020 - Hadiyth Ya 20: Waumini Ni Kama Jengo Hutiliana Nguvu


عَنْ أَبِي مُوسَى (رضي الله عنه) قال: قال رَسُولُ الله (صلى الله عليه و آله وسلم): ((الْمُؤْمِنَ لِلْمُؤْمِنِ كَالْبُنْيَانِ يَشُدُّ بَعْضُهُ بَعْضاً)) وَشَبَّكَ أَصَابِعَهُ - متفق عليه
Imepokelewa kutoka kwa Abu Muwsa (رضي الله عنه) kwamba Mtume wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Muumin kwa Muumin mwenziwe ni kama jengo, baadhi yake hutilia nguvu baadhi nyingine)). Akaviumanisha vidole vyake.[1]
 
Mafunzo Na Hidaaya:
 
  1. Waumini wa kweli ni wenye kuungana katika kila jambo lao.
 
وَالْمُؤْمِنُونَ وَالْمُؤْمِنَاتُ بَعْضُهُمْ أَوْلِيَاءُ بَعْضٍ ۚ
Na Waumini wanaume na Waumini wanawake ni marafiki walinzi  wao wa kwao[2]
 
  1. Waumini ni ndugu, hivyo inawapasa kutilia nguvu umoja wao. [Aal ‘Imraan 3: 200].
 
  1. Umoja unatia nguvu kama jengo linavyokuwa imara, na hakuna faida kutengana, kwani jengo halitokuwa na faida pindi linapokosa kushikana. [Asw-Swaff 61: 4].
 
  1. Umoja unasababisha mapenzi baina ya Waislamu na kupendeleana kheri za kila aina. [Rejea Hadiyth namba 21, 22, 80].
 
  1. Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) ni mwalimu bora kabisa kwa kutoa mifano mizuri ya hikma na busara katika kuonyesha au kuelezea jambo. [Al-Ahzaab 33: 21].
 
  1. Ni mbinu nzuri ya Da‘wah au ufundishaji kwa Daa‘iyyah au mwalimu kwa kuonyesha kitu kwa vitendo. Na kufanya hivyo kunamfanya msikilizaji kuelewa na kufahamu zaidi.



[1]  Al-Bukhaariy na Muslim.
[2]  At-Tawbah (9: 71).