سُورَةُ الإِنْسَان
Al-Insaan (76)
بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ
هَلْ أَتَىٰ عَلَى الْإِنسَانِ حِينٌ مِّنَ الدَّهْرِ لَمْ يَكُن شَيْئًا مَّذْكُورًا ﴿١﴾
|
1. Je, haukumpitia insani wakati katika dahari, hakuwa kitu kinachotajwa? |
إِنَّا خَلَقْنَا الْإِنسَانَ مِن نُّطْفَةٍ أَمْشَاجٍ نَّبْتَلِيهِ فَجَعَلْنَاهُ سَمِيعًا بَصِيرًا ﴿٢﴾
|
2. Hakika Sisi Tumemuumba insani kutokana na tone la manii iliyochanganyika ili Tumjaribu; Tukamjaalia mwenye kusikia na kuona. |
إِنَّا هَدَيْنَاهُ السَّبِيلَ إِمَّا شَاكِرًا وَإِمَّا كَفُورًا ﴿٣﴾
|
3. Hakika Sisi Tumemuongoza njia; (basi) ima (awe) mwenye kushukuru au (awe) mwenye kukufuru. |
إِنَّا أَعْتَدْنَا لِلْكَافِرِينَ سَلَاسِلَ وَأَغْلَالًا وَسَعِيرًا ﴿٤﴾
|
4. Hakika Sisi Tumewaandalia makafiri minyororo, na pingu na (Moto wa) Sa’iyraa (uwakao kwa nguvu).” |
إِنَّ الْأَبْرَارَ يَشْرَبُونَ مِن كَأْسٍ كَانَ مِزَاجُهَا كَافُورًا ﴿٥﴾
|
5. Hakika Al-Abraar (watu wema) watakunywa katika gilasi (kinywaji cha) mchanganyiko wa kafuri. |
عَيْنًا يَشْرَبُ بِهَا عِبَادُ اللَّـهِ يُفَجِّرُونَهَا تَفْجِيرًا ﴿٦﴾
|
6. Chemchemu watakayokunywa humo waja wa Allaah, watabubujua mbubujiko. |
يُوفُونَ بِالنَّذْرِ وَيَخَافُونَ يَوْمًا كَانَ شَرُّهُ مُسْتَطِيرًا ﴿٧﴾
|
7. (Ambao) Wanatimiza nadhiri (zao), na wanaiogopa siku ambayo shari yake ni yenye kuenea. |
وَيُطْعِمُونَ الطَّعَامَ عَلَىٰ حُبِّهِ مِسْكِينًا وَيَتِيمًا وَأَسِيرًا ﴿٨﴾
|
8. Na wanalisha chakula juu ya mapenzi yao (kwa hicho wanacholisha) masikini na mayatima na mateka. |
إِنَّمَا نُطْعِمُكُمْ لِوَجْهِ اللَّـهِ لَا نُرِيدُ مِنكُمْ جَزَاءً وَلَا شُكُورًا ﴿٩﴾
|
9. “Hakika sisi tunakulisheni kwa (ajili ya) Wajihi wa Allaah, hatutaki kwenu jazaa na wala shukurani. |
إِنَّا نَخَافُ مِن رَّبِّنَا يَوْمًا عَبُوسًا قَمْطَرِيرًا ﴿١٠﴾
|
10. “Hakika sisi tunakhofu kwa Rabb (Mola) wetu siku inayokunjisha uso ngumu nzito. |
فَوَقَاهُمُ اللَّـهُ شَرَّ ذَٰلِكَ الْيَوْمِ وَلَقَّاهُمْ نَضْرَةً وَسُرُورًا ﴿١١﴾
|
11. Basi Allaah Atawakinga na shari ya siku hiyo, na Atawakutanisha na mng’ao na furaha. |
وَجَزَاهُم بِمَا صَبَرُوا جَنَّةً وَحَرِيرًا ﴿١٢﴾
|
12. Na Atawalipa Jannah na (nguo za) hariri kwa kusubiri kwao. |
مُّتَّكِئِينَ فِيهَا عَلَى الْأَرَائِكِ ۖ لَا يَرَوْنَ فِيهَا شَمْسًا وَلَا زَمْهَرِيرًا ﴿١٣﴾
|
13. Wataegemea humo juu ya makochi (ya fakhari), hawatoona humo joto la jua wala baridi kali. |
وَدَانِيَةً عَلَيْهِمْ ظِلَالُهَا وَذُلِّلَتْ قُطُوفُهَا تَذْلِيلًا ﴿١٤﴾
|
14. Na vivuli (vyake) vitakuwa karibu yao, na kuchumwa kwake (matunda) yamening’inizwa (wayafikie). |
وَيُطَافُ عَلَيْهِم بِآنِيَةٍ مِّن فِضَّةٍ وَأَكْوَابٍ كَانَتْ قَوَارِيرَا ﴿١٥﴾
|
15. Na watazungushiwa vyombo vya fedha, na vikombe vilivyokuwa vya vigae. |
قَوَارِيرَ مِن فِضَّةٍ قَدَّرُوهَا تَقْدِيرًا ﴿١٦﴾
|
16. Vikombe vya vigae vya fedha wamevipima kwa kipimo. |
وَيُسْقَوْنَ فِيهَا كَأْسًا كَانَ مِزَاجُهَا زَنجَبِيلًا ﴿١٧﴾
|
17. Na watanyweshwa humo gilasi (kinywaji) mchanganyiko wake wa tangawizi. |
عَيْنًا فِيهَا تُسَمَّىٰ سَلْسَبِيلًا ﴿١٨﴾
|
18. Chemchemu inayoitwa Salsabiylaa. |
وَيَطُوفُ عَلَيْهِمْ وِلْدَانٌ مُّخَلَّدُونَ إِذَا رَأَيْتَهُمْ حَسِبْتَهُمْ لُؤْلُؤًا مَّنثُورًا ﴿١٩﴾
|
19. Na watawazungukia wavulana wa kudumu (kuwatumikia), utakapowaona, utawadhania ni lulu zilizotawanywa. |
وَإِذَا رَأَيْتَ ثَمَّ رَأَيْتَ نَعِيمًا وَمُلْكًا كَبِيرًا ﴿٢٠﴾
|
20. Na utakapoyaona (hayo yaliyoko), utaona neema (zisizo kifani) na ufalme mkubwa. |
عَالِيَهُمْ ثِيَابُ سُندُسٍ خُضْرٌ وَإِسْتَبْرَقٌ ۖ وَحُلُّوا أَسَاوِرَ مِن فِضَّةٍ وَسَقَاهُمْ رَبُّهُمْ شَرَابًا طَهُورًا ﴿٢١﴾
|
21. Juu yao wana nguo nzuri za hariri laini za kijani (kibichi) na za hariri nzito, na watapambwa bangili (vikuku) vya fedha; na Rabb (Mola) wao Atawanywesha kinywaji safi kabisa. |
إِنَّ هَـٰذَا كَانَ لَكُمْ جَزَاءً وَكَانَ سَعْيُكُم مَّشْكُورًا ﴿٢٢﴾
|
22. (Waatambiwa): “Hakika haya ni jazaa yenu, kwani juhudi zenu (za kutenda ‘amali duniani) zimethaminiwa.” |
إِنَّا نَحْنُ نَزَّلْنَا عَلَيْكَ الْقُرْآنَ تَنزِيلًا ﴿٢٣﴾
|
23. Hakika Sisi Tumekuteremshia (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) Qur-aan uteremsho wa hatua kwa hatua. |
فَاصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ وَلَا تُطِعْ مِنْهُمْ آثِمًا أَوْ كَفُورًا ﴿٢٤﴾
|
24. Basi subiri hukumu ya Rabb (Mola) wako, na wala usimtii miongoni mwao atendaye dhambi au mwenye kukufuru. |
وَاذْكُرِ اسْمَ رَبِّكَ بُكْرَةً وَأَصِيلًا ﴿٢٥﴾
|
25. Na lidhukuru Jina la Rabb (Mola) wako asubuhi na jioni. |
وَمِنَ اللَّيْلِ فَاسْجُدْ لَهُ وَسَبِّحْهُ لَيْلًا طَوِيلًا ﴿٢٦﴾
|
26. Na katika usiku, msujudie na msabbih usiku (muda) mrefu. |
إِنَّ هَـٰؤُلَاءِ يُحِبُّونَ الْعَاجِلَةَ وَيَذَرُونَ وَرَاءَهُمْ يَوْمًا ثَقِيلًا ﴿٢٧﴾
|
27. Hakika hawa (makafiri) wanapenda (uhai wa dunia) unaopita haraka kwa muda tu, na wanaacha nyuma yao siku nzito (ya Qiyamaah). |
نَّحْنُ خَلَقْنَاهُمْ وَشَدَدْنَا أَسْرَهُمْ ۖ وَإِذَا شِئْنَا بَدَّلْنَا أَمْثَالَهُمْ تَبْدِيلًا ﴿٢٨﴾
|
28. Sisi Tumewaumba, na Tumetia nguvu viungo vyao; na kama Tukitaka, Tutawabadilisha kama wao mbadiliko (kamilifu). |
إِنَّ هَـٰذِهِ تَذْكِرَةٌ ۖ فَمَن شَاءَ اتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِ سَبِيلًا ﴿٢٩﴾
|
29. Hakika hii ni tadhkirah (ukumbusho), basi anayetaka achukue njia ya (kuelea kwa) Rabb (Mola) wake. |
وَمَا تَشَاءُونَ إِلَّا أَن يَشَاءَ اللَّـهُ ۚ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلِيمًا حَكِيمًا ﴿٣٠﴾
|
30. Na (hamtoweza) kutaka (chochote kile mkitakacho) isipokuwa Atake Allaah; hakika Allaah daima ni ‘Aliyman-Hakiymaa (Mjuzi wa yote - Mwenye hikimah wa yote). |
يُدْخِلُ مَن يَشَاءُ فِي رَحْمَتِهِ ۚ وَالظَّالِمِينَ أَعَدَّ لَهُمْ عَذَابًا أَلِيمًا ﴿٣١﴾
|
31. Anamuingiza Amtakaye katika Rahmah Yake, na madhalimu Amewaandalia adhabu iumizayo.
Ukitaka kusoma Sura nyengine Rejeauliko toka
Ukiwa una shauri au maelezo juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii falhaqqiy@gmail.com |