Hadithi Ya 07: Dini Ni Nasiha

الحديث السابع
"الدين النصيحة"


 عن أبي رُقَيَّةَ تَمِيمِ بنِ أوْسٍ الدَّارِيِّ رضي اللهُ عنه: أَنَّ النَّبي صلى الله عليه وسلم قالَ:((الدِّينُ النَّصِيحَةُ)). قُلْنَا: لِمَنْ ؟ قالَ: ((للهِ، ولِكِتَابِهِ، ولِرَسُولِهِ، ولِلأَئِمةِ المُسْلِمِينَ، وعامَّتِهِمْ))

رَوَاهُ مُسْلِمٌ    
HADITHI YA 7
DINI NI NASIHA
Kutoka kwa Abu Ruqayyah Tamim Ibn Aus Addarryرضي الله عنه  ambaye amesema kuwa Bwana Mtume صلى الله عليه وسلم  kasema:
Dini ni nasiha.  Tukauliza: Kwa nani? Akasema kwa Allaah (Kukiri Uungu wake na kwamba Hana mshirika), Kitabu chake (Kukubali kuwa ni maneno ya Allah yasiyo na shaka), na Mtume wake (Kumkubali na kukubali ujumbe aliotumwa nao), na kwa Viongozi wa Waislamu (Kuwatii na kuwafuata katika mema na kuwaasa katika yale wanayokwenda nayo kinyume), na watu wa kawaida (kuusiana mema na kukatazana mabaya kwa njia nzuri).
Imesimuliwa na Muslim