الأَحْقَاف
Al-Ahqaaf: 46
(Imeteremka Makka)
Sura
hii tukufu inasimulia kuteremka kwa Qur'ani kutokana
na Mwenyezi Mungu, na kupasa kuiamini na kumuamini Muhammad s.a.w. na kuisadiki
Siku ya Kiyama. Na imekusudia kunabihisha watu wazingatie yaliyo wapata walio
tangulia walio muasi Mwenyezi Mungu na Mitume wake, na
imeita watu washughulikie kuwafanyia wema wazazi wawili, na kuzitunza haki zao.
Na hii Sura imeelezea kisa cha baadhi ya majini waliyo isikia Qur'ani tukufu,
wakaambizana waisikilize. Wakaiona kuwa inathibitisha yale
yale waliyo kuja nayo Mitume wa kabla ya Muhammad s.a.w., inaongoa kwendea Haki
na kwenye Njia Iliyo Nyooka. Wakaiamini; na wakawataka
wenzao wafuate yale yale. Ikamalizikia hadithi kwa
wito wa kumtaka Nabii s.a.w. avumilie vile anavyo kadhibishwa na kaumu yake, na
kumliwaza katika hayo kwa waliyo yastahamilia Mitume wa kabla yake wenye azma
ngumu.
بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ
حم﴿١﴾
1. Haa Miym.
تَنزِيلُ الْكِتَابِ مِنَ اللَّـهِ الْعَزِيزِ الْحَكِيمِ﴿٢﴾
2. Ni uteremsho wa Kitabu kutoka kwa Allaah Al-‘Aziyzil-Hakiym (Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika - Mwenye hikmah wa yote).
مَا خَلَقْنَا السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا إِلَّا بِالْحَقِّ وَأَجَلٍ مُّسَمًّى ۚ وَالَّذِينَ كَفَرُوا عَمَّا أُنذِرُوا مُعْرِضُونَ﴿٣﴾
3. Hatukuumba mbingu na ardhi na vilivyo baina yake isipokuwa kwa
haki na muda maalumu uliokadiriwa. Na wale waliokufuru kwa yale
wanayoonywa kwayo ni wenye kukengeuka.
قُلْ أَرَأَيْتُم مَّا تَدْعُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ أَرُونِي مَاذَا خَلَقُوا مِنَ الْأَرْضِ أَمْ لَهُمْ شِرْكٌ فِي السَّمَاوَاتِ ۖ ائْتُونِي بِكِتَابٍ مِّن قَبْلِ هَـٰذَا أَوْ أَثَارَةٍ مِّنْ عِلْمٍ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ﴿٤﴾
4. Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم):
“Je, mnaonaje wale mnaowaomba badala ya Allaah! Nionyesheni nini
wameumba katika ardhi; au wana ushirika katika (uumbaji wa) mbingu?
Nileteeni Kitabu kabla ya hiki, au alama yeyote iliobakia ya elimu mkiwa
wakweli.”
وَمَنْ
أَضَلُّ مِمَّن يَدْعُو مِن دُونِ اللَّـهِ مَن لَّا يَسْتَجِيبُ لَهُ
إِلَىٰ يَوْمِ الْقِيَامَةِ وَهُمْ عَن دُعَائِهِمْ غَافِلُونَ﴿٥﴾
5. “Na nani aliyepotoka zaidi kuliko ambaye anayeomba asiyekuwa
Allaah ambaye hamuitikii mpaka Siku ya Qiyaamah; nao kuhusu du’aa zao ni
wenye kughafilika.”
وَإِذَا حُشِرَ النَّاسُ كَانُوا لَهُمْ أَعْدَاءً وَكَانُوا بِعِبَادَتِهِمْ كَافِرِينَ﴿٦﴾
6. Na (Qiyaamah) watakapokusanywa watu (miungu ya uongo) watakuwa maadui wao, na watakuwa kwa ‘ibaadah zao ni wenye kuzikanusha.
وَإِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِمْ آيَاتُنَا بَيِّنَاتٍ قَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا لِلْحَقِّ لَمَّا جَاءَهُمْ هَـٰذَا سِحْرٌ مُّبِينٌ﴿٧﴾
7. Na wanaposomewa Aayaat Zetu bayana, husema wale waliokufuru kuhusu haki ilipowajia: “Hii ni sihiri bayana.”
أَمْ يَقُولُونَ افْتَرَاهُ ۖ قُلْ إِنِ افْتَرَيْتُهُ فَلَا تَمْلِكُونَ لِي مِنَ اللَّـهِ شَيْئًا ۖ هُوَ أَعْلَمُ بِمَا تُفِيضُونَ فِيهِ ۖ كَفَىٰ بِهِ شَهِيدًا بَيْنِي وَبَيْنَكُمْ ۖ وَهُوَ الْغَفُورُ الرَّحِيمُ﴿٨﴾
8. Je, wanasema ameitunga? Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم):
“Ikiwa nimeitunga, basi hamtomiliki kwa ajili yangu chochote (uwezo wa
kunilinda) kwa Allaah. Yeye Anajua zaidi yale mnayoyaropokwa.
Ananitosheleza kuwa Shahiydaa (Mwenye kushuhudia yote) baina yangu na baina yenu; Naye Ndiye Al-Ghafuwrur-Rahiym (Mwingi wa kughufuria - Mwenye kurehemu).
قُلْ مَا كُنتُ بِدْعًا مِّنَ الرُّسُلِ وَمَا أَدْرِي مَا يُفْعَلُ بِي وَلَا بِكُمْ ۖ إِنْ أَتَّبِعُ إِلَّا مَا يُوحَىٰ إِلَيَّ وَمَا أَنَا إِلَّا نَذِيرٌ مُّبِينٌ﴿٩﴾
9. Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم):
“Mimi sikuwa jambo jipya lilozuka miongoni mwa Rasuli na sijui
nitakavyofanyiwa mimi wala nyinyi. Sifuati isipokuwa niliyofunuliwa Wahy, nami si chochote isipokuwa ni mwonyaji bayana.”
قُلْ
أَرَأَيْتُمْ إِن كَانَ مِنْ عِندِ اللَّـهِ وَكَفَرْتُم بِهِ وَشَهِدَ
شَاهِدٌ مِّن بَنِي إِسْرَائِيلَ عَلَىٰ مِثْلِهِ فَآمَنَ
وَاسْتَكْبَرْتُمْ ۖ إِنَّ اللَّـهَ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الظَّالِمِينَ﴿١٠﴾
10. Sema: “Mnaonaje ikiwa (hii Qur-aan) ni kutoka kwa Allaah, na
mkaikanusha; na akashuhudia shahidi miongoni mwa wana wa Israaiyl juu ya
mfano wake, na akaamini nanyi mkatabari? Hakika Allaah Haongoi watu
madhalimu.”
وَقَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا لِلَّذِينَ آمَنُوا لَوْ كَانَ خَيْرًا مَّا سَبَقُونَا إِلَيْهِ ۚ وَإِذْ لَمْ يَهْتَدُوا بِهِ فَسَيَقُولُونَ هَـٰذَا إِفْكٌ قَدِيمٌ﴿١١﴾
11. Na wale waliokufuru wakasema kuwaambia walioamini: “Lau
ingelikuwa (kile walichokiamini) ni kheri, basi wasingetusabiki. Na kwa
kuwa hawakuongoka kwayo (Qur-aan), basi watasema: “Huu ni uongo wa
zamani.”
وَمِن قَبْلِهِ كِتَابُ مُوسَىٰ إِمَامًا وَرَحْمَةً ۚ وَهَـٰذَا كِتَابٌ مُّصَدِّقٌ لِّسَانًا عَرَبِيًّا لِّيُنذِرَ الَّذِينَ ظَلَمُوا وَبُشْرَىٰ لِلْمُحْسِنِينَ﴿١٢﴾
12. Na kabla yake ni kitabu cha Muwsaa (Tawraat); kiongozi na ni
Rahmah. Na hiki Kitabu kinasadikisha (vitabu vilivyokitangulia), lisani
ya Kiarabu ili kionye wale waliodhulumu na ni bishara kwa wafanyao
ihsaan.
إِنَّ الَّذِينَ قَالُوا رَبُّنَا اللَّـهُ ثُمَّ اسْتَقَامُوا فَلَا خَوْفٌ عَلَيْهِمْ وَلَا هُمْ يَحْزَنُونَ﴿١٣﴾
13. Hakika wale waliosema: “Rabb (Mola) wetu ni Allaah.” Kisha wakathibitika imara, basi hakutokuwa na khofu juu yao, na wala hawatohuzunika.
أُولَـٰئِكَ أَصْحَابُ الْجَنَّةِ خَالِدِينَ فِيهَا جَزَاءً بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ﴿١٤﴾
14. Hao ndio watu wa Jannah, ni wenye kudumu humo, jazaa kwa yale waliyokuwa wakitenda.
وَوَصَّيْنَا الْإِنسَانَ بِوَالِدَيْهِ إِحْسَانًا ۖ حَمَلَتْهُ أُمُّهُ كُرْهًا وَوَضَعَتْهُ كُرْهًا ۖ وَحَمْلُهُ وَفِصَالُهُ ثَلَاثُونَ شَهْرًا ۚ
حَتَّىٰ إِذَا بَلَغَ أَشُدَّهُ وَبَلَغَ أَرْبَعِينَ سَنَةً قَالَ رَبِّ
أَوْزِعْنِي أَنْ أَشْكُرَ نِعْمَتَكَ الَّتِي أَنْعَمْتَ عَلَيَّ وَعَلَىٰ
وَالِدَيَّ وَأَنْ أَعْمَلَ صَالِحًا تَرْضَاهُ وَأَصْلِحْ لِي فِي
ذُرِّيَّتِي ۖ إِنِّي تُبْتُ إِلَيْكَ وَإِنِّي مِنَ الْمُسْلِمِينَ﴿١٥﴾
15. Na Tumemuusia insani kuwafanyia wema wazazi wake wawili. Mama
yake amebeba mimba yake kwa tabu na akamzaa kwa tabu, na kuibeba mimba
na kuachishwa kwake kunyonya ni miezi thelathini. Mpaka anapofikia umri
wake wa kupevuka, na akafikia miaka arubaini; husema: “Rabb
(Mola) wangu! Niwezeshe nishukuru neema Yako ambayo Umenineemesha juu
yangu, na juu ya wazazi wangu wawili, na kwamba nitende ‘amali njema
Uridhike nazo na Nitengenezee katika dhuria wangu; hakika mimi nimetubu
Kwako, na hakika mimi ni miongoni mwa Waislamu.”
أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ نَتَقَبَّلُ عَنْهُمْ أَحْسَنَ مَا عَمِلُوا وَنَتَجَاوَزُ عَن سَيِّئَاتِهِمْ فِي أَصْحَابِ الْجَنَّةِ ۖ وَعْدَ الصِّدْقِ الَّذِي كَانُوا يُوعَدُونَ﴿١٦﴾
16. Hao ndio wale ambao Tunawatakabalia mazuri zaidi ya yale
waliyoyatenda, na Tunayaachilia mbali (Tunasamehe) maovu yao; (watakuwa)
katika watu wa Jannah. Ahadi ya kweli waliyokuwa wameahidiwa.
وَالَّذِي
قَالَ لِوَالِدَيْهِ أُفٍّ لَّكُمَا أَتَعِدَانِنِي أَنْ أُخْرَجَ وَقَدْ
خَلَتِ الْقُرُونُ مِن قَبْلِي وَهُمَا يَسْتَغِيثَانِ اللَّـهَ وَيْلَكَ
آمِنْ إِنَّ وَعْدَ اللَّـهِ حَقٌّ فَيَقُولُ مَا هَـٰذَا إِلَّا
أَسَاطِيرُ الْأَوَّلِينَ﴿١٧﴾
17. Na yule anaewaambia wazazi wake: “Uff (neno la karaha
kama kuguna ‘Ah!); mnanitishia kwamba nitatolewa (kufufuliwa) na hali
zimekwishapita karne nyingi kabla yangu; nao (wazee) wawili wanaomba
msaada kwa Allaah, na (humwambia mtoto wao): “Ole wako amini! Hakika
ahadi ya Allaah ni haki.” Lakini husema: “Haya si chochote isipokuwa ni
hekaya za watu wa kale.”
أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ حَقَّ عَلَيْهِمُ الْقَوْلُ فِي أُمَمٍ قَدْ خَلَتْ مِن قَبْلِهِم مِّنَ الْجِنِّ وَالْإِنسِ ۖ إِنَّهُمْ كَانُوا خَاسِرِينَ﴿١٨﴾
18. Hao ndio wale ambao imehakiki juu yao kauli (ya adhabu) katika
umati nyingi zilizokwishapita kabla yao miongoni mwa majini na wanadamu,
hakika wao wamekuwa ni wenye kukhasirika.
وَلِكُلٍّ دَرَجَاتٌ مِّمَّا عَمِلُوا ۖ وَلِيُوَفِّيَهُمْ أَعْمَالَهُمْ وَهُمْ لَا يُظْلَمُونَ﴿١٩﴾
19. Na kwa wote watakuwa na daraja kutokana na yale waliyoyatenda; na
ili (Allaah) Awalipe kikamilifu ‘amali zao, nao hawatodhulumiwa.
وَيَوْمَ
يُعْرَضُ الَّذِينَ كَفَرُوا عَلَى النَّارِ أَذْهَبْتُمْ طَيِّبَاتِكُمْ
فِي حَيَاتِكُمُ الدُّنْيَا وَاسْتَمْتَعْتُم بِهَا فَالْيَوْمَ تُجْزَوْنَ
عَذَابَ الْهُونِ بِمَا كُنتُمْ تَسْتَكْبِرُونَ فِي الْأَرْضِ بِغَيْرِ
الْحَقِّ وَبِمَا كُنتُمْ تَفْسُقُونَ﴿٢٠﴾
20. Na siku watakayotandazwa wale waliokufuru kwenye Moto (waambiwe):
“Je, mshamaliza vizuri vyenu katika uhai wenu wa dunia na
mshajistarehesha nayo? Basi leo mtalipwa adhabu ya udhalilifu kwa yale
mliyokuwa mkitakabari katika ardhi bila ya haki na kwa sababu mlikuwa
mnafanya ufasiki.”
وَاذْكُرْ
أَخَا عَادٍ إِذْ أَنذَرَ قَوْمَهُ بِالْأَحْقَافِ وَقَدْ خَلَتِ
النُّذُرُ مِن بَيْنِ يَدَيْهِ وَمِنْ خَلْفِهِ أَلَّا تَعْبُدُوا إِلَّا
اللَّـهَ إِنِّي أَخَافُ عَلَيْكُمْ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ﴿٢١﴾
21. Na mtaje (Huwd) ndugu (yao kina) ‘Aad alipowaonya watu wake katika Ahqaaf (nchi
ya machuguu ya mchanga) na walikwishapita waonyaji kabla yake na baada
yake: “Msiabudu isipokuwa Allaah. Hakika mimi nakukhofieni adhabu ya
Siku adhimu.”
قَالُوا أَجِئْتَنَا لِتَأْفِكَنَا عَنْ آلِهَتِنَا فَأْتِنَا بِمَا تَعِدُنَا إِن كُنتَ مِنَ الصَّادِقِينَ﴿٢٢﴾
22. Wakasema: “Je, umetujia ili utugeuzilie mbali na miungu yetu? Basi tuletee hayo unayotuahidi ukiwa ni miongoni mwa wakweli.”
قَالَ إِنَّمَا الْعِلْمُ عِندَ اللَّـهِ وَأُبَلِّغُكُم مَّا أُرْسِلْتُ بِهِ وَلَـٰكِنِّي أَرَاكُمْ قَوْمًا تَجْهَلُونَ﴿٢٣﴾
23. (Huwd) Akasema: “Hakika ujuzi (wa wakati kufika) uko kwa Allaah,
nami nabalighisha ambayo nimetumwa kwayo lakini nakuoneni nyinyi ni
kaumu wenye kufanya ujahili.”
فَلَمَّا رَأَوْهُ عَارِضًا مُّسْتَقْبِلَ أَوْدِيَتِهِمْ قَالُوا هَـٰذَا عَارِضٌ مُّمْطِرُنَا ۚ بَلْ هُوَ مَا اسْتَعْجَلْتُم بِهِ ۖ رِيحٌ فِيهَا عَذَابٌ أَلِيمٌ﴿٢٤﴾
24. Basi walipoliona wingu lilotanda upeoni linaelekea
mabonde yao; walisema: “Hili wingu lilotanda upeoni lenye kutunyeshea
mvua.” (Hapana!) Bali hilo ndilo mloharakiza, ni upepo mbaya ndani yake
kuna adhabu iumizayo.
تُدَمِّرُ كُلَّ شَيْءٍ بِأَمْرِ رَبِّهَا فَأَصْبَحُوا لَا يُرَىٰ إِلَّا مَسَاكِنُهُمْ ۚ كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْقَوْمَ الْمُجْرِمِينَ﴿٢٥﴾
25. Unadamirisha kila kitu kwa amri ya Rabb (Mola) wake. Wakapambaukiwa hayaonekani isipokuwa masikani zao. Hivyo ndivyo Tunavyolipa jaza watu wahalifu.
وَلَقَدْ
مَكَّنَّاهُمْ فِيمَا إِن مَّكَّنَّاكُمْ فِيهِ وَجَعَلْنَا لَهُمْ
سَمْعًا وَأَبْصَارًا وَأَفْئِدَةً فَمَا أَغْنَىٰ عَنْهُمْ سَمْعُهُمْ
وَلَا أَبْصَارُهُمْ وَلَا أَفْئِدَتُهُم مِّن شَيْءٍ إِذْ كَانُوا
يَجْحَدُونَ بِآيَاتِ اللَّـهِ وَحَاقَ بِهِم مَّا كَانُوا بِهِ
يَسْتَهْزِئُونَ﴿٢٦﴾
26. Na kwa yakini Tuliwamakinisha katika ambayo Hatukumakinisheni
humo (nyinyi Maquraysh); na Tukawajaalia masikio na macho na nyoyo;
lakini hayakuwafaa masikio yao na wala macho yao na wala nyoyo zao kwa
chochote walipokuwa wakikanusha kwa ujeuri Aayaat (hoja, ishara) za Allaah na yakawazunguka ambayo walikuwa wakiyafanyia istihzai.
وَلَقَدْ أَهْلَكْنَا مَا حَوْلَكُم مِّنَ الْقُرَىٰ وَصَرَّفْنَا الْآيَاتِ لَعَلَّهُمْ يَرْجِعُونَ﴿٢٧﴾
27. Na kwa yakini Tuliangamiza miji iliyokuwa pembezoni mwenu, na Tukasarifu waziwazi Aayaat (hoja, dalili) ili wapate kurejea.
فَلَوْلَا نَصَرَهُمُ الَّذِينَ اتَّخَذُوا مِن دُونِ اللَّـهِ قُرْبَانًا آلِهَةً ۖ بَلْ ضَلُّوا عَنْهُمْ ۚ وَذَٰلِكَ إِفْكُهُمْ وَمَا كَانُوا يَفْتَرُونَ﴿٢٨﴾
28. Basi kwa nini wasiwanusuru wale waliowafanya badala ya Allaah
kuwa ni miungu ya kikurubisho (Kwake)? Bali wamewapotea, na huo ndio
uongo wao na yale waliyokuwa wakiyatunga.
وَإِذْ صَرَفْنَا إِلَيْكَ نَفَرًا مِّنَ الْجِنِّ يَسْتَمِعُونَ الْقُرْآنَ فَلَمَّا حَضَرُوهُ قَالُوا أَنصِتُوا ۖ فَلَمَّا قُضِيَ وَلَّوْا إِلَىٰ قَوْمِهِم مُّنذِرِينَ﴿٢٩﴾
29. Na (taja ee Muhammadصلى الله عليه وآله وسلم )
Tulipowaelekeza kwako kundi miongoni mwa majini wakisikiliza kwa makini
Qur-aan; walipoihudhuria, walisema: “Bakieni kimya msikilize!”
Ilipomalizika; waligeuka kurudi kwa kaumu yao wakiwa wenye kuonya.
قَالُوا
يَا قَوْمَنَا إِنَّا سَمِعْنَا كِتَابًا أُنزِلَ مِن بَعْدِ مُوسَىٰ
مُصَدِّقًا لِّمَا بَيْنَ يَدَيْهِ يَهْدِي إِلَى الْحَقِّ وَإِلَىٰ
طَرِيقٍ مُّسْتَقِيمٍ﴿٣٠﴾
30. Wakasema: “Enyi kaumu yetu! Hakika sisi tumesikia (kinasomwa)
Kitabu kimeteremshwa baada ya Muwsaa, kinachosadikisha yaliyo kabla
yake, kinaongoza kwenye haki na kuelekea njia iliyonyooka.
يَا قَوْمَنَا أَجِيبُوا دَاعِيَ اللَّـهِ وَآمِنُوا بِهِ يَغْفِرْ لَكُم مِّن ذُنُوبِكُمْ وَيُجِرْكُم مِّنْ عَذَابٍ أَلِيمٍ﴿٣١﴾
31. “Enyi kaumu yetu! Mwitikieni mlinganiaji wa Allaah, na
mwaminini! (Allaah) Atakughufurieni madhambi yenu, na Atakukingeni na
adhabu iumizayo.
وَمَن لَّا يُجِبْ دَاعِيَ اللَّـهِ فَلَيْسَ بِمُعْجِزٍ فِي الْأَرْضِ وَلَيْسَ لَهُ مِن دُونِهِ أَوْلِيَاءُ ۚ أُولَـٰئِكَ فِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ﴿٣٢﴾
32. “Na yeyote asiyemuitikia mlinganiaji ya Allaah, basi hawezi
kushinda kukwepa (adhabu) katika ardhi na hatokuwa na walinzi badala ya
Allaah. Hao wamo katika upotofu bayana.”
أَوَلَمْ
يَرَوْا أَنَّ اللَّـهَ الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَلَمْ
يَعْيَ بِخَلْقِهِنَّ بِقَادِرٍ عَلَىٰ أَن يُحْيِيَ الْمَوْتَىٰ ۚ بَلَىٰ إِنَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ﴿٣٣﴾
33. Je, hawaoni kwamba Allaah Ambaye Ameumba mbingu na ardhi na wala Hakuchoka kwa kuziumba kwake, (hawaoni) kuwa ni Qaadir (Muweza) wa kuwafufua wafu. Bila shaka! Hakika Yeye juu ya kila kitu ni Qadiyr (Muweza).
وَيَوْمَ يُعْرَضُ الَّذِينَ كَفَرُوا عَلَى النَّارِ أَلَيْسَ هَـٰذَا بِالْحَقِّ ۖ قَالُوا بَلَىٰ وَرَبِّنَا ۚ قَالَ فَذُوقُوا الْعَذَابَ بِمَا كُنتُمْ تَكْفُرُونَ﴿٣٤﴾
34. Na Siku watakayotandazwa wale waliokufuru kwenye Moto (Itasemwa): “Je, hii si kweli?” Watasema: “Bali ndio! Tunaapa kwa Rabb (Mola) wetu!” Atasema: “Basi onjeni adhabu kwa yale mliyokuwa mnakufuru.”
فَاصْبِرْ كَمَا صَبَرَ أُولُو الْعَزْمِ مِنَ الرُّسُلِ وَلَا تَسْتَعْجِل لَّهُمْ ۚ كَأَنَّهُمْ يَوْمَ يَرَوْنَ مَا يُوعَدُونَ لَمْ يَلْبَثُوا إِلَّا سَاعَةً مِّن نَّهَارٍ ۚ بَلَاغٌ ۚ فَهَلْ يُهْلَكُ إِلَّا الْقَوْمُ الْفَاسِقُونَ﴿٣٥﴾
35. Basi subiri (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم)
kama walivyosubiri wenye azimio madhubuti miongoni mwa Rasuli na wala
usiwaharakizie. (Itakuwa) Kama kwamba wao - Siku watakayoona ambayo
wameahidiwa – hawakubakia (duniani) isipokuwa saa moja (tu) katika
mchana. (Huu ni) Ubalighisho! Je, basi kwani huangamizwa isipokuwa watu
mafasiki?
Ukitaka kusoma Sura nyengine Rejeauliko toka
Ukiwa una shauri au maelezo juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii falhaqqiy@gmail.com
Ukiwa una shauri au maelezo juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii falhaqqiy@gmail.com