakika sisi tutabakia hapa hapa.”

قَالَ رَبِّ إِنِّي لَا أَمْلِكُ إِلَّا نَفْسِي وَأَخِي ۖ فَافْرُقْ بَيْنَنَا وَبَيْنَ الْقَوْمِ الْفَاسِقِينَ﴿٢٥﴾
25. (Muwsaa) Akasema:  “Rabb (Mola) wangu! Hakika mimi similiki ila nafsi yangu na ndugu yangu; basi Tutenganishe baina yetu na watu mafasiki.”

قَالَ فَإِنَّهَا مُحَرَّمَةٌ عَلَيْهِمْ ۛ أَرْبَعِينَ سَنَةً ۛ يَتِيهُونَ فِي الْأَرْضِ ۚ فَلَا تَأْسَ عَلَى الْقَوْمِ الْفَاسِقِينَ﴿٢٦﴾
26. (Allaah) Akasema: “Basi hakika ardhi hiyo imeharamishwa kwao miaka arubaini; watatangatanga ardhini. Basi usisikitike juu ya watu mafasiki.”

وَاتْلُ عَلَيْهِمْ نَبَأَ ابْنَيْ آدَمَ بِالْحَقِّ إِذْ قَرَّبَا قُرْبَانًا فَتُقُبِّلَ مِنْ أَحَدِهِمَا وَلَمْ يُتَقَبَّلْ مِنَ الْآخَرِ قَالَ لَأَقْتُلَنَّكَ ۖ قَالَ إِنَّمَا يَتَقَبَّلُ اللَّـهُ مِنَ الْمُتَّقِينَ﴿٢٧﴾
27. Na wasomee (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) habari za wana wawili wa Aadam; kwa haki walipotoa qurbaan (swadaqah) ikakubaliwa ya mmoja wao, na haikukubaliwa ya mwengine; (asiyekubaliwa) akasema: “Nitakuua.” (Aliyekubaliwa) Akasema: “Hakika Allaah Anatakabalia wenye taqwa”.

لَئِن بَسَطتَ إِلَيَّ يَدَكَ لِتَقْتُلَنِي مَا أَنَا بِبَاسِطٍ يَدِيَ إِلَيْكَ لِأَقْتُلَكَ ۖ إِنِّي أَخَافُ اللَّـهَ رَبَّ الْعَالَمِينَ﴿٢٨﴾
28. “Ukininyoshea mkono wako ili uniue, mimi sitokunyoshea mkono wangu kukuua; hakika mimi namkhofu Allaah Rabb (Mola) wa walimwengu.”

إِنِّي أُرِيدُ أَن تَبُوءَ بِإِثْمِي وَإِثْمِكَ فَتَكُونَ مِنْ أَصْحَابِ النَّارِ ۚ وَذَٰلِكَ جَزَاءُ الظَّالِمِينَ﴿٢٩﴾
29. Hakika mimi nataka ubebe dhambi zangu na dhambi zako hapo utakuwa miongoni mwa watu wa Motoni; na hiyo ndiyo jazaa ya madhalimu.

فَطَوَّعَتْ لَهُ نَفْسُهُ قَتْلَ أَخِيهِ فَقَتَلَهُ فَأَصْبَحَ مِنَ الْخَاسِرِينَ﴿٣٠﴾
 30. Basi (aliyekataliwa swadaqah,) nafsi yake ikamwezesha kwa wepesi kumuua ndugu yake; akamuua na akawa miongoni mwa waliokhasirika.

فَبَعَثَ اللَّـهُ غُرَابًا يَبْحَثُ فِي الْأَرْضِ لِيُرِيَهُ كَيْفَ يُوَارِي سَوْءَةَ أَخِيهِ ۚ قَالَ يَا وَيْلَتَىٰ أَعَجَزْتُ أَنْ أَكُونَ مِثْلَ هَـٰذَا الْغُرَابِ فَأُوَارِيَ سَوْءَةَ أَخِي ۖ فَأَصْبَحَ مِنَ النَّادِمِينَ﴿٣١﴾
31. Kisha Allaah Akamleta kunguru akifukua katika ardhi ili amwonyeshe vipi asitiri maiti ya ndugu yake. (Muuaji) Akasema: “Ole wangu! Hivi nimeshindwa kuwa kama huyu kunguru nikamsitiri ndugu yangu?” Akawa miongoni mwa wajutao.


مِنْ أَجْلِ ذَٰلِكَ كَتَبْنَا عَلَىٰ بَنِي إِسْرَائِيلَ أَنَّهُ مَن قَتَلَ نَفْسًا بِغَيْرِ نَفْسٍ أَوْ فَسَادٍ فِي الْأَرْضِ فَكَأَنَّمَا قَتَلَ النَّاسَ جَمِيعًا وَمَنْ أَحْيَاهَا فَكَأَنَّمَا أَحْيَا النَّاسَ جَمِيعًا ۚ وَلَقَدْ جَاءَتْهُمْ رُسُلُنَا بِالْبَيِّنَاتِ ثُمَّ إِنَّ كَثِيرًا مِّنْهُم بَعْدَ ذَٰلِكَ فِي الْأَرْضِ لَمُسْرِفُونَ﴿٣٢﴾
32. Kwa ajili ya hivyo, Tukawaandikia (shariy’ah) wana wa Israaiyl kwamba; atakayeiua nafsi bila ya nafsi (kuua), au (bila ya) kufanya ufisadi katika ardhi; basi ni kama ameua watu wote. Na atakayeiokoa (kumsaidia kuishi) basi ni kama amewaokoa watu wote. Na bila shaka walifikiwa na Rasuli Wetu kwa hoja bayana; kisha wengi miongoni mwao baada ya hayo wamekuwa wapindukao mipaka ya kuasi.

إِنَّمَا جَزَاءُ الَّذِينَ يُحَارِبُونَ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ وَيَسْعَوْنَ فِي الْأَرْضِ فَسَادًا أَن يُقَتَّلُوا أَوْ يُصَلَّبُوا أَوْ تُقَطَّعَ أَيْدِيهِمْ وَأَرْجُلُهُم مِّنْ خِلَافٍ أَوْ يُنفَوْا مِنَ الْأَرْضِ ۚ ذَٰلِكَ لَهُمْ خِزْيٌ فِي الدُّنْيَا ۖ وَلَهُمْ فِي الْآخِرَةِ عَذَابٌ عَظِيمٌ﴿٣٣﴾
33. Hakika jazaa ya wale wanaompiga vita Allaah na Rasuli Wake na wanafanya bidii kufanya ufisadi katika ardhi; ni kwamba wauawe au wasulubiwe au wakatwe mikono yao na miguu yao kwa mabadilisho (mkono wa kulia kwa mguu wa kushoto, na mkono wa kushoto kwa mguu wa kulia) au kuhamishwa katika nchi. Hiyo ndiyo hizaya yao duniani. Na Aakhirah watapata adhabu kuu.

إِلَّا الَّذِينَ تَابُوا مِن قَبْلِ أَن تَقْدِرُوا عَلَيْهِمْ ۖ فَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ﴿٣٤﴾
34. Isipokuwa wale waliotubia kabla ya kuwashinda nguvu basi jueni kwamba hakika Allaah ni Ghafuwrur-Rahiym (Mwingi wa kughufuria - Mwenye kurehemu).

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّـهَ وَابْتَغُوا إِلَيْهِ الْوَسِيلَةَ وَجَاهِدُوا فِي سَبِيلِهِ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ﴿٣٥﴾
35. Enyi mlioamini! Mcheni Allaah na tafuteni Kwake al-wasiylah (njia za 'ibaadah kumkurubia); na fanyeni jihaad katika njia Yake mpate kufaulu.

إِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا لَوْ أَنَّ لَهُم مَّا فِي الْأَرْضِ جَمِيعًا وَمِثْلَهُ مَعَهُ لِيَفْتَدُوا بِهِ مِنْ عَذَابِ يَوْمِ الْقِيَامَةِ مَا تُقُبِّلَ مِنْهُمْ ۖ وَلَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ﴿٣٦﴾
36. Hakika wale waliokufuru, kama watakuwa na yale yote yaliyomo ardhini na mfano wake pamoja nayo, ili watoe fidia kwayo kuepukana na adhabu ya Siku ya Qiyaamah, hayatokubaliwa kutoka kwao, na watapata adhabu iumizayo.

يُرِيدُونَ أَن يَخْرُجُوا مِنَ النَّارِ وَمَا هُم بِخَارِجِينَ مِنْهَا ۖ وَلَهُمْ عَذَابٌ مُّقِيمٌ﴿٣٧﴾
37. Watataka kutoka katika Moto (kwa kila njia); lakini wao si wenye kutoka kamwe humo, na watapata adhabu ya kudumu.

وَالسَّارِقُ وَالسَّارِقَةُ فَاقْطَعُوا أَيْدِيَهُمَا جَزَاءً بِمَا كَسَبَا نَكَالًا مِّنَ اللَّـهِ ۗ وَاللَّـهُ عَزِيزٌ حَكِيمٌ﴿٣٨﴾
38. Mwizi mwanamume na mwizi mwanamke wakateni mikono yao (kitanga cha mkono wa kulia); ni malipo kwa yale waliyoyachuma, ndio adhabu ya mfano kutoka kwa Allaah. Na Allaah ni ‘Aziyzun-Hakiym (Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika - Mwenye hikmah wa yote).

فَمَن تَابَ مِن بَعْدِ ظُلْمِهِ وَأَصْلَحَ فَإِنَّ اللَّـهَ يَتُوبُ عَلَيْهِ ۗ إِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ﴿٣٩﴾
 39. Basi atakayetubia baada ya dhulma yake na akatengenea (kwa kutenda vitendo vizuri); basi Allaah Atapokea tawbah yake. Hakika Allaah ni Ghafuwrur-Rahiym (Mwingi wa kughufuria - Mwenye kurehemu).

أَلَمْ تَعْلَمْ أَنَّ اللَّـهَ لَهُ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ يُعَذِّبُ مَن يَشَاءُ وَيَغْفِرُ لِمَن يَشَاءُ ۗ وَاللَّـهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ﴿٤٠﴾
40. Je hujui ya kwamba ni Allaah Pekee Anao ufalme wa mbingu na ardhi? Humwadhibu Amtakae na Humghufiria Amtakae. Na Allaah juu ya kila kitu ni Qadiyr (Muweza).

يَا أَيُّهَا الرَّسُولُ لَا يَحْزُنكَ الَّذِينَ يُسَارِعُونَ فِي الْكُفْرِ مِنَ الَّذِينَ قَالُوا آمَنَّا بِأَفْوَاهِهِمْ وَلَمْ تُؤْمِن قُلُوبُهُمْ ۛ وَمِنَ الَّذِينَ هَادُوا ۛ سَمَّاعُونَ لِلْكَذِبِ سَمَّاعُونَ لِقَوْمٍ آخَرِينَ لَمْ يَأْتُوكَ ۖ يُحَرِّفُونَ الْكَلِمَ مِن بَعْدِ مَوَاضِعِهِ ۖ يَقُولُونَ إِنْ أُوتِيتُمْ هَـٰذَا فَخُذُوهُ وَإِن لَّمْ تُؤْتَوْهُ فَاحْذَرُوا ۚ وَمَن يُرِدِ اللَّـهُ فِتْنَتَهُ فَلَن تَمْلِكَ لَهُ مِنَ اللَّـهِ شَيْئًا ۚ أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ لَمْ يُرِدِ اللَّـهُ أَن يُطَهِّرَ قُلُوبَهُمْ ۚ لَهُمْ فِي الدُّنْيَا خِزْيٌ ۖ وَلَهُمْ فِي الْآخِرَةِ عَذَابٌ عَظِيمٌ﴿٤١﴾
41. Ee Rasuli! Wasikuhuzunishe wale wanaokimbilia kukufuru miongoni mwa wasemao kwa midomo yao: “Tumeamini” na hali nyoyo zao hazikuamini. Na miongoni mwa Mayahudi wanaosikiliza kwa makini kwa ajili ya uongo, wanaosikiliza kwa makini kwa ajili ya watu wengine (wakubwazao) wasiokufikia. Wanageuza maneno kutoka mahali pake; wanasema (kuwaambia wafuasi wao): “Mkipewa haya (tunayokuambieni kutoka kwa Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) basi yachukueni, na msipopewa hayo basi jihadharini!”. Na yule ambaye Allaah Anataka kumtia mtihanini, hutamiliki juu yake (uwezo wa kumsaidia) chochote mbele ya Allaah. Hao ndio ambao Allaah Hakutaka kuzitakasa nyoyo zao. Watapata hizaya duniani na Aakhirah watapata adhabu kuu.


سَمَّاعُونَ لِلْكَذِبِ أَكَّالُونَ لِلسُّحْتِ ۚ فَإِن جَاءُوكَ فَاحْكُم بَيْنَهُمْ أَوْ أَعْرِضْ عَنْهُمْ ۖ وَإِن تُعْرِضْ عَنْهُمْ فَلَن يَضُرُّوكَ شَيْئًا ۖ وَإِنْ حَكَمْتَ فَاحْكُم بَيْنَهُم بِالْقِسْطِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ الْمُقْسِطِينَ﴿٤٢﴾
42. (Hao) Wenye kusikiliza kwa makini uongo, walaji mno wa haraam. Basi wakikujia (ee Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم wahukumu baina yao au wapuuze. Na ukiwapuuza, hawatoweza kukudhuru chochote. Na kama ukihukumu, basi hukumu baina yao kwa uadilifu. Hakika Allaah Anapenda wafanyao uadilifu.


وَكَيْفَ يُحَكِّمُونَكَ وَعِندَهُمُ التَّوْرَاةُ فِيهَا حُكْمُ اللَّـهِ ثُمَّ يَتَوَلَّوْنَ مِن بَعْدِ ذَٰلِكَ ۚ وَمَا أُولَـٰئِكَ بِالْمُؤْمِنِينَ﴿٤٣﴾
43. Na vipi watakufanya wewe kuwa hakimu (wao) na hali wana Tawraat iliyomo ndani yake hukumu ya Allaah; kisha baada ya hayo wanakengeuka. Na hao si wenye kuamini.

إِنَّا أَنزَلْنَا التَّوْرَاةَ فِيهَا هُدًى وَنُورٌ ۚ يَحْكُمُ بِهَا النَّبِيُّونَ الَّذِينَ أَسْلَمُوا لِلَّذِينَ هَادُوا وَالرَّبَّانِيُّونَ وَالْأَحْبَارُ بِمَا اسْتُحْفِظُوا مِن كِتَابِ اللَّـهِ وَكَانُوا عَلَيْهِ شُهَدَاءَ ۚ فَلَا تَخْشَوُا النَّاسَ وَاخْشَوْنِ وَلَا تَشْتَرُوا بِآيَاتِي ثَمَنًا قَلِيلًا ۚ وَمَن لَّمْ يَحْكُم بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْكَافِرُونَ﴿٤٤﴾
44. Hakika Tumeteremsha Tawraat humo mna mwongozo na nuru; ambayo kwayo, Nabiy waliojisalimisha (kwa Allaah) waliwahukumu Mayahudi na Ar-Rabbaniyyuwna (Wanavyuoni wafanyao mno ‘ibaadah na kufanyia kazi elimu zao)  na Al-Ahbaar (Wanavyuoni mafuqahaa wa dini) pia (walihukumu kwa hiyo Tawraat) kwa sababu waliyokabidhiwa kuhifadhi Kitabu cha Allaah; na wakawa mashahidi juu yake. Basi msiwaogope watu, bali Niogopeni (Mimi), na wala msibadili Aayaat Zangu kwa thamani ndogo. Na yeyote asiyehukumu kwa yale Aliyoyateremsha Allaah, basi hao ndio makafiri.

وَكَتَبْنَا عَلَيْهِمْ فِيهَا أَنَّ النَّفْسَ بِالنَّفْسِ وَالْعَيْنَ بِالْعَيْنِ وَالْأَنفَ بِالْأَنفِ وَالْأُذُنَ بِالْأُذُنِ وَالسِّنَّ بِالسِّنِّ وَالْجُرُوحَ قِصَاصٌ ۚ فَمَن تَصَدَّقَ بِهِ فَهُوَ كَفَّارَةٌ لَّهُ ۚ وَمَن لَّمْ يَحْكُم بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ﴿٤٥﴾
45. Na Tumewaandikia (shariy’ah) humo kwamba uhai kwa uhai, na jichokwa jicho, na pua kwa pua, na sikio kwa sikio, jino kwa jino; na majaraha (kulipizana) kisasi. Lakini atakayetolea swadaqah (haki yake akasemehe) kwayo, basi itakuwa ni kafara kwake. Na yeyote asiyehukumu kwa yale Aliyoyateremsha Allaah, basi hao ndio madhalimu.


وَقَفَّيْنَا عَلَىٰ آثَارِهِم بِعِيسَى ابْنِ مَرْيَمَ مُصَدِّقًا لِّمَا بَيْنَ يَدَيْهِ مِنَ التَّوْرَاةِ ۖ وَآتَيْنَاهُ الْإِنجِيلَ فِيهِ هُدًى وَنُورٌ وَمُصَدِّقًا لِّمَا بَيْنَ يَدَيْهِ مِنَ التَّوْرَاةِ وَهُدًى وَمَوْعِظَةً لِّلْمُتَّقِينَ﴿٤٦﴾
46. Na Tukatuma, kufuatisha nyao zao (Mitume hao), ‘Iysaa mwana wa Maryam akisadikisha yale yaliyoko kabla yake katika Tawraat. Na Tukampa Injiyl iliyomo ndani yake mwongozo na nuru; na isadikishayo yale yaliyokuwa kabla yake katika Tawraat, na mwongozo na mawaidha kwa wenye taqwa.

وَلْيَحْكُمْ أَهْلُ الْإِنجِيلِ بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ فِيهِ ۚ وَمَن لَّمْ يَحْكُم بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْفَاسِقُونَ﴿٤٧﴾
47. Na watu (waliopewa) Injiyl wahukumu kwa yale Aliyoyateremsha Allaah ndani yake. Na yeyote asiyehukumu kwa yale Aliyoyateremsha Allaah, basi hao ndio mafasiki.

وَأَنزَلْنَا إِلَيْكَ الْكِتَابَ بِالْحَقِّ مُصَدِّقًا لِّمَا بَيْنَ يَدَيْهِ مِنَ الْكِتَابِ وَمُهَيْمِنًا عَلَيْهِ ۖ فَاحْكُم بَيْنَهُم بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ ۖ وَلَا تَتَّبِعْ أَهْوَاءَهُمْ عَمَّا جَاءَكَ مِنَ الْحَقِّ ۚ لِكُلٍّ جَعَلْنَا مِنكُمْ شِرْعَةً وَمِنْهَاجًا ۚ وَلَوْ شَاءَ اللَّـهُ لَجَعَلَكُمْ أُمَّةً وَاحِدَةً وَلَـٰكِن لِّيَبْلُوَكُمْ فِي مَا آتَاكُمْ ۖ فَاسْتَبِقُوا الْخَيْرَاتِ ۚ إِلَى اللَّـهِ مَرْجِعُكُمْ جَمِيعًا فَيُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمْ فِيهِ تَخْتَلِفُونَ﴿٤٨﴾
48. Na Tumekuteremshia (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) Kitabu kwa haki kinachosadikisha yale (yaliyokuja katika) Vitabu vilivyokuwa kabla yake na muhayminan (chenye kudhibiti, kushuhudia nakuhukumu) juu yake (hivo Vitabu). Basi hukumu baina yao kwa yale Aliyoyateremsha Allaah; na wala usifuate hawaa zao kwa kuacha haki iliyokujia. Kwa kila (ummah) katika nyinyi Tumeujaalia shariy’ah namanhaj. Nakama Angetaka Allaah Angelikufanyeni ummah mmoja; lakini (Allaah Amekufanyeni hivyo) ili Akujaribuni katika yale Aliyokupeni. Basi shindaneni katika mambo ya kheri. Kwa Allaah Pekee ndio marejeo yenu nyote; kisha Atakujulisheni yale mliyokuwa mkikhitilafiana.


وَأَنِ احْكُم بَيْنَهُم بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ وَلَا تَتَّبِعْ أَهْوَاءَهُمْ وَاحْذَرْهُمْ أَن يَفْتِنُوكَ عَن بَعْضِ مَا أَنزَلَ اللَّـهُ إِلَيْكَ ۖ فَإِن تَوَلَّوْا فَاعْلَمْ أَنَّمَا يُرِيدُ اللَّـهُ أَن يُصِيبَهُم بِبَعْضِ ذُنُوبِهِمْ ۗ وَإِنَّ كَثِيرًا مِّنَ النَّاسِ لَفَاسِقُونَ﴿٤٩﴾
49. Na wahukumu baina yao kwa yale Aliyoyateremsha Allaah, na wala usifuate hawaa zao, na jihadhari nao wasije kukufitini ukaacha baadhi ya yale Aliyokuteremshia Allaah. Na wakikengeuka, basi jua kuwa hakika Allaah Anataka kuwasibu (adhabu) kwa baadhi ya madhambi yao. Na hakikawengi katika watu ni mafasiki.

أَفَحُكْمَ الْجَاهِلِيَّةِ يَبْغُونَ ۚ وَمَنْ أَحْسَنُ مِنَ اللَّـهِ حُكْمًا لِّقَوْمٍ يُوقِنُونَ﴿٥٠﴾
50. Je, wanataka (uwahukumu kwa) hukumu ya kijaahiliyyah? (ujinga kabla ya Uislamu). Na nani mbora zaidi kuliko Allaah katika kuhukumu? (Yanafahamika haya) kwa watu wenye yakini.

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَتَّخِذُوا الْيَهُودَ وَالنَّصَارَىٰ أَوْلِيَاءَ ۘ بَعْضُهُمْ أَوْلِيَاءُ بَعْضٍ ۚ وَمَن يَتَوَلَّهُم مِّنكُمْ فَإِنَّهُ مِنْهُمْ ۗ إِنَّ اللَّـهَ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الظَّالِمِينَ﴿٥١﴾
51. Enyi mlioamini! Msifanye Mayahudi na Manaswara marafiki wandani na ushirikiano. Wao kwa wao ni marafiki wandani. Na yeyote atakayewafanya marafiki wao wandani; basi hakika yeye ni miongoni mwao. Hakika Allaah Haongoi watu madhalimu.

فَتَرَى الَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٌ يُسَارِعُونَ فِيهِمْ يَقُولُونَ نَخْشَىٰ أَن تُصِيبَنَا دَائِرَةٌ ۚ فَعَسَى اللَّـهُ أَن يَأْتِيَ بِالْفَتْحِ أَوْ أَمْرٍ مِّنْ عِندِهِ فَيُصْبِحُوا عَلَىٰ مَا أَسَرُّوا فِي أَنفُسِهِمْ نَادِمِينَ﴿٥٢﴾
52. Basi utawaona wale ambao katika nyoyo zao mna maradhi (ya shaka naunafiki) wanakimbilia kwao wakisema: “Tunakhofu isitusibu mgeuko. Basi Huenda Allaah Akaleta ushindi au jambo (lolote jengine) litokalo Kwake; wakawa wenye kujuta kwa waliyoyaficha katika nafsi zao.

وَيَقُولُ الَّذِينَ آمَنُوا أَهَـٰؤُلَاءِ الَّذِينَ أَقْسَمُوا بِاللَّـهِ جَهْدَ أَيْمَانِهِمْ ۙ إِنَّهُمْ لَمَعَكُمْ ۚ حَبِطَتْ أَعْمَالُهُمْ فَأَصْبَحُوا خَاسِرِينَ﴿٥٣﴾
 53. Na wale walioamini wanasema: “Je, hawa ndio wale ambao waliapa kwa (jina la) Allaah kwa viapo vyao vya nguvu, kwamba hakika wao wapopamoja nanyi?” Zimebatilika ‘amali zao, na wamekuwa wenye kukhasirika.

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا مَن يَرْتَدَّ مِنكُمْ عَن دِينِهِ فَسَوْفَ يَأْتِي اللَّـهُ بِقَوْمٍ يُحِبُّهُمْ وَيُحِبُّونَهُ أَذِلَّةٍ عَلَى الْمُؤْمِنِينَ أَعِزَّةٍ عَلَى الْكَافِرِينَ يُجَاهِدُونَ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ وَلَا يَخَافُونَ لَوْمَةَ لَائِمٍ ۚ ذَٰلِكَ فَضْلُ اللَّـهِ يُؤْتِيهِ مَن يَشَاءُ ۚ وَاللَّـهُ وَاسِعٌ عَلِيمٌ﴿٥٤﴾
54. Enyi mlioamini! Yeyote atakayeritadi miongoni mwenu kutoka Dini yake, basi Allaah Ataleta watu (badala yao) Atakaowapenda nao watampenda; wanyenyekevu kwa Waumini, wenye nguvu juu ya makafiri; wanafanya jihaad katika njia ya Allaah na wala hawakhofu lawama ya (yeyote) anayelaumu. Hiyo ni fadhila ya Allaah Humpa Amtakaye. Na Allaah niWaasi’un-‘Aliym (Mwenye wasaa - Mjuzi wa yote).

إِنَّمَا وَلِيُّكُمُ اللَّـهُ وَرَسُولُهُ وَالَّذِينَ آمَنُوا الَّذِينَ يُقِيمُونَ الصَّلَاةَ وَيُؤْتُونَ الزَّكَاةَ وَهُمْ رَاكِعُونَ﴿٥٥﴾
55. Hakika Waliyy (Mlinzi, Msimamizi) wenu ni Allaah na Rasuli Wake nawale walioamini, ambao wanasimamisha Swalaah na wanatoa Zakaah nahali ya kuwa wananyenyekea.

وَمَن يَتَوَلَّ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ وَالَّذِينَ آمَنُوا فَإِنَّ حِزْبَ اللَّـهِ هُمُ الْغَالِبُونَ﴿٥٦﴾
56. Na atakayemfanya Allaah kuwa ni Waliyy (Mlinzi, Msimamizi) na Rasuli Wake na wale walioamini (atafuzu); kwani hakika kundi la Allaah ndio washindi.

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَتَّخِذُوا الَّذِينَ اتَّخَذُوا دِينَكُمْ هُزُوًا وَلَعِبًا مِّنَ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ مِن قَبْلِكُمْ وَالْكُفَّارَ أَوْلِيَاءَ ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ إِن كُنتُم مُّؤْمِنِينَ﴿٥٧﴾
57. Enyi mlioamini! Msiwafanye wale walioifanya Dini yenu mzaha na mchezo - miongoni mwa wale waliopewa Kitabu kabla yenu, (pamoja na) makafiri (kuwa ndio) marafiki wandani na ushirikiano. Na mcheni Allaah, kamanyinyi ni Waumini (kweli).

وَإِذَا نَادَيْتُمْ إِلَى الصَّلَاةِ اتَّخَذُوهَا هُزُوًا وَلَعِبًا ۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمْ قَوْمٌ لَّا يَعْقِلُونَ﴿٥٨﴾
58. Na mnapoita (kuadhini) katika Swalaah; huifanyia mzaha na mchezo. Hivyo ni kwa kuwa wao ni watu wasiotia akilini.

قُلْ يَا أَهْلَ الْكِتَابِ هَلْ تَنقِمُونَ مِنَّا إِلَّا أَنْ آمَنَّا بِاللَّـهِ وَمَا أُنزِلَ إِلَيْنَا وَمَا أُنزِلَ مِن قَبْلُ وَأَنَّ أَكْثَرَكُمْ فَاسِقُونَ﴿٥٩﴾
59. Sema: “Enyi Ahlal-Kitaab Je, mnatuchukia tu kwa vile tumemwamini Allaah na (tunaamini) yale yaliyoteremshwa kwetu na (pia tunaamini) yale yaliyoteremshwa kabla; na kwamba wengi wenu ni mafasiki?”

قُلْ هَلْ أُنَبِّئُكُم بِشَرٍّ مِّن ذَٰلِكَ مَثُوبَةً عِندَ اللَّـهِ ۚ مَن لَّعَنَهُ اللَّـهُ وَغَضِبَ عَلَيْهِ وَجَعَلَ مِنْهُمُ الْقِرَدَةَ وَالْخَنَازِيرَ وَعَبَدَ الطَّاغُوتَ ۚ أُولَـٰئِكَ شَرٌّ مَّكَانًا وَأَضَلُّ عَن سَوَاءِ السَّبِيلِ﴿٦٠﴾
60. Sema: “Je, nikujulisheni yaliyo maovu zaidi kuliko hayo kwa malipo (mabaya) mbele ya Allaah?” Yule ambaye Allaah Amemlaani na Akamghadhibikia na Akawafanya miongoni mwao manyani na nguruwe na wakaabudu twaaghuwt, hao wana mahali pabaya mno (Aakhirah) na wapotofu zaidi na njia iliyo sawa (duniani)

وَإِذَا جَاءُوكُمْ قَالُوا آمَنَّا وَقَد دَّخَلُوا بِالْكُفْرِ وَهُمْ قَدْ خَرَجُوا بِهِ ۚ وَاللَّـهُ أَعْلَمُ بِمَا كَانُوا يَكْتُمُونَ﴿٦١﴾
61. Na wanapokujieni husema: “Tumeamini.” Na hali wameingia na ukafiri na wakatoka nao. Na Allaah Anajua zaidi yale waliyokuwa wakiyaficha.

وَتَرَىٰ كَثِيرًا مِّنْهُمْ يُسَارِعُونَ فِي الْإِثْمِ وَالْعُدْوَانِ وَأَكْلِهِمُ السُّحْتَ ۚ لَبِئْسَ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ﴿٦٢﴾
62. Na utawaona wengi miongoni mwao wanakimbilia katika dhambi na uadui na kula kwao haraam. Ubaya ulioje yale waliyokuwa wakiyatenda.

لَوْلَا يَنْهَاهُمُ الرَّبَّانِيُّونَ وَالْأَحْبَارُ عَن قَوْلِهِمُ الْإِثْمَ وَأَكْلِهِمُ السُّحْتَ ۚ لَبِئْسَ مَا كَانُوا يَصْنَعُونَ﴿٦٣﴾
63. Mbona hawawakatazi Ar-Rabbaniyyuwna (Wanavyuoni wafanyao mno ‘ibaadah na kufanyia kazi elimu zao) na Al-Ahbaar (Wanavyuoni mafuqahaa wa dini) kuhusu kauli zao za dhambi na ulaji wao wa haraam. Bila shaka ubaya ulioje yale waliyokuwa wakitenda.

وَقَالَتِ الْيَهُودُ يَدُ اللَّـهِ مَغْلُولَةٌ ۚ غُلَّتْ أَيْدِيهِمْ وَلُعِنُوا بِمَا قَالُوا ۘ بَلْ يَدَاهُ مَبْسُوطَتَانِ يُنفِقُ كَيْفَ يَشَاءُ ۚ وَلَيَزِيدَنَّ كَثِيرًا مِّنْهُم مَّا أُنزِلَ إِلَيْكَ مِن رَّبِّكَ طُغْيَانًا وَكُفْرًا ۚ وَأَلْقَيْنَا بَيْنَهُمُ الْعَدَاوَةَ وَالْبَغْضَاءَ إِلَىٰ يَوْمِ الْقِيَامَةِ ۚ كُلَّمَا أَوْقَدُوا نَارًا لِّلْحَرْبِ أَطْفَأَهَا اللَّـهُ ۚ وَيَسْعَوْنَ فِي الْأَرْضِ فَسَادًا ۚ وَاللَّـهُ لَا يُحِبُّ الْمُفْسِدِينَ﴿٦٤﴾
64. Na Mayahudi wakasema: “Mkono wa Allaah umefumbwa.” (Siyo, bali) mikono yao ndio iliyofumbwa; na wamelaaniwa kwa yale waliyoyasema. Bali Mikono Yake (Allaah) imefumbuliwa Hutoa Atakavyo. Kwa yakini yaliyoteremshwa kwako kutoka kwa Rabb (Mola) wako, yatawazidisha wengi miongoni mwao (hao Mayahudi) upindukaji mipaka ya kuasi na kufuru. Na Tumewatilia baina yao uadui na bughudha mpaka Siku ya Qiyaamah. Kila wanapouwasha moto wa vita (dhidi yako), Allaah Huuzima. Na wanafanya bidii kufanya ufisadi katika ardhi. Na Allaah Hapendi mafisadi.

وَلَوْ أَنَّ أَهْلَ الْكِتَابِ آمَنُوا وَاتَّقَوْا لَكَفَّرْنَا عَنْهُمْ سَيِّئَاتِهِمْ وَلَأَدْخَلْنَاهُمْ جَنَّاتِ النَّعِيمِ﴿٦٥﴾
65. Na lau kama Ahlal-Kitaab wangeamini na wakawa na taqwa, bila shaka Tungeliwafutia maovu yao, na bila shaka Tungeliwaingiza katika Jannaat za neema (za kila aina).

وَلَوْ أَنَّهُمْ أَقَامُوا التَّوْرَاةَ وَالْإِنجِيلَ وَمَا أُنزِلَ إِلَيْهِم مِّن رَّبِّهِمْ لَأَكَلُوا مِن فَوْقِهِمْ وَمِن تَحْتِ أَرْجُلِهِم ۚ مِّنْهُمْ أُمَّةٌ مُّقْتَصِدَةٌ ۖ وَكَثِيرٌ مِّنْهُمْ سَاءَ مَا يَعْمَلُونَ﴿٦٦﴾
66. Na lau kama wangeliisimamisha Tawraat na Injiyl na yale yaliyoteremshwa kwao kutoka kwa Rabb (Mola) wao; bila shaka wangelikula (rizki) kutoka juu yao na chini ya miguu yao. Miongoni mwao ni wastani (wanaofuata Tawraat na Injiyl kwa kiasi), na wengi wao wanayoyafanya ni mabaya mno

يَا أَيُّهَا الرَّسُولُ بَلِّغْ مَا أُنزِلَ إِلَيْكَ مِن رَّبِّكَ ۖ وَإِن لَّمْ تَفْعَلْ فَمَا بَلَّغْتَ رِسَالَتَهُ ۚ وَاللَّـهُ يَعْصِمُكَ مِنَ النَّاسِ ۗ إِنَّ اللَّـهَ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الْكَافِرِينَ﴿٦٧﴾
67. Ee Rasuli! Balighisha yale yaliyoteremshwa kwako kutoka kwa Rabb (Mola) wako. Na usipofanya, basi utakuwa hukubalighisha ujumbe Wake. Na Allaah Atakuhifadhi dhidi ya watu. Hakika Allaah Haongoi watu makafiri.

قُلْ يَا أَهْلَ الْكِتَابِ لَسْتُمْ عَلَىٰ شَيْءٍ حَتَّىٰ تُقِيمُوا التَّوْرَاةَ وَالْإِنجِيلَ وَمَا أُنزِلَ إِلَيْكُم مِّن رَّبِّكُمْ ۗ وَلَيَزِيدَنَّ كَثِيرًا مِّنْهُم مَّا أُنزِلَ إِلَيْكَ مِن رَّبِّكَ طُغْيَانًا وَكُفْرًا ۖ فَلَا تَأْسَ عَلَى الْقَوْمِ الْكَافِرِينَ﴿٦٨﴾
68. Sema: “Enyi Ahlal-Kitaab! Hamko juu ya chochote mpaka muisimamishe (shariy’ah ya) Tawraat na Injiyl na yale yaliyoteremshwa kwenu kutoka kwa Rabb (Mola) wenu. Kwa yakini yaliyoteremshwa kwako kutoka kwa Rabb wako, yatawazidisha wengi miongoni mwao upindukaji mipaka ya kuasi na kufuru. Basi usisikitike juu ya watu makafiri.

إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَالَّذِينَ هَادُوا وَالصَّابِئُونَ وَالنَّصَارَىٰ مَنْ آمَنَ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ وَعَمِلَ صَالِحًا فَلَا خَوْفٌ عَلَيْهِمْ وَلَا هُمْ يَحْزَنُونَ﴿٦٩﴾
69. Hakika wale walioamini (Allaah na Muhammad  صلى الله عليه وآله وسلم)  na wale (kabla ya Uislamu;) Mayahudi na Masabai (waabudu nyota) na Manaswara, atakayemwamini Allaah na Siku ya Mwisho na akatenda mema, basi awatokuwa na khofu na wala hawatohuzunika

لَقَدْ أَخَذْنَا مِيثَاقَ بَنِي إِسْرَائِيلَ وَأَرْسَلْنَا إِلَيْهِمْ رُسُلًا ۖ كُلَّمَا جَاءَهُمْ رَسُولٌ بِمَا لَا تَهْوَىٰ أَنفُسُهُمْ فَرِيقًا كَذَّبُوا وَفَرِيقًا يَقْتُلُونَ﴿٧٠﴾
70. Kwa yakini Tulichukua fungamano la wana wa Israaiyl na Tukawapelekea Rasuli. Basi kila alipowajia Rasuli kwa yale yasiyoyapenda nafsi zao; kundi waliwakadhibisha (Rasuli hao) na kundi wakawaua.

وَحَسِبُوا أَلَّا تَكُونَ فِتْنَةٌ فَعَمُوا وَصَمُّوا ثُمَّ تَابَ اللَّـهُ عَلَيْهِمْ ثُمَّ عَمُوا وَصَمُّوا كَثِيرٌ مِّنْهُمْ ۚ وَاللَّـهُ بَصِيرٌ بِمَا يَعْمَلُونَ﴿٧١﴾
71. Na walidhani kwamba haitokuwa fitnah (mitihani au adhabu), basi wakawa vipofu na wakawa viziwi; kisha Allaah Akapokea tawbah yao; kisha (tena) wengi wao wakawa vipofu na wakawa viziwi. Na Allaah ni Baswiyr (Mwenye kuona) kwa yale wayatendayo.

لَقَدْ كَفَرَ الَّذِينَ قَالُوا إِنَّ اللَّـهَ هُوَ الْمَسِيحُ ابْنُ مَرْيَمَ ۖ وَقَالَ الْمَسِيحُ يَا بَنِي إِسْرَائِيلَ اعْبُدُوا اللَّـهَ رَبِّي وَرَبَّكُمْ ۖ إِنَّهُ مَن يُشْرِكْ بِاللَّـهِ فَقَدْ حَرَّمَ اللَّـهُ عَلَيْهِ الْجَنَّةَ وَمَأْوَاهُ النَّارُ ۖ وَمَا لِلظَّالِمِينَ مِنْ أَنصَارٍ﴿٧٢﴾
72. Kwa yakini wamekufuru wale waliosema: “Hakika Allaah ni Al-Masiyh mwana wa Maryam.” Na Al-Masiyh alisema: “Enyi wana wa Israaiyl! Mwabuduni Allaah, Rabb (Mola) wangu na Rabb wenu. (Kwani) Hakika mwenye kumshirikisha Allaah bila shaka Allaah Atamharamishia Jannah, na makazi yake yatakuwa ni Motoni. Na madhalimu hawatopata mwenye kunusuru yeyote.”

لَّقَدْ كَفَرَ الَّذِينَ قَالُوا إِنَّ اللَّـهَ ثَالِثُ ثَلَاثَةٍ ۘ وَمَا مِنْ إِلَـٰهٍ إِلَّا إِلَـٰهٌ وَاحِدٌ ۚ وَإِن لَّمْ يَنتَهُوا عَمَّا يَقُولُونَ لَيَمَسَّنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ﴿٧٣﴾
73. Kwa yakini wamekufuru wale waliosema: “Hakika Allaah ni watatu wa utatu. ”Na hali hapana ilaah (muabudiwa wa haki) isipokuwa Ilaah Mmoja (Pekee). Na wasipoacha yale wanayoyasema, bila ya shaka itawagusa wale waliokufuru miongoni mwao adhabu iumizayo.

أَفَلَا يَتُوبُونَ إِلَى اللَّـهِ وَيَسْتَغْفِرُونَهُ ۚ وَاللَّـهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ﴿٧٤﴾
74. Je hawatubii kwa Allaah na wakamwomba maghfira? Na Allaah ni Ghafuwrur-Rahiym (Mwingi wa kughufuria - Mwenye kurehemu).

مَّا الْمَسِيحُ ابْنُ مَرْيَمَ إِلَّا رَسُولٌ قَدْ خَلَتْ مِن قَبْلِهِ الرُّسُلُ وَأُمُّهُ صِدِّيقَةٌ ۖ كَانَا يَأْكُلَانِ الطَّعَامَ ۗ انظُرْ كَيْفَ نُبَيِّنُ لَهُمُ الْآيَاتِ ثُمَّ انظُرْ أَنَّىٰ يُؤْفَكُونَ﴿٧٥﴾
75. Al-Masiyh mwana wa Maryam si chochote ila ni Rasuli (tu); bila shaka Wamekwishapita kabla yake Rasuli (wengine). Na mama yake ni swiddiyqah (mkweli). Wote wawili walikuwa wanakula chakula (na hali Allaah Hali). Tazama jinsi Tunavyowabainishia Aayaat (ishara, dalili n.k) kisha tazama vipi wanavyoghilibiwa (kuacha haki).

قُلْ أَتَعْبُدُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ مَا لَا يَمْلِكُ لَكُمْ ضَرًّا وَلَا نَفْعًا ۚ وَاللَّـهُ هُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ﴿٧٦﴾
76. Sema: “Vipi mnaabudu asiyekuwa Allaah asiyemiliki (uwezo wa) kukudhuruni wala kukunufaisheni! Na Allaah Ndiye As-Samiy’ul-‘Aliym” (Mwenye kusikia yote - Mjuzi wa yote).


قُلْ يَا أَهْلَ الْكِتَابِ لَا تَغْلُوا فِي دِينِكُمْ غَيْرَ الْحَقِّ وَلَا تَتَّبِعُوا أَهْوَاءَ قَوْمٍ قَدْ ضَلُّوا مِن قَبْلُ وَأَضَلُّوا كَثِيرًا وَضَلُّوا عَن سَوَاءِ السَّبِيلِ﴿٧٧﴾
77. Sema:  “Enyi Ahlal-Kitaab! Msipindukie mipaka katika dini yenu bila ya haki; na wala msifuate hawaa za watu waliokwishapotea kabla na wakapotosha wengi na wakapotea njia iliyo sawa.”

لُعِنَ الَّذِينَ كَفَرُوا مِن بَنِي إِسْرَائِيلَ عَلَىٰ لِسَانِ دَاوُودَ وَعِيسَى ابْنِ مَرْيَمَ ۚ ذَٰلِكَ بِمَا عَصَوا وَّكَانُوا يَعْتَدُونَ﴿٧٨﴾
78. Wamelaaniwa wale waliokufuru miongoni mwa wana wa Israaiyl kwa lisani ya Daawuwd na ‘Iysaa mwana wa Maryam. Hivyo ni kwa sababu ya (kuendelea) kuasi kwao na walikuwa wakitaadi.

كَانُوا لَا يَتَنَاهَوْنَ عَن مُّنكَرٍ فَعَلُوهُ ۚ لَبِئْسَ مَا كَانُوا يَفْعَلُونَ﴿٧٩﴾
79. Walikuwa hawakatazani munkari waliyofanya. Uovu ulioje waliyokuwa wakiyafanya.

تَرَىٰ كَثِيرًا مِّنْهُمْ يَتَوَلَّوْنَ الَّذِينَ كَفَرُوا ۚ لَبِئْسَ مَا قَدَّمَتْ لَهُمْ أَنفُسُهُمْ أَن سَخِطَ اللَّـهُ عَلَيْهِمْ وَفِي الْعَذَابِ هُمْ خَالِدُونَ﴿٨٠﴾
80. Utawaona wengi miongoni mwao (Mayahudi) wanawafanya marafiki (wa karibu, walinzi) wale waliokufuru. Ubaya ulioje yale yaliyowatangulizia nafsi zao, (nayo ni) kuwa Allaah Amewaghadhibikia, na katika adhabu wao ni wenye kudumu.

وَلَوْ كَانُوا يُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ وَالنَّبِيِّ وَمَا أُنزِلَ إِلَيْهِ مَا اتَّخَذُوهُمْ أَوْلِيَاءَ وَلَـٰكِنَّ كَثِيرًا مِّنْهُمْ فَاسِقُونَ﴿٨١﴾
81. Na lau wangelikuwa wanamwamini Allaah na (huyu) Nabiy (Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) na yale yaliyoteremshwa kwake, wasingeliwafanya hao marafiki wandani na ushirikiano, lakini wengi miongoni mwao ni mafasiki.


لَتَجِدَنَّ أَشَدَّ النَّاسِ عَدَاوَةً لِّلَّذِينَ آمَنُوا الْيَهُودَ وَالَّذِينَ أَشْرَكُوا ۖ وَلَتَجِدَنَّ أَقْرَبَهُم مَّوَدَّةً لِّلَّذِينَ آمَنُوا الَّذِينَ قَالُوا إِنَّا نَصَارَىٰ ۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّ مِنْهُمْ قِسِّيسِينَ وَرُهْبَانًا وَأَنَّهُمْ لَا يَسْتَكْبِرُونَ﴿٨٢﴾
82. Bila shaka utawakuta walio maadui zaidi kuliko watu (wote) kwa wale walioamini, ni Mayahudi na wale washirikina. Na bila shaka utawakuta walio karibu zaidi kwa mapenzi kwa Waumini ni wale wanaosema: “Sisi ni Manaswara.” Hivyo ni kwa kuwa miongoni mwao kuna Qissiysiyna (Makasisi) na Ruhbaan (Wamonaki - watawa) na kwamba wao hawatakabari.


وَإِذَا سَمِعُوا مَا أُنزِلَ إِلَى الرَّسُولِ تَرَىٰ أَعْيُنَهُمْ تَفِيضُ مِنَ الدَّمْعِ مِمَّا عَرَفُوا مِنَ الْحَقِّ ۖ يَقُولُونَ رَبَّنَا آمَنَّا فَاكْتُبْنَا مَعَ الشَّاهِدِينَ ﴿٨٣﴾
83. Na wanaposikia yale yaliyoteremshwa kwa Rasuli utaona macho yao yanachururika machozi kutokana na yale waliyoyatambua ya haki. Wanasema: “Rabb (Mola) wetu tumeamini, basi Tuandike pamoja na wenye kushuhudia.”


وَمَا لَنَا لَا نُؤْمِنُ بِاللَّـهِ وَمَا جَاءَنَا مِنَ الْحَقِّ وَنَطْمَعُ أَن يُدْخِلَنَا رَبُّنَا مَعَ الْقَوْمِ الصَّالِحِينَ ﴿٨٤﴾
84. “Na kwa nini Tusimwamini Allaah na haki iliyotufikia na hali tunatumai Rabb (Mola) wetu Atuingize (Jannah) pamoja na Swalihina?”


فَأَثَابَهُمُ اللَّـهُ بِمَا قَالُوا جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا ۚ وَذَٰلِكَ جَزَاءُ الْمُحْسِنِينَ ﴿٨٥﴾
85. Basi Allaah Akawalipa kwa yale waliyoyasema, Jannaat zipitizao chini yake mito, ni wenye kudumu humo. Na hiyo ndio jazaa ya wafanyao ihsaan.


وَالَّذِينَ كَفَرُوا وَكَذَّبُوا بِآيَاتِنَا أُولَـٰئِكَ أَصْحَابُ الْجَحِيمِ ﴿٨٦﴾
86. Na wale waliokufuru na wakazikadhibisha Aayaat (na ishara, dalili) Zetu hao ni watu wa (Moto wa) Al-Jahiym.


يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تُحَرِّمُوا طَيِّبَاتِ مَا أَحَلَّ اللَّـهُ لَكُمْ وَلَا تَعْتَدُوا ۚ إِنَّ اللَّـهَ لَا يُحِبُّ الْمُعْتَدِينَ ﴿٨٧﴾
87. Enyi mlioamini! Msiharamishe vizuri Aliyokuhalalishieni Allaah, na wala msitaadi. Hakika Allaah Hapendi wenye kutaadi.


وَكُلُوا مِمَّا رَزَقَكُمُ اللَّـهُ حَلَالًا طَيِّبًا ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ الَّذِي أَنتُم بِهِ مُؤْمِنُونَ ﴿٨٨﴾
88. Na kuleni katika vile Alivyowaruzuku Allaah vya halaal na vizuri. Na mcheni Allaah Ambaye nyinyi mnamwamini.


لَا يُؤَاخِذُكُمُ اللَّـهُ بِاللَّغْوِ فِي أَيْمَانِكُمْ وَلَـٰكِن يُؤَاخِذُكُم بِمَا عَقَّدتُّمُ الْأَيْمَانَ ۖ فَكَفَّارَتُهُ إِطْعَامُ عَشَرَةِ مَسَاكِينَ مِنْ أَوْسَطِ مَا تُطْعِمُونَ أَهْلِيكُمْ أَوْ كِسْوَتُهُمْ أَوْ تَحْرِيرُ رَقَبَةٍ ۖ فَمَن لَّمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ ۚ ذَٰلِكَ كَفَّارَةُ أَيْمَانِكُمْ إِذَا حَلَفْتُمْ ۚ وَاحْفَظُوا أَيْمَانَكُمْ ۚ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللَّـهُ لَكُمْ آيَاتِهِ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ ﴿٨٩﴾
89. Allaah Hatokuchukulieni kukuadhibuni kwa viapo vyenu vya upuuzi, lakini Atakuchukulieni kwa (kuvunja) viapo mlivyoapa kwa niyyah mlioifunga thabiti. Basi kafara yake (ya kuvunja viapo hivi) ni kulisha maskini kumi chakula cha wastani mnachowalisha ahli zenu, au kuwavisha nguo, au kuacha huru mtumwa. Lakini asiyeweza kupata (moja katika hayo), basi afunge Swiyaam siku tatu. Hiyo ndio kafara ya viapo vyenu mnapoapa. Na hifadhini viapo vyenu (msiape kila mara). Hivyo ndivyo Allaah Anavokubainishieni Aayaat (na hukmu) Zake mpate kushukuru.


يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّمَا الْخَمْرُ وَالْمَيْسِرُ وَالْأَنصَابُ وَالْأَزْلَامُ رِجْسٌ مِّنْ عَمَلِ الشَّيْطَانِ فَاجْتَنِبُوهُ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ ﴿٩٠﴾
90. Enyi mlioamini!  Hakika ulevi na kamari na (kuabudu) masanamu, na kutazamia kwa mishale ya kupigia ramli; (yote hayo) ni rijsun (uchafu) katika kitendo cha shaytwaan; basi jiepusheni navyo, mpate kufaulu.


إِنَّمَا يُرِيدُ الشَّيْطَانُ أَن يُوقِعَ بَيْنَكُمُ الْعَدَاوَةَ وَالْبَغْضَاءَ فِي الْخَمْرِ وَالْمَيْسِرِ وَيَصُدَّكُمْ عَن ذِكْرِ اللَّـهِ وَعَنِ الصَّلَاةِ ۖ فَهَلْ أَنتُم مُّنتَهُونَ ﴿٩١﴾
91. Hakika shaytwaan anataka kukutilieni baina yenu uadui na bughudha katika ulevi na kamari na akuzuieni na kumdhukuru Allaah na (akuzuieni pia) Swalaah; basi je mtaacha (maasi hayo)?



وَأَطِيعُوا اللَّـهَ وَأَطِيعُوا الرَّسُولَ وَاحْذَرُوا ۚ فَإِن تَوَلَّيْتُمْ فَاعْلَمُوا أَنَّمَا عَلَىٰ رَسُولِنَا الْبَلَاغُ الْمُبِينُ ﴿٩٢﴾
92. Na mtiini Allaah na mtiini Rasuli na tahadharini! Mkikengeuka, basi jueni kwamba juu ya Rasuli Wetu ni (jukumu tu la) kufikisha ujumbe bayana.


لَيْسَ عَلَى الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ جُنَاحٌ فِيمَا طَعِمُوا إِذَا مَا اتَّقَوا وَّآمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ ثُمَّ اتَّقَوا وَّآمَنُوا ثُمَّ اتَّقَوا وَّأَحْسَنُوا ۗ وَاللَّـهُ يُحِبُّ الْمُحْسِنِينَ ﴿٩٣﴾
93. Hakuna lawama juu ya wale walioamini na wakatenda mema katika vile walivyokula (kabla ya kuharimishwa) ikiwa watakuwa na taqwa na wakaamini na wakatenda mema; kisha wakawa na taqwa na wakaamini, kisha wakawa na taqwa na wakafanya ihsaan. Na Allaah Anapenda wafanyao ihsaan.


يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَيَبْلُوَنَّكُمُ اللَّـهُ بِشَيْءٍ مِّنَ الصَّيْدِ تَنَالُهُ أَيْدِيكُمْ وَرِمَاحُكُمْ لِيَعْلَمَ اللَّـهُ مَن يَخَافُهُ بِالْغَيْبِ ۚ فَمَنِ اعْتَدَىٰ بَعْدَ ذَٰلِكَ فَلَهُ عَذَابٌ أَلِيمٌ ﴿٩٤﴾
94. Enyi mlioamini! Bila shaka Allaah Atakujaribuni kwa baadhi ya wanyama wa kuwinda inayowafikia mikono yenu na mikuki yenu, ili Allaah Ajue mwenye kumkhofu kwa ghayb. Na atakayetaadi baada ya hayo, basi atapata adhabu iumizayo.


يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَقْتُلُوا الصَّيْدَ وَأَنتُمْ حُرُمٌ ۚ وَمَن قَتَلَهُ مِنكُم مُّتَعَمِّدًا فَجَزَاءٌ مِّثْلُ مَا قَتَلَ مِنَ النَّعَمِ يَحْكُمُ بِهِ ذَوَا عَدْلٍ مِّنكُمْ هَدْيًا بَالِغَ الْكَعْبَةِ أَوْ كَفَّارَةٌ طَعَامُ مَسَاكِينَ أَوْ عَدْلُ ذَٰلِكَ صِيَامًا لِّيَذُوقَ وَبَالَ أَمْرِهِ ۗ عَفَا اللَّـهُ عَمَّا سَلَفَ ۚ وَمَنْ عَادَ فَيَنتَقِمُ اللَّـهُ مِنْهُ ۗ وَاللَّـهُ عَزِيزٌ ذُو انتِقَامٍ ﴿٩٥﴾
95. Enyi mlioamini! Msiue mawindo na hali mko katika ihraam. Na atakayemuua (mnyama) miongoni mwenu kwa kusudi, basi malipo yake itakuwa (kuchinja) kilicho sawa na alichokiua katika wanyama (wa mifugo wa malishoni). Ahukumu kwacho (watu) wawili walio waadilifu miongoni mwenu. Mnyama huyo afikishwe Ka’bah (akachinjwe), au kafara ya kulisha maskini, au badala ya hayo, kufunga swiyaam ili aonje matokeo maovu ya jambo lake. Allaah Ameshasamehe yaliyopita; na yeyote atakayerudia (kufanya) tena, basi Allaah Atamlipizia (adhabu). Na Allaah ni ‘Aziyz (Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika), Mwenye kulipiza.


أُحِلَّ لَكُمْ صَيْدُ الْبَحْرِ وَطَعَامُهُ مَتَاعًا لَّكُمْ وَلِلسَّيَّارَةِ ۖ وَحُرِّمَ عَلَيْكُمْ صَيْدُ الْبَرِّ مَا دُمْتُمْ حُرُمًا ۗ وَاتَّقُوا اللَّـهَ الَّذِي إِلَيْهِ تُحْشَرُونَ ﴿٩٦﴾
96. Mmehalalishiwa mawindo ya bahari na chakula chake ni manufaa kwenu na kwa wasafiri. Na mmeharamishiwa mawindo ya nchi kavu madamu mtakuwa katika ihraam. Na mcheni Allaah Ambaye Kwake (Pekee) mtakusanywa.


جَعَلَ اللَّـهُ الْكَعْبَةَ الْبَيْتَ الْحَرَامَ قِيَامًا لِّلنَّاسِ وَالشَّهْرَ الْحَرَامَ وَالْهَدْيَ وَالْقَلَائِدَ ۚ ذَٰلِكَ لِتَعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ يَعْلَمُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ وَأَنَّ اللَّـهَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ ﴿٩٧﴾
97. Allaah Amejaalia Ka’bah Nyumba Tukufu kuwa simamio (tegemeo) la watu, na (pia Ameijaalia) miezi mitukufu na wanyama wa kafara (dhabihu) na vigwe (alama ya waliokusudiwa kafara).  Hivyo ili mpate kujua kuwa Allaah Anajua yale yaliyomo mbinguni na ardhini na kwamba Allaah ni kwa kila kitu ‘Aliym (Mjuzi).



اعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ شَدِيدُ الْعِقَابِ وَأَنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿٩٨﴾
98. Jueni kuwa Allaah ni Mkali wa kuakibu na kwamba Allaah ni Ghafuwrur-Rahiym (Mwingi wa kughufuria - Mwenye kurehemu).


مَّا عَلَى الرَّسُولِ إِلَّا الْبَلَاغُ ۗ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ مَا تُبْدُونَ وَمَا تَكْتُمُونَ ﴿٩٩﴾
99. Hapana (jukumu) juu ya Rasuli ila ubalighisho wa ujumbe. Na Allaah Anayajua yale mnayoyadhihirisha na yale mnayoyaficha.


قُل لَّا يَسْتَوِي الْخَبِيثُ وَالطَّيِّبُ وَلَوْ أَعْجَبَكَ كَثْرَةُ الْخَبِيثِ ۚ فَاتَّقُوا اللَّـهَ يَا أُولِي الْأَلْبَابِ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ ﴿١٠٠﴾
100. Sema: “Haviwi sawasawa khabiyth (watu waovu na kila uovu; kauli, amali n.k) na twayyib (watu wema na kila zuri) japokuwa utakupendekezea wingi wa khabiyth”. Basi mcheni Allaah, enyi wenye akili ili mpate kufaulu.


يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَسْأَلُوا عَنْ أَشْيَاءَ إِن تُبْدَ لَكُمْ تَسُؤْكُمْ وَإِن تَسْأَلُوا عَنْهَا حِينَ يُنَزَّلُ الْقُرْآنُ تُبْدَ لَكُمْ عَفَا اللَّـهُ عَنْهَا ۗ وَاللَّـهُ غَفُورٌ حَلِيمٌ ﴿١٠١﴾
101. Enyi mlioamini! Msiulizie mambo ambayo mkifichuliwa yatakusikitisheni. Na mkiyaulizia pale inapoteremshwa Qur-aan mtafichuliwa. Allaah Ameyasamehe hayo. Na Allaah ni Ghafuwrun-Haliym (Mwingi wa kughufuria - Mpole wa kuwavumilia waja).


قَدْ سَأَلَهَا قَوْمٌ مِّن قَبْلِكُمْ ثُمَّ أَصْبَحُوا بِهَا كَافِرِينَ ﴿١٠٢﴾
102. Walikwishayauliza (mambo) hayo watu wa kabla yenu, kisha wakawa kwayo ni makafiri.


مَا جَعَلَ اللَّـهُ مِن بَحِيرَةٍ وَلَا سَائِبَةٍ وَلَا وَصِيلَةٍ وَلَا حَامٍ ۙ وَلَـٰكِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا يَفْتَرُونَ عَلَى اللَّـهِ الْكَذِبَ ۖ وَأَكْثَرُهُمْ لَا يَعْقِلُونَ ﴿١٠٣﴾
103. Allaah Hakujaalia (uharamu wowote wa) bahiyrah (ngamia aliyezaa matumbo matano), wala saaibah (ngamia aliyeachiliwa kwa nadhiri), wala waswiylah (kondoo aliyezaa matumbo saba), wala haam (fahali lililozalisha matumbo kumi), lakini wale waliokufuru wanamtungia Allaah uongo, na wengi wao hawatumii akili.

وَإِذَا قِيلَ لَهُمْ تَعَالَوْا إِلَىٰ مَا أَنزَلَ اللَّـهُ وَإِلَى الرَّسُولِ قَالُوا حَسْبُنَا مَا وَجَدْنَا عَلَيْهِ آبَاءَنَا ۚ أَوَلَوْ كَانَ آبَاؤُهُمْ لَا يَعْلَمُونَ شَيْئًا وَلَا يَهْتَدُونَ ﴿١٠٤﴾
104. Na wanapoambiwa: “Njooni (katika) yale Aliyoyateremsha Allaah na kwa Rasuli” Husema: “Yanatutosheleza yale tuliyowakuta nayo baba zetu”. Je, japokuwa walikuwa baba zao hawajui chochote na wala hawakuongoka?


يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا عَلَيْكُمْ أَنفُسَكُمْ ۖ لَا يَضُرُّكُم مَّن ضَلَّ إِذَا اهْتَدَيْتُمْ ۚ إِلَى اللَّـهِ مَرْجِعُكُمْ جَمِيعًا فَيُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ﴿١٠٥﴾
105. Enyi mlioamini! Ni juu yenu (majukumu ya) nafsi zenu. Hawakudhuruni waliopotoka ikiwa mmeongoka. Kwa Allaah Pekee ni marejeo yenu nyote, kisha Atakujulisheni kwa yale mliyokuwa mkiyatenda.



يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا شَهَادَةُ بَيْنِكُمْ إِذَا حَضَرَ أَحَدَكُمُ الْمَوْتُ حِينَ الْوَصِيَّةِ اثْنَانِ ذَوَا عَدْلٍ مِّنكُمْ أَوْ آخَرَانِ مِنْ غَيْرِكُمْ إِنْ أَنتُمْ ضَرَبْتُمْ فِي الْأَرْضِ فَأَصَابَتْكُم مُّصِيبَةُ الْمَوْتِ ۚ تَحْبِسُونَهُمَا مِن بَعْدِ الصَّلَاةِ فَيُقْسِمَانِ بِاللَّـهِ إِنِ ارْتَبْتُمْ لَا نَشْتَرِي بِهِ ثَمَنًا وَلَوْ كَانَ ذَا قُرْبَىٰ ۙ وَلَا نَكْتُمُ شَهَادَةَ اللَّـهِ إِنَّا إِذًا لَّمِنَ الْآثِمِينَ ﴿١٠٦﴾
106. Enyi mlioamini! Ushahidi (uweko kushuhudiwa) baina yenu yanapohudhuria mauti (kwa) mmoja wenu wakati anapousia. Waweko (mashahidi) wawili wenye uadilifu miongoni mwenu; au wawili wengine ghairi yenu (wasio Waislamu) mnapokuwa safarini ukakufikeni msiba wa mauti. Muwazuie (wawili hao) baada ya Swalaah, na waape kwa (jina la) Allaah mkitilia shaka (ushahidi wao. Hivyo waseme): “Hatutobadilisha kwayo (viapo vyetu) kwa thamani yoyote ile japo akiwa ni jamaa yetu wa karibu. Na wala hatutoficha ushuhuda wa   Allaah. (Kwani tukifanya hivyo) hakika hapo tutakuwa miongoni mwa wenye kutenda dhambi.”


فَإِنْ عُثِرَ عَلَىٰ أَنَّهُمَا اسْتَحَقَّا إِثْمًا فَآخَرَانِ يَقُومَانِ مَقَامَهُمَا مِنَ الَّذِينَ اسْتَحَقَّ عَلَيْهِمُ الْأَوْلَيَانِ فَيُقْسِمَانِ بِاللَّـهِ لَشَهَادَتُنَا أَحَقُّ مِن شَهَادَتِهِمَا وَمَا اعْتَدَيْنَا إِنَّا إِذًا لَّمِنَ الظَّالِمِينَ ﴿١٠٧﴾
107. Ikigundilikana kwamba hao wawili wana hatia ya dhambi (kwa kusema uongo katika waliyoyashuhudia); basi wawili wengine wasimame mahali pao katika walio karibu zaidi (na mrithiwa) miongoni mwa waliokuwa na haki ki-shariy’ah; basi waape kwa (jina la) Allaah (kwa kusema): “Bila shaka ushahidi wetu ni wa kweli zaidi kuliko ushahidi (wa wawili) wao; nasi hatukutaadi; (ikiwa tumefanya hivyo), hakika hapo tutakuwa miongoni mwa madhalimu.


ذَٰلِكَ أَدْنَىٰ أَن يَأْتُوا بِالشَّهَادَةِ عَلَىٰ وَجْهِهَا أَوْ يَخَافُوا أَن تُرَدَّ أَيْمَانٌ بَعْدَ أَيْمَانِهِمْ ۗ وَاتَّقُوا اللَّـهَ وَاسْمَعُوا ۗ وَاللَّـهُ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الْفَاسِقِينَ ﴿١٠٨﴾
108. Hivyo inaelekea zaidi ya kwamba watatoa ushahidi kama ipasavyo au watakhofu visije vikaletwa viapo (vingine) baada ya viapo vyao. Na mcheni Allaah na sikizeni!  Na Allaah Haongoi watu mafasiki.


يَوْمَ يَجْمَعُ اللَّـهُ الرُّسُلَ فَيَقُولُ مَاذَا أُجِبْتُمْ ۖ قَالُوا لَا عِلْمَ لَنَا ۖ إِنَّكَ أَنتَ عَلَّامُ الْغُيُوبِ ﴿١٠٩﴾
109. (Tahadharini) Siku Allaah Atakayowakusanya Rasuli na Kuwaambia: “Mlijibiwa nini?” (Rasuli) Watasema: “Hatuna ujuzi nalo; hakika Wewe Ndiye ‘Allaamu (Mjuzi) wa ghayb.


إِذْ قَالَ اللَّـهُ يَا عِيسَى ابْنَ مَرْيَمَ اذْكُرْ نِعْمَتِي عَلَيْكَ وَعَلَىٰ وَالِدَتِكَ إِذْ أَيَّدتُّكَ بِرُوحِ الْقُدُسِ تُكَلِّمُ النَّاسَ فِي الْمَهْدِ وَكَهْلًا ۖ وَإِذْ عَلَّمْتُكَ الْكِتَابَ وَالْحِكْمَةَ وَالتَّوْرَاةَ وَالْإِنجِيلَ ۖ وَإِذْ تَخْلُقُ مِنَ الطِّينِ كَهَيْئَةِ الطَّيْرِ بِإِذْنِي فَتَنفُخُ فِيهَا فَتَكُونُ طَيْرًا بِإِذْنِي ۖ وَتُبْرِئُ الْأَكْمَهَ وَالْأَبْرَصَ بِإِذْنِي ۖ وَإِذْ تُخْرِجُ الْمَوْتَىٰ بِإِذْنِي ۖ وَإِذْ كَفَفْتُ بَنِي إِسْرَائِيلَ عَنكَ إِذْ جِئْتَهُم بِالْبَيِّنَاتِ فَقَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْهُمْ إِنْ هَـٰذَا إِلَّا سِحْرٌ مُّبِينٌ ﴿١١٠﴾
110. (Siku) Allaah Ataposema: “Ee ‘Iysaa mwana wa Maryam! Kumbuka neema Yangu juu yako na juu ya mama yako; Nilipokusaidia kwa Ruwhil-Qudus (Jibriyl (عليه السلام; unasemesha watu katika utoto na utuuzimani; na (kumbuka) Nilipokufunza Kitabu na Hikmah na Tawraat na Injiyl; na (kumbuka pale) ulipotengeneza kutokana na udongo kama umbo la ndege kwa idhini Yangu; ukapulizia likawa ndege kwa idhini Yangu; na ulipowaponyesha vipofu na ubarasi kwa idhini Yangu; na ulipowatoa wafu (kutoka makaburini mwao) kwa idhini Yangu; na Nilipowazuia wana wa Israaiyl dhidi yako (kutaka kuua) ulipowajia kwa hoja bayana; wakasema wale waliokufuru miongoni mwao: “Haya si chochote ila ni sihiri bayana.”


وَإِذْ أَوْحَيْتُ إِلَى الْحَوَارِيِّينَ أَنْ آمِنُوا بِي وَبِرَسُولِي قَالُوا آمَنَّا وَاشْهَدْ بِأَنَّنَا مُسْلِمُونَ ﴿١١١﴾
111. Na (kumbuka pale) Nilipowatia ilhamu Al-Hawariyyiyna (wafuasi, Answaar wako) kwamba: “Niaminini Mimi na Rasuli Wangu.” Wakasema: “Tumeamini na shuhudia kwamba sisi ni Waislamu (tuliojisalimisha kwa Allaah).”


إِذْ قَالَ الْحَوَارِيُّونَ يَا عِيسَى ابْنَ مَرْيَمَ هَلْ يَسْتَطِيعُ رَبُّكَ أَن يُنَزِّلَ عَلَيْنَا مَائِدَةً مِّنَ السَّمَاءِ ۖ قَالَ اتَّقُوا اللَّـهَ إِن كُنتُم مُّؤْمِنِينَ ﴿١١٢﴾
112. (Kumbuka pale) waliposema Al-Hawariyyiyna: “Ee ‘Iysaa mwana wa Maryam! Je Anaweza Rabb (Mola) wako Kututeremshia maaidah (meza iliyotandazwa chakula) kutoka mbinguni?” (‘Iysaa) Akasema: “Mcheni Allaah, kama nyinyi ni Waumini.”


قَالُوا نُرِيدُ أَن نَّأْكُلَ مِنْهَا وَتَطْمَئِنَّ قُلُوبُنَا وَنَعْلَمَ أَن قَدْ صَدَقْتَنَا وَنَكُونَ عَلَيْهَا مِنَ الشَّاهِدِينَ ﴿١١٣﴾
113. (Al-Hawariyyiyna) Wakasema: “Tunataka kula katika hicho; na (ili) nyoyo zetu zitulie; na tujue kwamba kwa yakini umetuambia kweli; na kwayo tuwe miongoni wa wanaoshuhudia.”


قَالَ عِيسَى ابْنُ مَرْيَمَ اللَّـهُمَّ رَبَّنَا أَنزِلْ عَلَيْنَا مَائِدَةً مِّنَ السَّمَاءِ تَكُونُ لَنَا عِيدًا لِّأَوَّلِنَا وَآخِرِنَا وَآيَةً مِّنكَ ۖ وَارْزُقْنَا وَأَنتَ خَيْرُ الرَّازِقِينَ ﴿١١٤﴾
114. Akasema ‘Iysaa mwana wa Maryam: “Ee Allaah, Rabb (Mola) wetu, Tuteremshie maaidah kutoka mbinguni (ili) iwe kwetu ni sikukuu kwa wa mwanzo wetu na wa mwisho wetu; na iwe Aayah (ishara, hoja) itokayo Kwako; basi Turuzuku; kwani Wewe ni Mbora wa wenye kuruzuku”.


قَالَ اللَّـهُ إِنِّي مُنَزِّلُهَا عَلَيْكُمْ ۖ فَمَن يَكْفُرْ بَعْدُ مِنكُمْ فَإِنِّي أُعَذِّبُهُ عَذَابًا لَّا أُعَذِّبُهُ أَحَدًا مِّنَ الْعَالَمِينَ ﴿١١٥﴾
115. Akasema Allaah: “Hakika Mimi Nitaiteremsha kwenu; (lakini) atakayekufuru miongoni mwenu baada ya hapo; basi hakika Nitamuadhibu adhabu (ambayo) Sitomuadhibu mmoja yeyote katika walimwengu.”


وَإِذْ قَالَ اللَّـهُ يَا عِيسَى ابْنَ مَرْيَمَ أَأَنتَ قُلْتَ لِلنَّاسِ اتَّخِذُونِي وَأُمِّيَ إِلَـٰهَيْنِ مِن دُونِ اللَّـهِ ۖ قَالَ سُبْحَانَكَ مَا يَكُونُ لِي أَنْ أَقُولَ مَا لَيْسَ لِي بِحَقٍّ ۚ إِن كُنتُ قُلْتُهُ فَقَدْ عَلِمْتَهُ ۚ تَعْلَمُ مَا فِي نَفْسِي وَلَا أَعْلَمُ مَا فِي نَفْسِكَ ۚ إِنَّكَ أَنتَ عَلَّامُ الْغُيُوبِ ﴿١١٦﴾
116. Na (Tahadhari Siku) Allaah Atakaposema: “Ee ‘Iysaa mwana wa Maryam!  Je, wewe uliwaambia watu: “Nifanyeni mimi na mama yangu kuwa ni miungu miwili pasi naya Allaah?” (‘Iysaa) Atasema: “Subhaanak (Utakasifu ni Wako)! Hainipasi mimi kusema yasiyo kuwa haki kwangu; ikiwa nimesema hayo basi kwa yakini Ungeliyajua; Unayajua yale yote yaliyomo katika nafsi yangu; na wala (mimi) sijui yale yaliyomo katika Nafsi Yako; hakika Wewe ni ‘Allaamu (Mjuzi) wa ghayb.


مَا قُلْتُ لَهُمْ إِلَّا مَا أَمَرْتَنِي بِهِ أَنِ اعْبُدُوا اللَّـهَ رَبِّي وَرَبَّكُمْ ۚ وَكُنتُ عَلَيْهِمْ شَهِيدًا مَّا دُمْتُ فِيهِمْ ۖ فَلَمَّا تَوَفَّيْتَنِي كُنتَ أَنتَ الرَّقِيبَ عَلَيْهِمْ ۚ وَأَنتَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ شَهِيدٌ ﴿١١٧﴾
117. “Sijawaambia (lolote) ila yale Uliyoniamrisha kwayo kwamba: Mwabuduni Allaah Rabb (Mola) wangu na Rabb wenu. Na nilikuwa juu yao shahidi wakati nilipokuwa nao. Uliponichukua juu (mbinguni) Ulikuwa Wewe Ar-Raqiyba (Mwenye kuchunga) juu yao. Na Wewe juu ya kila kitu ni Shahiyd” (Mwenye kushuhudia).


إِن تُعَذِّبْهُمْ فَإِنَّهُمْ عِبَادُكَ ۖ وَإِن تَغْفِرْ لَهُمْ فَإِنَّكَ أَنتَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ ﴿١١٨﴾
118. “Ukiwaadhibu, basi bila shaka hao ni waja Wako; na Ukiwaghufuria basi hakika Wewe Ndiye Al-‘Aziyzul-Hakiym” (Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika - Mwenye hikmah wa yote).


قَالَ اللَّـهُ هَـٰذَا يَوْمُ يَنفَعُ الصَّادِقِينَ صِدْقُهُمْ ۚ لَهُمْ جَنَّاتٌ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا أَبَدًا ۚ رَّضِيَ اللَّـهُ عَنْهُمْ وَرَضُوا عَنْهُ ۚ ذَٰلِكَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ ﴿١١٩﴾
119. Allaah Atasema: “Hii ndiyo Siku itakayowafaa as-Swaadiqiyna ukweli wao; watapata Jannaat zipitazo chini yake mito; ni wenye kudumu humo abadi.  Allaah Ameridhika nao, nao wameridhika Naye. Huko ni kufuzu adhimu.”


لِلَّـهِ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا فِيهِنَّ ۚ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿١٢٠﴾
120. Ni wa Allaah (Pekee) ufalme wa mbingu na ardhi na yale yote yaliyomo humo.  Naye juu ya kila kitu ni Qadiyr (Muweza).


Ukitaka kusoma Sura nyengine Rejeauliko toka
Ukiwa una shauri au maelezo juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii falhaqqiy@gmail.com