Kuna Idadi Maalum ya Rakaa kwa Sala za Usiku?



KUNA IDADI YA RAKAA – QIYAAMU LLAYL ?


Hakuna uthibitisho unaoelezea kama sala za usiku zina idadi za rakaa maalum. Ila sunna iliyothibiti  husaliwa rakaa mbili mbili kama ilivyopokelewa na Ibnu ‘Umar Allah awawie radhi(yeye na baba yake) kutoka kwa hadithi ya Mtume Salla Allahu ‘Alayhi Wasallam

صلاة الليل مثنى مثنى فإذا خشي أحدكم الصبح صلى ركعة واحدة توتر له ما قد صلى

Sala za usiku (husaliwa) rakaa mbili mbili na akichelea mmoja wenu kufikiwa na Alfajiri asali rakaa moja ambayo huwa witr aliyoisali
                                        Bukhari na Muslim

Katika Fataawa za Ibnu Tamiyah amesema

( ومن ظنَّ أن قيام رمضان فيه عدد موقت عن النبي- صلى الله عليه وسلم- لا يزاد
                                                          ولا ينقص منه فقد أخطأ ) فيه  
الفتاوى 22/272

Mwenye kudhani kwamba sala za usiku za Ramadhaan zimeekewa idadi maalum na Mtume Salla Allahu ‘Alayhi Wasallam haizidi wala haipungui basi amekosea.

Fataawa 22/272

فقد سئلت عائشة رضي الله عنها : بكم كان رسول الله صلى الله عليه وسلم يوتر ؟ قالت : " كان يوتر بأربع وثلاث، وست وثلاث، وعشر وثلاث، ولم يكن يوتر بأنقص من سبع ولا بأكثر من ثلاث عشرة " رواه أبو داود وأحمد وغيرهما.  

،
Aliwahi kuulizwa bibi ‘Aishah Allah amuwie radhi : “Mtume Salla Allahu ‘Alayhi Wasallam  alikuwa akisali Witr rakaa ngapi? Akasema : Alikuwa  akisali rakaa nne kisha husali tatu na akisali sita na (kisha) tatu na kumi (kisha) na tatu na alikuwa hapunguzi chini ya rakaa saba na wala hazidishi zaidi ya kumi na tatu

                              Abu Daaud na Ahmad na wengineo