018 - Hadiyth Ya 18: Alama Za Mnafiki Ni Tatu: Uongo, Kutokutimiza Ahadi, Kufanya Khiyana
عَنْ
أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ (صلى الله عليه و آله
وسلم): ((آيَةُ الْمُنَافِقِ ثلاَثٌ إِذَا حَدَّثَ كَذَبَ وَإِذَا وَعَدَ
أَخْلَفَ وَإِذَا اؤْتُمِنَ خَانَ)) متفق عليه . وفي رواية: ((وَإِنْ صَامَ
وَصَلَّى وَزَعَمَ أَنَّهُ مُسْلِمٌ)) متفق عليه
Imepokelewa kutoka kwa Abu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Alama za mnafiki ni tatu: anapozungumza husema uongo, anapotoa ahadi hukhalifu (hatimizi), na anapoaminiwa hufanya khiyana))[1]. Na katika riwaaya nyingine: ((Hata akifunga na akiswali na akidai kuwa yeye ni Muislamu))[2]
Mafunzo Na Hidaaya:
- Unafiki ni miongoni mwa maradhi ya moyo ya hatari yanayokemewa sana katika Uislamu. [Al-Maaidah 5: 52, Al-Anfaal 8: 49, Al-Hajj 22: 53].
- Sifa tatu hizo ni sifa mashuhuri miongoni mwa sifa za wanafiki. [An-Nisaa 4: 143, Al-Baqarah 2: 8-15] Lakini hizo sio zote zinazowahusu, bali wanazo sifa mbaya zaidi ya hizo.
- Mwenye kuwa na sifa zote tatu hizo ajitambue kuwa ni mnafiki.
- Kukimbilia kujirekebisha pindi Muislamu anapotambua kuwa ana sifa mojawapo kabla ya kumiliki sifa zote tatu.
- Uislamu unafunza sifa njema za ukweli, kutimiza ahadi na uaminifu. [An-Nisaa 4: 58, An-Nahl 16: 91]. Nazo ni miongoni mwa sifa za watakaopata Pepo ya Al-Firdaws [Al-Muuminuwn 23: 8]. Na pia:
وَالَّذِينَ هُمْ لِأَمَانَاتِهِمْ وَعَهْدِهِمْ رَاعُونَ
Na ambao amana zao na ahadi zao wanazichunga (kuzitimiza)[3]
- Mtu anaweza kudhaniya kuwa ni Muislamu wa kweli kwa sababu ya utekelezaji wake wa ‘Ibaadah, kumbe ni mnafiki.