Fadhila za Mwenye Kutafuta Elimu


Hapa tutasita katika mlango wa elimu kabla ya kauli na amali katika kitabu cha sahihi Bukhari.
Imam Bukhari ameuita mlango huu kuwa ni elimu kabla ya kauli na amali – vitendo. Muislamu hutakiwa kwanza ajifunze kabla ya kutenda au kusema jambo lolote linalohusu dini yetu na tutachukua baadhi ya aya na hadithi zinazoonesha umuhimu huu.
Anasema Allah Subhaanahu Wata’ala katika Qur’aan Al Mujaadalah /11
يَرْفَعِ اللَّهُ الَّذِينَ آمَنُوا مِنكُمْ وَالَّذِينَ أُوتُوا الْعِلْمَ دَرَجَاتٍ وَاللَّهُ بِمَا تَعْمَلُونَ خَبِيرٌ
Allah atawainua walioamini miongoni mwenu, na walio pewa elimu daraja za juu. Na Allah anazo khabari za mnayoyatenda
Na anasema katika Suuraatu Muhammad/19
                                                         فَاعْلَمْ أَنَّهُ لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ
Basi jua ya kwamba hapana Mungu ila Allah
وأن العلماء هم ورثة الأنبياء، ورثوا العلم، من أخذه أخذه بحظ وافر، ومن سلك                      
                                   يطلب به علما سهل الله له طريقا إلى الجنة    

 
 
Hakika Maulamaa ni warithi wa Mitume kwani wamerithi elimu na mwenye kuichukua basi ameichukua akiwa na bahati nzuri . Na atakaenyoosha njia kutafuta ndani yake elimu basi Allah humuwepesishia njia ya kwenda peponi.
Katika Suuratu Faatir/28
                                  إِنَّمَا يَخْشَى اللَّهَ مِنْ عِبَادِهِ الْعُلَمَاء    
Kwa hakika wanao mcha Allah miongoni mwa waja wake ni Wanazuoni - Maulamaa
Al Ankaboot /43
                                       وَمَا يَعْقِلُهَا إِلَّا الْعَالِمُونَ
   Na hawaifahamu ila wenye elimu
Al Mulk/10
                       وَقَالُوا لَوْ كُنَّا نَسْمَعُ أَوْ نَعْقِلُ مَا كُنَّا فِي أَصْحَابِ السَّعِيرِ
Na watasema: Lau kuwa tungelisikia, au tungelikuwa na akili, tusingelikuwa katika watu wa Motoni!
Azzumar/9
                      قُلْ هَلْ يَسْتَوِي الَّذِينَ يَعْلَمُونَ وَالَّذِينَ لَا يَعْلَمُونَ
Sema: Ati watakuwa sawa wale wanao jua na wale wasio jua?
           
   وقال النبي صلى الله عليه وسلم: (من يرد الله به خيرا يفقهه في الدين) 
 
Mwenye kutakiwa kheri na Allah basi humpa maarifa na upeo katika dini.
                                   
                          و(إنما العلم بالتعلم).
    Hakika ya elimu ni kwa kujifundisha
Mwisho wa kunukuu kutoka kitabu cha sahihi Bukhari.
Pia Anasema Mtume Salla Allahu ‘Alayhi Wasallam katika hadithi maarufu kwamba :
: ( طَلَبُ الْعِلْمِ فَرِيضَةٌ عَلَى كُلِّ مُسْلِمٍ )  وصححه الألباني في صحيح سنن ابن ماجة 
         
 “Kutafuta elimu ni wajibu kwa kila muislamu.”
Ameisahihisha Sh Albani katika Sahihi za sunnan Ibnu Majah
Kutafuta elimu ni ibada. Allah Subhaanahu Wata’ala anaabudiwa pia kwa kutafuta elimu. Na hizi tulizozitaja ni fadhila chache tu za mwenye kufanya hima katika kutafuta elimu.
Tumuombe Allah Subhaanahu Wata’ala atujaalie miongoni mwa wanaoitafuta elimu ya dini yetu tuweze kuijua na kuifahamu kama walivyoifahamu waliokuwa kabla yetu. Tumuombe Allah Subhaanahu Wata’ala atupe hima na hamu ya kusoma na kuifahamu vyema elimu ya dini yetu.
Amin!.