إِبْرَاهِيم
14. SURAT IBRAAHIYM
(Imeteremka Makka)
بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ
الر ۚ
كِتَابٌ أَنزَلْنَاهُ إِلَيْكَ لِتُخْرِجَ النَّاسَ مِنَ الظُّلُمَاتِ
إِلَى النُّورِ بِإِذْنِ رَبِّهِمْ إِلَىٰ صِرَاطِ الْعَزِيزِ الْحَمِيدِ ﴿١﴾
1. Alif Laam Raa. Kitabu Tumekiteremsha kwako (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) ili uwatoe watu katika viza kuwaingiza katika nuru kwa idhini ya Rabb (Mola) wao, waelekee katika njia ya Al-‘Aziyzil-Hamiyd (Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika - Mwenye kustahiki kuhimidiwa kwa yote).
اللَّـهِ الَّذِي لَهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ ۗ وَوَيْلٌ لِّلْكَافِرِينَ مِنْ عَذَابٍ شَدِيدٍ ﴿٢﴾
2. Allaah Ambaye ni Vyake Pekee (vyote) viliyomo katika mbingu na katika ardhi. Na ole kwa makafiri kutokana na adhabu kali.
الَّذِينَ يَسْتَحِبُّونَ الْحَيَاةَ الدُّنْيَا عَلَى الْآخِرَةِ وَيَصُدُّونَ عَن سَبِيلِ اللَّـهِ وَيَبْغُونَهَا عِوَجًا ۚ أُولَـٰئِكَ فِي ضَلَالٍ بَعِيدٍ ﴿٣﴾
3. Ambao wanaositahabu uhai wa dunia
kuliko wa Aakhirah, na wanazuia (watu) njia ya Allaah, na wanaitakia
upogo (kosa). Hao wamo katika upotofu wa mbali.
وَمَا أَرْسَلْنَا مِن رَّسُولٍ إِلَّا بِلِسَانِ قَوْمِهِ لِيُبَيِّنَ لَهُمْ ۖ فَيُضِلُّ اللَّـهُ مَن يَشَاءُ وَيَهْدِي مَن يَشَاءُ ۚ وَهُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ ﴿٤﴾
4. Na Hatukutuma Rasuli yeyote
isipokuwa kwa lugha ya kaumu yake ili awabainishie (ujumbe). Basi Allaah
Humpotoa Amtakaye na Humuongoza Amtakaye. Naye ni Al-‘Aziyzul-Hakiym (Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika - Mwenye hikmah wa yote).
وَلَقَدْ
أَرْسَلْنَا مُوسَىٰ بِآيَاتِنَا أَنْ أَخْرِجْ قَوْمَكَ مِنَ
الظُّلُمَاتِ إِلَى النُّورِ وَذَكِّرْهُم بِأَيَّامِ اللَّـهِ ۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّكُلِّ صَبَّارٍ شَكُورٍ﴿٥﴾
5. Na kwa yakini Tulimpeleka Muwsaa kwa Aayaat
(miujiza) Zetu nyingi (Tukimwambia): “Itoe kaumu yako katika viza
kwenda katika nuru, na wakumbushe Siku za Allaah. Hakika katika hayo
kuna Aayaat (ishara, zingatio, mafunzo, mawaidha n.k) kwa kila mwingi wa kusuburi na kushukuru.
وَإِذْ
قَالَ مُوسَىٰ لِقَوْمِهِ اذْكُرُوا نِعْمَةَ اللَّـهِ عَلَيْكُمْ إِذْ
أَنجَاكُم مِّنْ آلِ فِرْعَوْنَ يَسُومُونَكُمْ سُوءَ الْعَذَابِ
وَيُذَبِّحُونَ أَبْنَاءَكُمْ وَيَسْتَحْيُونَ نِسَاءَكُمْ ۚ وَفِي ذَٰلِكُم بَلَاءٌ مِّن رَّبِّكُمْ عَظِيمٌ ﴿٦﴾
6. Na (kumbukeni pale) Muwsaa
alipoiambia kaumu yake yake: “Kumbukeni neema ya Allaah juu yenu, (pale)
Alipokuokoeni kutokana na watu wa Fir’awn, walipokusibuni adhabu mbaya
wakiwachinja watoto wenu (wachanga wa kiume), na wakiacha hai wanawake
wenu, na katika hayo kwenu ulikuwa ni mtihani mkuu kutoka kwa Rabb (Mola) wenu.
وَإِذْ تَأَذَّنَ رَبُّكُمْ لَئِن شَكَرْتُمْ لَأَزِيدَنَّكُمْ ۖ وَلَئِن كَفَرْتُمْ إِنَّ عَذَابِي لَشَدِيدٌ﴿٧﴾
7. Na (kumbukeni) Alipotangaza Rabb (Mola) wenu (kwamba) “Mkishukuru, bila shaka Nitakuzidishieni (neema Zangu); na mkikufuru, basi hakika adhabu Yangu ni kali.
وَقَالَ مُوسَىٰ إِن تَكْفُرُوا أَنتُمْ وَمَن فِي الْأَرْضِ جَمِيعًا فَإِنَّ اللَّـهَ لَغَنِيٌّ حَمِيدٌ ﴿٨﴾
8. Na Muwsaa alisema: “Mkikufuru nyinyi na wote walioko ardhini, basi hakika Allaah ni Ghaniyyun-Hamiyd (Mkwasi - Mwenye kustahiki kuhimidiwa kwa yote).
أَلَمْ يَأْتِكُمْ نَبَأُ الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ قَوْمِ نُوحٍ وَعَادٍ وَثَمُودَ ۛ وَالَّذِينَ مِن بَعْدِهِمْ ۛ لَا يَعْلَمُهُمْ إِلَّا اللَّـهُ ۚ
جَاءَتْهُمْ رُسُلُهُم بِالْبَيِّنَاتِ فَرَدُّوا أَيْدِيَهُمْ فِي
أَفْوَاهِهِمْ وَقَالُوا إِنَّا كَفَرْنَا بِمَا أُرْسِلْتُم بِهِ وَإِنَّا
لَفِي شَكٍّ مِّمَّا تَدْعُونَنَا إِلَيْهِ مُرِيبٍ ﴿٩﴾
9. Je, haijakufikieni habari ya wale
wa kabla yenu; watu wa Nuwh, na ‘Aad na Thamuwd, na wale wa baada yao.
Hakuna Awajuao isipokuwa Allaah. Waliwajia Rasuli wao kwa hoja bayana.
Wakarudisha mikono yao katika midomo yao (kuitafuna kwa hamaki), na
wakasema: “Hakika sisi tumeyakanusha yale mliyotumwa nayo, na hakika
sisi tumo katika shaka kutokana na mnayotuitia kwayo na tunayashuku.
قَالَتْ رُسُلُهُمْ أَفِي اللَّـهِ شَكٌّ فَاطِرِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ يَدْعُوكُمْ لِيَغْفِرَ لَكُم مِّن ذُنُوبِكُمْ وَيُؤَخِّرَكُمْ إِلَىٰ أَجَلٍ مُّسَمًّى ۚ
قَالُوا إِنْ أَنتُمْ إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُنَا تُرِيدُونَ أَن
تَصُدُّونَا عَمَّا كَانَ يَعْبُدُ آبَاؤُنَا فَأْتُونَا بِسُلْطَانٍ
مُّبِينٍ ﴿١٠﴾
10. Rasuli wao wakasema: “Je, kuna
shaka kuhusiana na Allaah, Muanzilishi wa mbingu na ardhi. Anakuiteni
(katika iymaan) ili Akughufurieni madhambi yenu na Akuakhirisheni mpaka
muda maalumu uliokadiriwa?” (Makafiri) wakasema: “Nyinyi si chochote
isipokuwa ni watu kama sisi, mnataka kutuzuia na yale waliyokuwa
wakiabudu baba zetu. Basi tuleteeni hoja bayana.
قَالَتْ لَهُمْ رُسُلُهُمْ إِن نَّحْنُ إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُكُمْ وَلَـٰكِنَّ اللَّـهَ يَمُنُّ عَلَىٰ مَن يَشَاءُ مِنْ عِبَادِهِ ۖ وَمَا كَانَ لَنَا أَن نَّأْتِيَكُم بِسُلْطَانٍ إِلَّا بِإِذْنِ اللَّـهِ ۚ وَعَلَى اللَّـهِ فَلْيَتَوَكَّلِ الْمُؤْمِنُونَ ﴿١١﴾
11. Rasuli wao wakawajibu: “Sisi si
chochote isipokuwa ni watu kama nyinyi, lakini Allaah Anamfadhilisha
Amtakaye miongoni mwa waja Wake. Na haikutupasa sisi kukujieni kwa hoja
(mnazotaka) isipokuwa kwa idhini ya Allaah. Na kwa Allaah (Pekee)
watawakali Waumini.
وَمَا لَنَا أَلَّا نَتَوَكَّلَ عَلَى اللَّـهِ وَقَدْ هَدَانَا سُبُلَنَا ۚ وَلَنَصْبِرَنَّ عَلَىٰ مَا آذَيْتُمُونَا ۚ وَعَلَى اللَّـهِ فَلْيَتَوَكَّلِ الْمُتَوَكِّلُونَ ﴿١٢﴾
12. “Na tuna nini (sisi) hata
tusitawakali kwa Allaah na hali Amekwishatuongoza njia yetu? Na bila
shaka tutasubiri kwa yale munayotuudhi nayo. Na kwa Allaah (Pekee)
watawakali wanaotawakali.”
وَقَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا لِرُسُلِهِمْ لَنُخْرِجَنَّكُم مِّنْ أَرْضِنَا أَوْ لَتَعُودُنَّ فِي مِلَّتِنَا ۖ فَأَوْحَىٰ إِلَيْهِمْ رَبُّهُمْ لَنُهْلِكَنَّ الظَّالِمِينَ ﴿١٣﴾
13. Na wale waliokufuru wakawaambia Rasuli wao: “Bila shaka tutakutoeni katika ardhi (nchi) yetu, au mtarudi katika millah (dini) zetu.” Basi Rabb (Mola) wao Akawafunulia Wahy kwamba: “Bila shaka Tutawahiliki madhalimu.”
وَلَنُسْكِنَنَّكُمُ الْأَرْضَ مِن بَعْدِهِمْ ۚ ذَٰلِكَ لِمَنْ خَافَ مَقَامِي وَخَافَ وَعِيدِ ﴿١٤﴾
14. “Na bila shaka Tutakukalisheni
katika ardhi baada yao. Haya ni kwa yule anayekhofu kusimamishwa mbele
Yangu na akakhofu maonyo Yangu.”
وَاسْتَفْتَحُوا وَخَابَ كُلُّ جَبَّارٍ عَنِيدٍ﴿١٥﴾
15. Na (Rasuli) wakaomba ushindi (kwa Allaah), na akapita patupu kila jabari mkaidi.
مِّن وَرَائِهِ جَهَنَّمُ وَيُسْقَىٰ مِن مَّاءٍ صَدِيدٍ ﴿١٦﴾
16. Nyuma yake (huyo jabari mkaidi, muasi) kuna (Moto wa) Jahannam, na atanyweshwa (humo) maji ya usaha.
يَتَجَرَّعُهُ وَلَا يَكَادُ يُسِيغُهُ وَيَأْتِيهِ الْمَوْتُ مِن كُلِّ مَكَانٍ وَمَا هُوَ بِمَيِّتٍ ۖ وَمِن وَرَائِهِ عَذَابٌ غَلِيظٌ ﴿١٧﴾
17. Atayagugumia kwa tabu na wala
hatakaribia (kuweza) kuyameza, na yatamjia mauti kutoka kila upande,
naye wala hafi. Na (juu ya hivyo), nyuma yake kuna adhabu nzito.
مَّثَلُ الَّذِينَ كَفَرُوا بِرَبِّهِمْ ۖ أَعْمَالُهُمْ كَرَمَادٍ اشْتَدَّتْ بِهِ الرِّيحُ فِي يَوْمٍ عَاصِفٍ ۖ لَّا يَقْدِرُونَ مِمَّا كَسَبُوا عَلَىٰ شَيْءٍ ۚ ذَٰلِكَ هُوَ الضَّلَالُ الْبَعِيدُ ﴿١٨﴾
18. Mfano wa wale waliomkufuru Rabb
(Mola) wao, ‘amali zao ni kama jivu linalopeperushwa kwa nguvu za upepo
siku ya dhoruba. Hawatoweza kupata chochote katika yale waliyoyachuma.
Huo ndio upotofu wa mbali.
أَلَمْ تَرَ أَنَّ اللَّـهَ خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ بِالْحَقِّ ۚ إِن يَشَأْ يُذْهِبْكُمْ وَيَأْتِ بِخَلْقٍ جَدِيدٍ ﴿١٩﴾
19. Je, huoni kwamba Allaah Ameumba
mbingu na ardhi kwa haki. Akitaka Atakuondosheleeni mbali na na Alete
viumbe vipya (badala yenu).
وَمَا ذَٰلِكَ عَلَى اللَّـهِ بِعَزِيزٍ ﴿٢٠﴾
20. Na hivyo kwa Allaah si kugumu.
وَبَرَزُوا
لِلَّـهِ جَمِيعًا فَقَالَ الضُّعَفَاءُ لِلَّذِينَ اسْتَكْبَرُوا إِنَّا
كُنَّا لَكُمْ تَبَعًا فَهَلْ أَنتُم مُّغْنُونَ عَنَّا مِنْ عَذَابِ
اللَّـهِ مِن شَيْءٍ ۚ قَالُوا لَوْ هَدَانَا اللَّـهُ لَهَدَيْنَاكُمْ ۖ سَوَاءٌ عَلَيْنَا أَجَزِعْنَا أَمْ صَبَرْنَا مَا لَنَا مِن مَّحِيصٍ ﴿٢١﴾
21. Na watahudhuria wote mbele ya
Allaah, wanyonge watasema (kuwaambia) wale waliotakabari: “Hakika sisi
tulikuwa wafuasi wenu (tukikutiini). Basi je, nyinyi (leo) mtaweza
kutusaidia (kutuondolea) kitu chochote katika adhabu ya Allaah?”
(Waliotakabari) Watasema: “Kama Allaah Angetuongoa, bila shaka
tungelikuongozeni. (Lakini) Ni sawasawa kwetu; tukipapatika au
tukisubiri, hatuna mahali pa kukimbilia.”
وَقَالَ الشَّيْطَانُ لَمَّا قُضِيَ الْأَمْرُ إِنَّ اللَّـهَ وَعَدَكُمْ وَعْدَ الْحَقِّ وَوَعَدتُّكُمْ فَأَخْلَفْتُكُمْ ۖ وَمَا كَانَ لِيَ عَلَيْكُم مِّن سُلْطَانٍ إِلَّا أَن دَعَوْتُكُمْ فَاسْتَجَبْتُمْ لِي ۖ فَلَا تَلُومُونِي وَلُومُوا أَنفُسَكُم ۖ مَّا أَنَا بِمُصْرِخِكُمْ وَمَا أَنتُم بِمُصْرِخِيَّ ۖ إِنِّي كَفَرْتُ بِمَا أَشْرَكْتُمُونِ مِن قَبْلُ ۗ إِنَّ الظَّالِمِينَ لَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ ﴿٢٢﴾
22. Na shaytwaan atasema
itakapohukumiwa amri: (ya kuingia Jannah au Motoni) “Hakika Allaah
Alikuahidini ahadi ya haki (na leo Ameitimiza); nami nilikuahidini
lakini sikukutimizieni (nikakusalitini). Na sikuwa na mamlaka juu yenu
isipokuwa nilikuiteni mkaniitikia. Basi msinilaumu, bali laumuni nafsi
zenu. Mimi siwezi kukusaidieni (shida ya adhabu) wala nyinyi hamuwezi
kunisaidia. Hakika mimi nilikanusha kwa yale mliyonishirikisha zamani.
Hakika madhalimu watapa adhabu iumizayo.”
وَأُدْخِلَ
الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن
تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا بِإِذْنِ رَبِّهِمْ ۖ تَحِيَّتُهُمْ فِيهَا سَلَامٌ ﴿٢٣﴾
23. Na wataingizwa wale walioamini na wakatenda mema, Jannaat zipitazo chini yake mito, ni wenye kudumu humo kwa idhini ya Rabb (Mola) wao. Maamkizi yao humo yatakuwa ni ‘Salaam’.
أَلَمْ تَرَ كَيْفَ ضَرَبَ اللَّـهُ مَثَلًا كَلِمَةً طَيِّبَةً كَشَجَرَةٍ طَيِّبَةٍ أَصْلُهَا ثَابِتٌ وَفَرْعُهَا فِي السَّمَاءِ ﴿٢٤﴾
24. Je, huoni vipi Allaah Amepiga mfano wa neno twayyibah (zuri) kama mti mzuri mizizi yake imethibitika imara na matawi yake (yanafikia) mbinguni?
تُؤْتِي أُكُلَهَا كُلَّ حِينٍ بِإِذْنِ رَبِّهَا ۗ وَيَضْرِبُ اللَّـهُ الْأَمْثَالَ لِلنَّاسِ لَعَلَّهُمْ يَتَذَكَّرُونَ ﴿٢٥﴾
25. Unatoa mazao yake kila wakati kwa idhini ya Rabb (Mola) wake. Na Allaah Anapiga mifano kwa watu ili wapate kukumbuka (na kuzingatia).
وَمَثَلُ كَلِمَةٍ خَبِيثَةٍ كَشَجَرَةٍ خَبِيثَةٍ اجْتُثَّتْ مِن فَوْقِ الْأَرْضِ مَا لَهَا مِن قَرَارٍ ﴿٢٦﴾
26. Na mfano wa neno baya ni kama mti mbaya uliong’olewa juu ya ardhi hauna imara.
يُثَبِّتُ اللَّـهُ الَّذِينَ آمَنُوا بِالْقَوْلِ الثَّابِتِ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَفِي الْآخِرَةِ ۖ وَيُضِلُّ اللَّـهُ الظَّالِمِينَ ۚ وَيَفْعَلُ اللَّـهُ مَا يَشَاءُ﴿٢٧﴾
27. Allaah Huwathibitisha wale
walioamini kwa kauli thabiti katika uhai wa dunia na Aakhirah. Na Allaah
Huwaacha kupotoka madhalimu. Na Allaah Anafanya Atakavyo.
أَلَمْ تَرَ إِلَى الَّذِينَ بَدَّلُوا نِعْمَتَ اللَّـهِ كُفْرًا وَأَحَلُّوا قَوْمَهُمْ دَارَ الْبَوَارِ﴿٢٨﴾
28. Je, huoni wale waliobadilisha neema ya Allaah kwa kufuru, na wakawafikisha watu wao nyumba ya mateketezi?
جَهَنَّمَ يَصْلَوْنَهَا ۖ وَبِئْسَ الْقَرَارُ ﴿٢٩﴾
29. (Moto wa) Jahannam watauingia na kuungua, na ubaya ulioje mahala pa makazi.
وَجَعَلُوا لِلَّـهِ أَندَادًا لِّيُضِلُّوا عَن سَبِيلِهِ ۗ قُلْ تَمَتَّعُوا فَإِنَّ مَصِيرَكُمْ إِلَى النَّارِ ﴿٣٠﴾
30. Na wakamfanyia Allaah walinganishi
ili wapoteze (watu) na njia Yake. Sema: “Stareheni! (Na uhai mfupi wa
duniani); kwani hakika mahali penu pa kuishia ni Motoni”.
قُل
لِّعِبَادِيَ الَّذِينَ آمَنُوا يُقِيمُوا الصَّلَاةَ وَيُنفِقُوا مِمَّا
رَزَقْنَاهُمْ سِرًّا وَعَلَانِيَةً مِّن قَبْلِ أَن يَأْتِيَ يَوْمٌ لَّا
بَيْعٌ فِيهِ وَلَا خِلَالٌ ﴿٣١﴾
31. Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم kuwaambia)
waja Wangu ambao wameamini: Wasimamishe Swalaah na watoe katika yale
Tuliyowaruzuku kwa siri na (kwa) dhahiri kabla haijafika Siku (ambayo)
hakutakuweko biashara na wala rafiki wa kweli.
اللَّـهُ
الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَأَنزَلَ مِنَ السَّمَاءِ
مَاءً فَأَخْرَجَ بِهِ مِنَ الثَّمَرَاتِ رِزْقًا لَّكُمْ ۖ وَسَخَّرَ لَكُمُ الْفُلْكَ لِتَجْرِيَ فِي الْبَحْرِ بِأَمْرِهِ ۖ وَسَخَّرَ لَكُمُ الْأَنْهَارَ﴿٣٢﴾
32. Allaah Ambaye Ameumba mbingu na
ardhi, na Akateremsha maji (mvua) kutoka mbinguni, Akataoa kwayo (kila
aina ya) mazao kuwa ni riziki kwenu. Na Akakutiishieni majahazi ili
zipitie baharini kwa amri Yake. Na Akakutiishieni mito (pia).
وَسَخَّرَ لَكُمُ الشَّمْسَ وَالْقَمَرَ دَائِبَيْنِ ۖ وَسَخَّرَ لَكُمُ اللَّيْلَ وَالنَّهَارَ ﴿٣٣﴾
33. Na Akakutiishieni jua na mwezi daima dawamu na Akakuitishieni usiku na mchana.
وَآتَاكُم مِّن كُلِّ مَا سَأَلْتُمُوهُ ۚ وَإِن تَعُدُّوا نِعْمَتَ اللَّـهِ لَا تُحْصُوهَا ۗ إِنَّ الْإِنسَانَ لَظَلُومٌ كَفَّارٌ ﴿٣٤﴾
34. Na Akakupeni kila mnachomuomba. Na
mkihesabu neema za Allaah hamtoweza kuzihesabu (zote). Hakika insani ni
dhalimu mkubwa mwenye kukufuru sana (neema).
وَإِذْ قَالَ إِبْرَاهِيمُ رَبِّ اجْعَلْ هَـٰذَا الْبَلَدَ آمِنًا وَاجْنُبْنِي وَبَنِيَّ أَن نَّعْبُدَ الْأَصْنَامَ ﴿٣٥﴾
35. Na (taja ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم pale) Ibraahiym aliposema: “Ee Rabb (Mola) wangu! Ujaalie mji huu (Makkah) uwe wa amani; na Uniepushe na wanangu kuabudu masanamu.
رَبِّ إِنَّهُنَّ أَضْلَلْنَ كَثِيرًا مِّنَ النَّاسِ ۖ فَمَن تَبِعَنِي فَإِنَّهُ مِنِّي ۖ وَمَنْ عَصَانِي فَإِنَّكَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿٣٦﴾
36. “Rabb (Mola) wangu!
Hakika hao (masanamu) wamepoteza wengi sana katika watu. Basi
atakayenifuata, huyo ni katika mimi, na atakayeniasi, basi hakika Wewe
ni Ghafuwrur-Rahiym (Mwingi wa kughufuria - Mwenye kurehemu).
رَّبَّنَا
إِنِّي أَسْكَنتُ مِن ذُرِّيَّتِي بِوَادٍ غَيْرِ ذِي زَرْعٍ عِندَ
بَيْتِكَ الْمُحَرَّمِ رَبَّنَا لِيُقِيمُوا الصَّلَاةَ فَاجْعَلْ
أَفْئِدَةً مِّنَ النَّاسِ تَهْوِي إِلَيْهِمْ وَارْزُقْهُم مِّنَ
الثَّمَرَاتِ لَعَلَّهُمْ يَشْكُرُونَ ﴿٣٧﴾
37. “Rabb wetu! Hakika mimi nimewaweka
baadhi ya dhuria wangu katika bonde (la Makkah) lisilokuwa na mmea
wowote, kwenye Nyumba Yako Tukufu. Rabb wetu, ili wasimamishe Swalaah na
Ujaalie nyoyo za watu zielekee kwao na Uwaruzuku mazao ili wapate
kushukuru.
رَبَّنَا إِنَّكَ تَعْلَمُ مَا نُخْفِي وَمَا نُعْلِنُ ۗ وَمَا يَخْفَىٰ عَلَى اللَّـهِ مِن شَيْءٍ فِي الْأَرْضِ وَلَا فِي السَّمَاءِ ﴿٣٨﴾
38. “Rabb (Mola) wetu! Hakika
Wewe Unajua tunayoyaficha na tunayoyadhihirisha. Na hakifichiki kitu
chochote kwa Allaah katika ardhi wala katika mbingu.
الْحَمْدُ لِلَّـهِ الَّذِي وَهَبَ لِي عَلَى الْكِبَرِ إِسْمَاعِيلَ وَإِسْحَاقَ ۚ إِنَّ رَبِّي لَسَمِيعُ الدُّعَاءِ ﴿٣٩﴾
39. “AlhamduliLLaahi (Himidi zote
Anastahiki Allaah) Ambaye Amenitunukia juu ya umri mkubwa wangu (watoto
wawili) Ismaa’iyl na Is-haaq. Hakika Rabb (Mola) wangu bila shaka ni Samiy’u (Mwenye kusikia) du’aa yangu.
رَبِّ اجْعَلْنِي مُقِيمَ الصَّلَاةِ وَمِن ذُرِّيَّتِي ۚ رَبَّنَا وَتَقَبَّلْ دُعَاءِ﴿٤٠﴾
40. “Rabb (Mola) wangu! Nijaalie niwe mwenye kusimamisha Swalaah na dhuria wangu. Rabb wetu! Nitakabalie du’aa yangu.
رَبَّنَا اغْفِرْ لِي وَلِوَالِدَيَّ وَلِلْمُؤْمِنِينَ يَوْمَ يَقُومُ الْحِسَابُ ﴿٤١﴾
41. “Rabb (Mola) wetu! Nighufurie na wazazi wangu wawili na Waumini Siku itakayosimama hesabu.”
وَلَا تَحْسَبَنَّ اللَّـهَ غَافِلًا عَمَّا يَعْمَلُ الظَّالِمُونَ ۚ إِنَّمَا يُؤَخِّرُهُمْ لِيَوْمٍ تَشْخَصُ فِيهِ الْأَبْصَارُ ﴿٤٢﴾
42. Na wala usidhanie kwamba Allaah
Ameghafilika na yale wanayoyatenda madhalimu. Hakika Anawaakhirisha kwa
ajili ya Siku ambayo macho (yao) yatadokoka (kwa kiwewe kubwa).
مُهْطِعِينَ مُقْنِعِي رُءُوسِهِمْ لَا يَرْتَدُّ إِلَيْهِمْ طَرْفُهُمْ ۖ وَأَفْئِدَتُهُمْ هَوَاءٌ ﴿٤٣﴾
43. (Watakuwa) Wenye kukimbia mbio vichwa vyao juu, macho yao hayapepesi; na nyoyo zao ni tupu (kwa kiwewe).
وَأَنذِرِ
النَّاسَ يَوْمَ يَأْتِيهِمُ الْعَذَابُ فَيَقُولُ الَّذِينَ ظَلَمُوا
رَبَّنَا أَخِّرْنَا إِلَىٰ أَجَلٍ قَرِيبٍ نُّجِبْ دَعْوَتَكَ وَنَتَّبِعِ
الرُّسُلَ ۗ أَوَلَمْ تَكُونُوا أَقْسَمْتُم مِّن قَبْلُ مَا لَكُم مِّن زَوَالٍ﴿٤٤﴾
44. Na waonye watu Siku itakayowafikia adhabu; wale waliodhulumu watasema: “Rabb
(Mola) wetu! Tuakhirishe mpaka muda mdogo (tu) ili tuitikie wito Wako,
na tuwafuate Rasuli.” (Wataambiwa): “Je, kwani hamkuwa mmeapa kabla
kwamba hamtokuwa na mhamo wowote (wa dunia na kuelekea Aakhirah?).”
وَسَكَنتُمْ
فِي مَسَاكِنِ الَّذِينَ ظَلَمُوا أَنفُسَهُمْ وَتَبَيَّنَ لَكُمْ كَيْفَ
فَعَلْنَا بِهِمْ وَضَرَبْنَا لَكُمُ الْأَمْثَالَ ﴿٤٥﴾
45. “Na mkakaa katika maskani ya wale
waliodhulumu nafsi zao na ikakubainikieni vipi Tulivyowafanya, na
Tukakupigieni mifano mingi?”
وَقَدْ مَكَرُوا مَكْرَهُمْ وَعِندَ اللَّـهِ مَكْرُهُمْ وَإِن كَانَ مَكْرُهُمْ لِتَزُولَ مِنْهُ الْجِبَالُ﴿٤٦﴾
46. Na kwa yakini wakafanya mipango ya
njama zao, na kwa Allaah kuna (rekodi ya) njama zao, na japokuwa njama
zao haziwezi kuondosha majabali.
فَلَا تَحْسَبَنَّ اللَّـهَ مُخْلِفَ وَعْدِهِ رُسُلَهُ ۗ إِنَّ اللَّـهَ عَزِيزٌ ذُو انتِقَامٍ ﴿٤٧﴾
47. Basi usidhanie kwamba Allaah (ni) Mwenye kukhalifu ahadi Yake (kwa) Rasuli Wake. Hakika Allaah ni ‘Aziyz (Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika), Mwenye kulipiza.
يَوْمَ تُبَدَّلُ الْأَرْضُ غَيْرَ الْأَرْضِ وَالسَّمَاوَاتُ ۖ وَبَرَزُوا لِلَّـهِ الْوَاحِدِ الْقَهَّارِ﴿٤٨﴾
48. Siku ardhi itakapobadilishwa kuwa ardhi nyingine na mbingu (pia ziwe nyingine) na (viumbe wote) watahudhuria kwa Allaah Al-Waahidil-Qahhaar (Mmoja Pekee - Mwenye kudhibiti na kudhalilisha, Mshindi, Asiyepingika).”
وَتَرَى الْمُجْرِمِينَ يَوْمَئِذٍ مُّقَرَّنِينَ فِي الْأَصْفَادِ ﴿٤٩﴾
49. Na utawaona wahalifu Siku hiyo wamezungurushwa katika minyororo.
سَرَابِيلُهُم مِّن قَطِرَانٍ وَتَغْشَىٰ وُجُوهَهُمُ النَّارُ﴿٥٠﴾
50. Mavazi yao ya chuma ni ya lami, na Moto utafunika nyuso zao.
لِيَجْزِيَ اللَّـهُ كُلَّ نَفْسٍ مَّا كَسَبَتْ ۚ إِنَّ اللَّـهَ سَرِيعُ الْحِسَابِ ﴿٥١﴾
51. Ili Allaah Alipe kila nafsi yale iliyoyachuma. Hakika Allaah ni Mwepesi wa kuhesabu.
هَـٰذَا بَلَاغٌ لِّلنَّاسِ وَلِيُنذَرُوا بِهِ وَلِيَعْلَمُوا أَنَّمَا هُوَ إِلَـٰهٌ وَاحِدٌ وَلِيَذَّكَّرَ أُولُو الْأَلْبَابِ﴿٥٢﴾
52. Hii (Qur’aan) ni ubalighisho (wa ujumbe) kwa watu, na ili wawaonye kwayo, na ili wapate kujua kwamba hakika Yeye ni Ilaah (Muabudiwa wa haki) Mmoja (Pekee) na ili wakumbuke (na wawaidhike) wenye akili.
Ukitaka kusoma Sura nyengine Rejeauliko toka
Ukiwa una shauri au maelezo juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii falhaqqiy@gmail.com
Ukiwa una shauri au maelezo juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii falhaqqiy@gmail.com