Al-Kawthar (108)

سُورَةُ  الْكَوْثَر
Al-Kawthar (108)

(Imeteremka Makka)

Mwenyezi Mungu katika Sura hii anamtajia Mtume wake s.a.w. neema alizo mfanyia kwa kumpa kheri nyingi na neema kubwa kubwa katika dunia na Akhera, na akamtaka adumishe Sala iliyo safi kwa kumridhi Mwenyezi Mungu, na atoe mhanga bora ya mali yake kwa dhahiya ya shukrani kwa ukarimu alio pewa. Kisha Sura imekhitimisha kwa kumbashiria Nabii s.a.w. kuwa atakatiliwa mbali huyo anaye mchukia na kumbughudhi Mtume.

بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ

إِنَّا أَعْطَيْنَاكَ الْكَوْثَرَ ﴿١﴾

1. Hakika Sisi Tumekupa (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) Al-Kawthar (mto katika Jannah).

فَصَلِّ لِرَبِّكَ وَانْحَرْ ﴿٢﴾

2. Basi swali kwa ajili ya Rabb (Mola) wako na chinja (kwa ajili Yake).

إِنَّ شَانِئَكَ هُوَ الْأَبْتَرُ ﴿٣﴾

3. Hakika (adui yako) anayekuchukia yeye ndiye atakayekatiliwa mbali (kizazi na kila kheri).





Ukitaka kusoma Sura nyengine Rejeauliko toka
Ukiwa una shauri au maelezo juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii falhaqqiy@gmail.com