النِّسَاء
An-Nisaa: 4
(Imeteremka Makka)
بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ
يَا
أَيُّهَا النَّاسُ اتَّقُوا رَبَّكُمُ الَّذِي خَلَقَكُم مِّن نَّفْسٍ
وَاحِدَةٍ وَخَلَقَ مِنْهَا زَوْجَهَا وَبَثَّ مِنْهُمَا رِجَالًا كَثِيرًا
وَنِسَاءً ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ الَّذِي تَسَاءَلُونَ بِهِ وَالْأَرْحَامَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلَيْكُمْ رَقِيبًا ﴿١﴾
1. Enyi watu! Mcheni Rabb (Mola)
wenu Ambaye Amekuumbeni kutokana na nafsi moja (Aadam) na Akaumba
kutoka humo mke wake (Hawwaa) na Akaeneza kutoka hao wawili wanaume
wengi na wanawake. Na mcheni Allaah Ambaye Kwake mnaombana na jamaa.
Hakika Allaah Amekuwa juu yenu Raqiybaa (Mwenye kuchunga).
وَآتُوا الْيَتَامَىٰ أَمْوَالَهُمْ ۖ وَلَا تَتَبَدَّلُوا الْخَبِيثَ بِالطَّيِّبِ ۖ وَلَا تَأْكُلُوا أَمْوَالَهُمْ إِلَىٰ أَمْوَالِكُمْ ۚ إِنَّهُ كَانَ حُوبًا كَبِيرًا ﴿٢﴾
2. Na wapeni mayatima mali zao, na
wala msibadilishe kibaya (chenu) kwa kizuri (chao). Na wala msile mali
zao pamoja na mali zenu. Hakika hilo limekuwa ni dhambi kubwa.
وَإِنْ خِفْتُمْ أَلَّا تُقْسِطُوا فِي الْيَتَامَىٰ فَانكِحُوا مَا طَابَ لَكُم مِّنَ النِّسَاءِ مَثْنَىٰ وَثُلَاثَ وَرُبَاعَ ۖ فَإِنْ خِفْتُمْ أَلَّا تَعْدِلُوا فَوَاحِدَةً أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُكُمْ ۚ ذَٰلِكَ أَدْنَىٰ أَلَّا تَعُولُوا ﴿٣﴾
3. Na mkikhofu kuwa hamtoweza kufanya
uadilifu kwa mayatima; basi oeni waliokupendezeni katika wanawake;
wawili au watatu au wanne. Mkikhofu kuwa hamtoweza kufanya uadilifu,
basi (oeni) mmoja au ambao mikono yenu ya kulia imewamiliki (masuriya).
Hivyo ni karibu zaidi kwamba hamtoelemea (kudhulumu).
وَآتُوا النِّسَاءَ صَدُقَاتِهِنَّ نِحْلَةً ۚ فَإِن طِبْنَ لَكُمْ عَن شَيْءٍ مِّنْهُ نَفْسًا فَكُلُوهُ هَنِيئًا مَّرِيئًا ﴿٤﴾
4. Na wapeni wanawake (mnaowaoa)
mahari zao kwa maridhawa. Lakini wakitoa chochote wenyewe katika mahari
yao kwa khiari zao, basi kuleni kwa kufurahia na kunufaika (bila ya
dhara).
وَلَا
تُؤْتُوا السُّفَهَاءَ أَمْوَالَكُمُ الَّتِي جَعَلَ اللَّـهُ لَكُمْ
قِيَامًا وَارْزُقُوهُمْ فِيهَا وَاكْسُوهُمْ وَقُولُوا لَهُمْ قَوْلًا
مَّعْرُوفًا﴿٥﴾
5. Wala msiwape wasiokomaa akili mali
zenu ambazo Allaah Amekujaalieni kuwa ni njia ya kujipatia riziki, na
walisheni humo na wavisheni na waambieni maneno ya ma’-ruwfaa (ya haki na kwa huruma).
وَابْتَلُوا
الْيَتَامَىٰ حَتَّىٰ إِذَا بَلَغُوا النِّكَاحَ فَإِنْ آنَسْتُم
مِّنْهُمْ رُشْدًا فَادْفَعُوا إِلَيْهِمْ أَمْوَالَهُمْ ۖ وَلَا تَأْكُلُوهَا إِسْرَافًا وَبِدَارًا أَن يَكْبَرُوا ۚ وَمَن كَانَ غَنِيًّا فَلْيَسْتَعْفِفْ ۖ وَمَن كَانَ فَقِيرًا فَلْيَأْكُلْ بِالْمَعْرُوفِ ۚ فَإِذَا دَفَعْتُمْ إِلَيْهِمْ أَمْوَالَهُمْ فَأَشْهِدُوا عَلَيْهِمْ ۚ وَكَفَىٰ بِاللَّـهِ حَسِيبًا ﴿٦﴾
6. Na wajaribuni mayatima (uwezo wao
wa kufahamu na kusimamia mambo) mpaka wakifikia kuoa (kubalegehe). Na
mkihisi kupevuka kwao, basi wapeni mali zao. Wala msiile kwa israfu na
pupa kwa (kukhofu) kuwa watakuja kuwa watu wazima. Na (mlezi) aliyekuwa
tajiri basi ajizuie (kuchukua ujira kuwahudumia hao mayatima); na
aliyekuwa fakiri basi ale kwa ma’-ruwf (kadiri ya kukubalika ki shariy’ah). Mtapowapa mali zao washuhudizeni. Na Allaah Anatosheleza kuwa Hasiybaa (Mwenye kuhisabu).
لِّلرِّجَالِ
نَصِيبٌ مِّمَّا تَرَكَ الْوَالِدَانِ وَالْأَقْرَبُونَ وَلِلنِّسَاءِ
نَصِيبٌ مِّمَّا تَرَكَ الْوَالِدَانِ وَالْأَقْرَبُونَ مِمَّا قَلَّ
مِنْهُ أَوْ كَثُرَ ۚ نَصِيبًا مَّفْرُوضًا ﴿٧﴾
7. Wanaume wana fungu katika yale
waliyoacha wazazi na jamaa wa karibu. Na wanawake (pia) wana fungu
katika yale waliyoacha wazazi na jamaa wa karibu, ikiwa ni kidogo au
kingi; fungu iliyofaridhishwa.
وَإِذَا
حَضَرَ الْقِسْمَةَ أُولُو الْقُرْبَىٰ وَالْيَتَامَىٰ وَالْمَسَاكِينُ
فَارْزُقُوهُم مِّنْهُ وَقُولُوا لَهُمْ قَوْلًا مَّعْرُوفًا﴿٨﴾
8. Na wakati wa kugawa, wakihudhuria
jamaa wa karibu na mayatima na masikini, basi wapeni kitu katika hayo na
wasemezeni kauli ya ma’-ruwfaa (ifaayo ya haki na kwa huruma).
وَلْيَخْشَ
الَّذِينَ لَوْ تَرَكُوا مِنْ خَلْفِهِمْ ذُرِّيَّةً ضِعَافًا خَافُوا
عَلَيْهِمْ فَلْيَتَّقُوا اللَّـهَ وَلْيَقُولُوا قَوْلًا سَدِيدًا﴿٩﴾
9. Na waogope (hao walezi au
wasimamizi kukhini) wale ambao lau (nao) wangeliacha nyuma yao dhuriya
dhaifu wangeliwakhofia; basi wamche Allaah na waseme kauli iliyo sawa
(ya haki).
إِنَّ الَّذِينَ يَأْكُلُونَ أَمْوَالَ الْيَتَامَىٰ ظُلْمًا إِنَّمَا يَأْكُلُونَ فِي بُطُونِهِمْ نَارًا ۖ وَسَيَصْلَوْنَ سَعِيرًا ﴿١٠﴾
10. Hakika wale wanaokula mali ya
mayatima kwa dhulma hapana shaka kwamba wanakula katika matumbo yao
moto, na watauingia (Moto wa) Sa’iyraa (uwakao kwa nguvu).”
يُوصِيكُمُ اللَّـهُ فِي أَوْلَادِكُمْ ۖ لِلذَّكَرِ مِثْلُ حَظِّ الْأُنثَيَيْنِ ۚ فَإِن كُنَّ نِسَاءً فَوْقَ اثْنَتَيْنِ فَلَهُنَّ ثُلُثَا مَا تَرَكَ ۖ وَإِن كَانَتْ وَاحِدَةً فَلَهَا النِّصْفُ ۚ وَلِأَبَوَيْهِ لِكُلِّ وَاحِدٍ مِّنْهُمَا السُّدُسُ مِمَّا تَرَكَ إِن كَانَ لَهُ وَلَدٌ ۚ فَإِن لَّمْ يَكُن لَّهُ وَلَدٌ وَوَرِثَهُ أَبَوَاهُ فَلِأُمِّهِ الثُّلُثُ ۚ فَإِن كَانَ لَهُ إِخْوَةٌ فَلِأُمِّهِ السُّدُسُ ۚ مِن بَعْدِ وَصِيَّةٍ يُوصِي بِهَا أَوْ دَيْنٍ ۗ آبَاؤُكُمْ وَأَبْنَاؤُكُمْ لَا تَدْرُونَ أَيُّهُمْ أَقْرَبُ لَكُمْ نَفْعًا ۚ فَرِيضَةً مِّنَ اللَّـهِ ۗ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلِيمًا حَكِيمًا ﴿١١﴾
11. Allaah Anakuamrisheni katika
auladi wenu. Mwanamume atastahiki mfano wa fungu la wanawake wawili. Na
ikiwa wanawake ni zaidi ya wawili basi watastahiki theluthi mbili za
alichoacha (maiti). Na akiwa mwanamke ni mmoja pekee basi atastahiki
nusu, na wazazi wake wawili kila mmoja wao atastahiki sudusi (sehemu ya
sita) katika alichoacha (maiti) ikiwa (maiti huyo) anaye waladi wa
kiume. Na ikiwa hakuwa na waladi wa kiume na wazazi wake wawili ndio
warithi wake, basi mama yake atastahiki theluthi (sehemu ya tatu). Na
ikiwa (maiti huyo) anao ndugu basi mama yake atastahiki sudusi, baada ya
kutoa wasia aliousia (maiti) au (kulipa) deni (aloliacha). Baba zenu na
watoto wenu hamjui ni yupi miongoni mwao aliyekaribu zaidi kwenu kwa
manufaa. (Ugawaji huu wa mirathi) Ni shariy’ah kutoka kwa Allaah. Hakika Allaah ni ‘Aliyman-Hakiymaa (Mjuzi wa yote - Mwenye hikmah wa yote).
وَلَكُمْ نِصْفُ مَا تَرَكَ أَزْوَاجُكُمْ إِن لَّمْ يَكُن لَّهُنَّ وَلَدٌ ۚ فَإِن كَانَ لَهُنَّ وَلَدٌ فَلَكُمُ الرُّبُعُ مِمَّا تَرَكْنَ ۚ مِن بَعْدِ وَصِيَّةٍ يُوصِينَ بِهَا أَوْ دَيْنٍ ۚ وَلَهُنَّ الرُّبُعُ مِمَّا تَرَكْتُمْ إِن لَّمْ يَكُن لَّكُمْ وَلَدٌ ۚ فَإِن كَانَ لَكُمْ وَلَدٌ فَلَهُنَّ الثُّمُنُ مِمَّا تَرَكْتُم ۚ مِّن بَعْدِ وَصِيَّةٍ تُوصُونَ بِهَا أَوْ دَيْنٍ ۗ وَإِن كَانَ رَجُلٌ يُورَثُ كَلَالَةً أَوِ امْرَأَةٌ وَلَهُ أَخٌ أَوْ أُخْتٌ فَلِكُلِّ وَاحِدٍ مِّنْهُمَا السُّدُسُ ۚ فَإِن كَانُوا أَكْثَرَ مِن ذَٰلِكَ فَهُمْ شُرَكَاءُ فِي الثُّلُثِ ۚ مِن بَعْدِ وَصِيَّةٍ يُوصَىٰ بِهَا أَوْ دَيْنٍ غَيْرَ مُضَارٍّ ۚ وَصِيَّةً مِّنَ اللَّـهِ ۗ وَاللَّـهُ عَلِيمٌ حَلِيمٌ ﴿١٢﴾
12. Nanyi mtastahiki nusu katika
walichoacha wake zenu ikiwa hawakuwa na waladi. Na ikiwa wana waladi,
basi mtastahiki robo katika walichoacha, baada ya kutoa wasia waliyousia
au (kulipa) deni (waloliacha). Nao (wake zenu) watastahiki robo katika
mlichoacha ikiwa hamna waladi. Na ikiwa mna waladi basi (wake zenu)
watastahiki thumni katika mlichoacha, baada ya kutoa wasia mliousia au
kulipa deni. Na ikiwa mwanamume au mwanamke anayerithiwa hana mtoto wala
wazazi, lakini anaye kaka au dada, basi kila mmoja kati yao atastahiki
sudusi. Na wakiwa ni wengi ya hiyvo basi watashirikiana katika theluthi,
baada ya kutoa wasia uliousiwa na kulipwa deni pasipo kuleta dhara.
Huu ni wasia kutoka kwa Allaah, na Allaah ni ‘Aliymun-Haliym (Mjuzi wa yote - Mpole wa kuwavumilia waja).
تِلْكَ حُدُودُ اللَّـهِ ۚ وَمَن يُطِعِ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ يُدْخِلْهُ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا ۚ وَذَٰلِكَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ ﴿١٣﴾
13. Hiyo ni mipaka ya Allaah. Na yeyote atakayemtii Allaah na Rasuli Wake Atamuingiza Jannaat zipitazo chini yake mito, ni wenye kudumu humo, na huko ndiko kufuzu adhimu.
وَمَن يَعْصِ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ وَيَتَعَدَّ حُدُودَهُ يُدْخِلْهُ نَارًا خَالِدًا فِيهَا وَلَهُ عَذَابٌ مُّهِينٌ﴿١٤﴾
14. Na yeyote atakayemuasi Allaah na
Rasuli Wake na akapindukia mipaka Yake Atamuingiza Motoni, ni mwenye
kudumu humo na atapata adhabu ya kudhalilisha.
وَاللَّاتِي يَأْتِينَ الْفَاحِشَةَ مِن نِّسَائِكُمْ فَاسْتَشْهِدُوا عَلَيْهِنَّ أَرْبَعَةً مِّنكُمْ ۖ فَإِن شَهِدُوا فَأَمْسِكُوهُنَّ فِي الْبُيُوتِ حَتَّىٰ يَتَوَفَّاهُنَّ الْمَوْتُ أَوْ يَجْعَلَ اللَّـهُ لَهُنَّ سَبِيلًا ﴿١٥﴾
15. Na wale wanaofanya uchafu miongoni
mwa wanawake wenu, basi washuhudisheni (mashahidi) wanne kati yenu. Na
wakishuhudia basi wazuieni majumbani mpaka mauti yawafishe au Allaah
Awajaalie njia (nyingine).
وَاللَّذَانِ يَأْتِيَانِهَا مِنكُمْ فَآذُوهُمَا ۖ فَإِن تَابَا وَأَصْلَحَا فَأَعْرِضُوا عَنْهُمَا ۗ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ تَوَّابًا رَّحِيمًا ﴿١٦﴾
16. Na wale wawili wanaofanya huo (uchafu) waadhibuni. Wakitubu na kutengenea basi waacheni. Hakika Allaah ni Tawwabar-Rahiymaa (Mwingi wa kupokea tawbah - Mwenye kurehemu).
إِنَّمَا
التَّوْبَةُ عَلَى اللَّـهِ لِلَّذِينَ يَعْمَلُونَ السُّوءَ بِجَهَالَةٍ
ثُمَّ يَتُوبُونَ مِن قَرِيبٍ فَأُولَـٰئِكَ يَتُوبُ اللَّـهُ عَلَيْهِمْ ۗ وَكَانَ اللَّـهُ عَلِيمًا حَكِيمًا ﴿١٧﴾
17. Hakika tawbah inayokubaliwa na
Allaah ni ya wale wanaofanya uovu kwa ujahili kisha wakatubia haraka,
basi hao Allaah Anapokea tawbah yao. Na Allaah ni ‘Aliyman-Hakiymaa (Mjuzi wa yote - Mwenye hikmah wa yote).
وَلَيْسَتِ
التَّوْبَةُ لِلَّذِينَ يَعْمَلُونَ السَّيِّئَاتِ حَتَّىٰ إِذَا حَضَرَ
أَحَدَهُمُ الْمَوْتُ قَالَ إِنِّي تُبْتُ الْآنَ وَلَا الَّذِينَ
يَمُوتُونَ وَهُمْ كُفَّارٌ ۚ أُولَـٰئِكَ أَعْتَدْنَا لَهُمْ عَذَابًا أَلِيمًا ﴿١٨﴾
18. Lakini tawbah si kwa wale
wanaofanya maovu mpaka mauti yanapohudhuria kwa mmoja wao husema:
“Hakika mimi sasa nimetubu.” (Hao hawakubaliwi). Na wala wale wanaokufa
na hali wao ni makafiri. Hao Tumewaandalia adhabu iumizayo.
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا يَحِلُّ لَكُمْ أَن تَرِثُوا النِّسَاءَ كَرْهًا ۖ وَلَا تَعْضُلُوهُنَّ لِتَذْهَبُوا بِبَعْضِ مَا آتَيْتُمُوهُنَّ إِلَّا أَن يَأْتِينَ بِفَاحِشَةٍ مُّبَيِّنَةٍ ۚ وَعَاشِرُوهُنَّ بِالْمَعْرُوفِ ۚ فَإِن كَرِهْتُمُوهُنَّ فَعَسَىٰ أَن تَكْرَهُوا شَيْئًا وَيَجْعَلَ اللَّـهُ فِيهِ خَيْرًا كَثِيرًا ﴿١٩﴾
19. Enyi mlioamini! Si halaal
kwenu kurithi wanawake kwa kuwakirihisha. Na wala msiwazuie kwa inda
ili mpokonye baadhi ya vile mlivyowapa isipokuwa wakiwa wamefanya uchafu
bayana. Na kaeni nao kwa wema. Na mkiwachukia, basi huenda ikiwa
mnachukia jambo na Allaah Akalijaalia kuwa lenye kheri nyingi.
وَإِنْ أَرَدتُّمُ اسْتِبْدَالَ زَوْجٍ مَّكَانَ زَوْجٍ وَآتَيْتُمْ إِحْدَاهُنَّ قِنطَارًا فَلَا تَأْخُذُوا مِنْهُ شَيْئًا ۚ أَتَأْخُذُونَهُ بُهْتَانًا وَإِثْمًا مُّبِينًا ﴿٢٠﴾
20. Na mkitaka kubadlisha mke mahali
pa mke, na mmempa mmoja wao (zawadi ya) mirundi ya mali, basi msichukue
humo chochote. Je, mnakichukua kwa dhulma na dhambi iliyo bayana?
وَكَيْفَ تَأْخُذُونَهُ وَقَدْ أَفْضَىٰ بَعْضُكُمْ إِلَىٰ بَعْضٍ وَأَخَذْنَ مِنكُم مِّيثَاقًا غَلِيظًا﴿٢١﴾
21. Na mtachukuaje na hali nyinyi kwa nyinyi mmeingiliana, na (wao wanawake) wakapokea kwenu fungamano thabiti?
وَلَا تَنكِحُوا مَا نَكَحَ آبَاؤُكُم مِّنَ النِّسَاءِ إِلَّا مَا قَدْ سَلَفَ ۚ إِنَّهُ كَانَ فَاحِشَةً وَمَقْتًا وَسَاءَ سَبِيلًا ﴿٢٢﴾
22. Na wala msiwaoe (wake) waliowaoa
baba zenu isipokuwa yaliyokwisha pita. Hakika hayo yalikuwa ni uchafu na
chukizo (kwa Allaah) na njia ovu.
حُرِّمَتْ
عَلَيْكُمْ أُمَّهَاتُكُمْ وَبَنَاتُكُمْ وَأَخَوَاتُكُمْ وَعَمَّاتُكُمْ
وَخَالَاتُكُمْ وَبَنَاتُ الْأَخِ وَبَنَاتُ الْأُخْتِ وَأُمَّهَاتُكُمُ
اللَّاتِي أَرْضَعْنَكُمْ وَأَخَوَاتُكُم مِّنَ الرَّضَاعَةِ وَأُمَّهَاتُ
نِسَائِكُمْ وَرَبَائِبُكُمُ اللَّاتِي فِي حُجُورِكُم مِّن نِّسَائِكُمُ
اللَّاتِي دَخَلْتُم بِهِنَّ فَإِن لَّمْ تَكُونُوا دَخَلْتُم بِهِنَّ
فَلَا جُنَاحَ عَلَيْكُمْ وَحَلَائِلُ أَبْنَائِكُمُ الَّذِينَ مِنْ
أَصْلَابِكُمْ وَأَن تَجْمَعُوا بَيْنَ الْأُخْتَيْنِ إِلَّا مَا قَدْ
سَلَفَ ۗ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿٢٣﴾
23. Mmeharamishiwa (kuwaoa) mama zenu,
na mabinti zenu, na dada zenu, na shangazi zenu, na makhalati zenu
(mama wakubwa na wadogo), na mabinti wa kaka, na mabinti wa dada, na
mama zenu ambao wamekunyonyesheni, na ndugu zenu kwa kunyonya, na mama
wa wake zenu, na watoto wenu wa kambo walio katika ulinzi wenu
waliozaliwa na wake zenu ambao mmewaingilia. Lakini ikiwa hamkuwaingilia
basi hakuna dhambi (kuwaoa). Na (mmeharamishwa) wake wa watoto wenu
waliotoka katika migongo yenu. Na (mmeharamishwa) kuwaoa dada wawili kwa
wakati mmoja, isipokuwa yaliyokwisha pita. Hakika Allaah ni Ghafuwrar-Rahiymaa (Mwingi wa kughufuria - Mwenye kurehemu).
وَالْمُحْصَنَاتُ مِنَ النِّسَاءِ إِلَّا مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُكُمْ ۖ كِتَابَ اللَّـهِ عَلَيْكُمْ ۚ وَأُحِلَّ لَكُم مَّا وَرَاءَ ذَٰلِكُمْ أَن تَبْتَغُوا بِأَمْوَالِكُم مُّحْصِنِينَ غَيْرَ مُسَافِحِينَ ۚ فَمَا اسْتَمْتَعْتُم بِهِ مِنْهُنَّ فَآتُوهُنَّ أُجُورَهُنَّ فَرِيضَةً ۚ وَلَا جُنَاحَ عَلَيْكُمْ فِيمَا تَرَاضَيْتُم بِهِ مِن بَعْدِ الْفَرِيضَةِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلِيمًا حَكِيمًا﴿٢٤﴾
24. Na (Mmeharamishiwa pia) wanawake walio katika ndoa isipokuwa iliyowamiliki mikono yenu ya kuume. Ni shariy’ah
ya Allaah kwenu. Na mmehalalishiwa (wengineo) wasiokuwa hao, mtafute
(kuwaoa) kwa (mahari kutoka) mali zenu mkijistahi pasi na kuzini. Basi
mliostarehe nao (katika ndoa) wapeni mahari yao kuwa ni waajib. Na wala
si dhambi kwenu katika mliyoridhiana baada ya yaliyowajibika. Hakika
Allaah daima ni ‘Aliyman-Hakiymaa (Mjuzi wa yote - Mwenye hikmah wa yote).
وَمَن
لَّمْ يَسْتَطِعْ مِنكُمْ طَوْلًا أَن يَنكِحَ الْمُحْصَنَاتِ
الْمُؤْمِنَاتِ فَمِن مَّا مَلَكَتْ أَيْمَانُكُم مِّن فَتَيَاتِكُمُ
الْمُؤْمِنَاتِ ۚ وَاللَّـهُ أَعْلَمُ بِإِيمَانِكُم ۚ بَعْضُكُم مِّن بَعْضٍ ۚ
فَانكِحُوهُنَّ بِإِذْنِ أَهْلِهِنَّ وَآتُوهُنَّ أُجُورَهُنَّ
بِالْمَعْرُوفِ مُحْصَنَاتٍ غَيْرَ مُسَافِحَاتٍ وَلَا مُتَّخِذَاتِ
أَخْدَانٍ ۚ فَإِذَا أُحْصِنَّ فَإِنْ أَتَيْنَ بِفَاحِشَةٍ فَعَلَيْهِنَّ نِصْفُ مَا عَلَى الْمُحْصَنَاتِ مِنَ الْعَذَابِ ۚ ذَٰلِكَ لِمَنْ خَشِيَ الْعَنَتَ مِنكُمْ ۚ وَأَن تَصْبِرُوا خَيْرٌ لَّكُمْ ۗ وَاللَّـهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ﴿٢٥﴾
25. Na asiyeweza kati yenu kupata mali ya kuolea wanawake Waumini waliohuru, basi
(aoe) katika wale iliyomiliki mikono yenu ya kulia miongoni mwa
wajakazi wenu Waumini. Na Allaah Anajua zaidi iymaan yenu. Nyinyi kwa
nyinyi. Basi waoeni kwa idhini ya watu wao na wapeni mahari yao kwa ma’-ruwf (ada inayokubalika) (waoeni na hali ya kuwa ni) wanaojistiri na machafu si makahaba na wala si wenye kuchukua hawara. Na
watakapohifadhiwa katika ndoa, kisha wakafanya uchafu (zinaa) basi
adhabu yao itakuwa ni nusu ya adhabu ya waliyowekewa wanawake waliohuru
(wasioolewa). Hayo ni kwa yule anayeogopa dhambi ya zinaa miongoni
mwenu. Na mkisubiri ni kheri kwenu. Na Allaah ni Ghafuwrur-Rahiym (Mwingi wa kughufuria – Mwenye kurehemu).
يُرِيدُ اللَّـهُ لِيُبَيِّنَ لَكُمْ وَيَهْدِيَكُمْ سُنَنَ الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ وَيَتُوبَ عَلَيْكُمْ ۗ وَاللَّـهُ عَلِيمٌ حَكِيمٌ﴿٢٦﴾
26. Allaah Anataka kukubainishieni (yaliyo halaal na haraam) na kukuongozeni nyendo (nzuri) za wale walio kabla yenu, na Apokee tawbah kwenu. Na Allaah ni ‘Aliymun-Hakiym (Mjuzi wa yote - Mwenye hikmah wa yote).
وَاللَّـهُ يُرِيدُ أَن يَتُوبَ عَلَيْكُمْ وَيُرِيدُ الَّذِينَ يَتَّبِعُونَ الشَّهَوَاتِ أَن تَمِيلُوا مَيْلًا عَظِيمًا﴿٢٧﴾
27. Na Allaah Anataka kupokea tawbah
kwenu; na wale wanaofuata matamanio (yao) wanataka mkengeuke mkengeuko
mkuu (uliokhalifu haki).
يُرِيدُ اللَّـهُ أَن يُخَفِّفَ عَنكُمْ ۚ وَخُلِقَ الْإِنسَانُ ضَعِيفًا﴿٢٨﴾
28. Allaah Anataka kukukhafifishieni (tabu zenu); kwani insani ameumbwa dhaifu.
يَا
أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَأْكُلُوا أَمْوَالَكُم بَيْنَكُم
بِالْبَاطِلِ إِلَّا أَن تَكُونَ تِجَارَةً عَن تَرَاضٍ مِّنكُمْ ۚ وَلَا تَقْتُلُوا أَنفُسَكُمْ ۚ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ بِكُمْ رَحِيمًا﴿٢٩﴾
29. Enyi mlioamini! Msiliane mali zenu
kwa ubatilifu, isipokuwa iwe biashara kwa kuridhiana baina yenu. Wala
msijiue (wala msiue wenzenu). Hakika Allaah daima kwenu ni Rahiymaa (Mwenye kurehemu).
وَمَن يَفْعَلْ ذَٰلِكَ عُدْوَانًا وَظُلْمًا فَسَوْفَ نُصْلِيهِ نَارًا ۚ وَكَانَ ذَٰلِكَ عَلَى اللَّـهِ يَسِيرًا﴿٣٠﴾
30. Na atakayefanya hivyo kwa uadui na dhulma, basi Tutamuingiza Motoni. Na hilo kwa Allaah ni mepesi.
إِن تَجْتَنِبُوا كَبَائِرَ مَا تُنْهَوْنَ عَنْهُ نُكَفِّرْ عَنكُمْ سَيِّئَاتِكُمْ وَنُدْخِلْكُم مُّدْخَلًا كَرِيمًا﴿٣١﴾
31. Mkijiepusha na kabaaira (madhambi makubwa) mnayokatazwa Tutakufutieni madhambi yenu madogo na Tutakuingizeni katika mahali patukufu (Peponi).
وَلَا تَتَمَنَّوْا مَا فَضَّلَ اللَّـهُ بِهِ بَعْضَكُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ ۚ لِّلرِّجَالِ نَصِيبٌ مِّمَّا اكْتَسَبُوا ۖ وَلِلنِّسَاءِ نَصِيبٌ مِّمَّا اكْتَسَبْنَ ۚ وَاسْأَلُوا اللَّـهَ مِن فَضْلِهِ ۗ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمًا﴿٣٢﴾
32. Wala msitamani ambayo Allaah
Amewafadhilisha baadhi yenu kuliko wengine. Wanaume wanayo sehemu katika
waliyoyachuma, na wanawake wana sehemu katika waliyoyachuma. Na
muombeni Allaah fadhila Zake. Hakika Allaah daima kwa kila kitu ni ‘Aliymaa (Mjuzi).
وَلِكُلٍّ جَعَلْنَا مَوَالِيَ مِمَّا تَرَكَ الْوَالِدَانِ وَالْأَقْرَبُونَ ۚ وَالَّذِينَ عَقَدَتْ أَيْمَانُكُمْ فَآتُوهُمْ نَصِيبَهُمْ ۚ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ شَهِيدًا﴿٣٣﴾
33. Na kila mmoja
Tumemuwekea jamaa (zake) wa kurithi katika yale waliyoyaacha wazazi
wawili na jamaa wa karibu. Na wale mliofungamana nao viapo basi wapeni sehemu yao. Hakika Allaah daima juu ya kila kitu ni Shahiydaa (Mwenye kushuhudia).
الرِّجَالُ قَوَّامُونَ عَلَى النِّسَاءِ بِمَا فَضَّلَ اللَّـهُ بَعْضَهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ وَبِمَا أَنفَقُوا مِنْ أَمْوَالِهِمْ ۚ فَالصَّالِحَاتُ قَانِتَاتٌ حَافِظَاتٌ لِّلْغَيْبِ بِمَا حَفِظَ اللَّـهُ ۚ وَاللَّاتِي تَخَافُونَ نُشُوزَهُنَّ فَعِظُوهُنَّ وَاهْجُرُوهُنَّ فِي الْمَضَاجِعِ وَاضْرِبُوهُنَّ ۖ فَإِنْ أَطَعْنَكُمْ فَلَا تَبْغُوا عَلَيْهِنَّ سَبِيلًا ۗ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلِيًّا كَبِيرًا﴿٣٤﴾
34. Wanaume ni wasimamizi juu ya wanawake kwa kuwa Allaah Amefadhilisha baadhi yao kuliko wengine na kwa sababu ya (matumizi) wanayotoa katika mali zao. Basi wanawake wema watiifu, wenye kuhifadhi (hata) wanapokuwa hawapo (waume zao) kwa kuwa Allaah (Ameamrisha) wayahifadhi. Na wale (wanawake) ambao
mnakhofu uasi wao, basi waonyeni na (wakiendelea uasi) wahameni katika
malazi (vitanda) na (mwishowe wakishikilia uasi) wapigeni. Wakikutiini,
basi msitafute dhidi yao njia (ya kuwaudhi bure). Hakika Allaah daima ni ‘Aliyyan Kabiyraa (Mwenye Uluwa, Ametukuka – Mkubwa wa dhati, vitendo na sifa).
وَإِنْ
خِفْتُمْ شِقَاقَ بَيْنِهِمَا فَابْعَثُوا حَكَمًا مِّنْ أَهْلِهِ
وَحَكَمًا مِّنْ أَهْلِهَا إِن يُرِيدَا إِصْلَاحًا يُوَفِّقِ اللَّـهُ
بَيْنَهُمَا ۗ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلِيمًا خَبِيرًا﴿٣٥﴾
35. Na mkikhofu mafarikiano baina yao
(mke na mume), basi pelekeni mwamuzi kutoka watu wake (mume) na mwamuzi
kutoka watu wake (mke). Wakitaka sulhu (mapatano) Allaah Atawawafikisha
baina yao. Hakika Allaah daima ni ‘Aliyman Khabiyraa (Mjuzi wa yote - Mjuzi wa yaliyodhahiri na yaliyofichikana).
وَاعْبُدُوا اللَّـهَ وَلَا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا ۖ
وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا وَبِذِي الْقُرْبَىٰ وَالْيَتَامَىٰ
وَالْمَسَاكِينِ وَالْجَارِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَالْجَارِ الْجُنُبِ
وَالصَّاحِبِ بِالْجَنبِ وَابْنِ السَّبِيلِ وَمَا مَلَكَتْ أَيْمَانُكُمْ ۗ إِنَّ اللَّـهَ لَا يُحِبُّ مَن كَانَ مُخْتَالًا فَخُورًا﴿٣٦﴾
36. Na mwabuduni Allaah na wala msimshirikishe na chochote. Na wafanyieni
ihsaan wazazi wawili na jamaa wa karibu, na mayatima, na masikini na
majirani wa karibu na majirani walio mbali, na rafiki wa ubavuni na
msafiri na wale iliyowamiliki mikono yenu ya kulia. Hakika Allaah Hapendi mwenye majivuno mwenye kujifakharisha.
الَّذِينَ يَبْخَلُونَ وَيَأْمُرُونَ النَّاسَ بِالْبُخْلِ وَيَكْتُمُونَ مَا آتَاهُمُ اللَّـهُ مِن فَضْلِهِ ۗ وَأَعْتَدْنَا لِلْكَافِرِينَ عَذَابًا مُّهِينًا﴿٣٧﴾
37. Wale wanaofanya ubakhili na
wanawaamrisha watu ubakhili na wanaficha Aliyowapa Allaah katika fadhila
Zake. Na Tumewaandalia makafiri adhabu ya kudhalilisha.
وَالَّذِينَ يُنفِقُونَ أَمْوَالَهُمْ رِئَاءَ النَّاسِ وَلَا يُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ وَلَا بِالْيَوْمِ الْآخِرِ ۗ وَمَن يَكُنِ الشَّيْطَانُ لَهُ قَرِينًا فَسَاءَ قَرِينًا﴿٣٨﴾
38. Na (pia) wale wanaotoa malizao kwa riyaa-a (kujionyesha mbele) ya watu na wala hawamwamini Allaah wala Siku ya Mwisho. Na yule ambaye shaytwaan amekuwa ni rafiki yake mwandani, basi mbaya aliyoje rafiki mwandani (huyo).
وَمَاذَا عَلَيْهِمْ لَوْ آمَنُوا بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ وَأَنفَقُوا مِمَّا رَزَقَهُمُ اللَّـهُ ۚ وَكَانَ اللَّـهُ بِهِمْ عَلِيمًا﴿٣٩﴾
39. Na ingekuwa nini juu yao lau
wangelimwamini Allaah na Siku ya Mwisho na wakatoa katika yale
Aliyowaruzuku Allaah. Na Allaah daima kwao ni ‘Aliymaa (Mjuzi).
إِنَّ اللَّـهَ لَا يَظْلِمُ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ ۖ وَإِن تَكُ حَسَنَةً يُضَاعِفْهَا وَيُؤْتِ مِن لَّدُنْهُ أَجْرًا عَظِيمًا﴿٤٠﴾
40. Hakika Allaah Hadhulumu (viumbe
Vyake hata) uzito wa atomu (au sisimizi). Na ikiwa ni (‘amali) nzuri
Huizidisha na Hutoa kutoka Kwake ujira adhimu.
فَكَيْفَ إِذَا جِئْنَا مِن كُلِّ أُمَّةٍ بِشَهِيدٍ وَجِئْنَا بِكَ عَلَىٰ هَـٰؤُلَاءِ شَهِيدًا﴿٤١﴾
41. Basi itakuwaje Tutakapoleta kutoka kila Ummah shahidi, na Tukakuleta (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) kuwa shahidi juu ya hawa?
يَوْمَئِذٍ يَوَدُّ الَّذِينَ كَفَرُوا وَعَصَوُا الرَّسُولَ لَوْ تُسَوَّىٰ بِهِمُ الْأَرْضُ وَلَا يَكْتُمُونَ اللَّـهَ حَدِيثًا﴿٤٢﴾
42. Siku hiyo wale waliokufuru na
wakamuasi Rasuli watatamani lau ardhi isawazishwe juu yao. Na wala
hawatoweza kumficha Allaah hadiythaa (kauli hata moja).
يَا
أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَقْرَبُوا الصَّلَاةَ وَأَنتُمْ
سُكَارَىٰ حَتَّىٰ تَعْلَمُوا مَا تَقُولُونَ وَلَا جُنُبًا إِلَّا
عَابِرِي سَبِيلٍ حَتَّىٰ تَغْتَسِلُوا ۚ
وَإِن كُنتُم مَّرْضَىٰ أَوْ عَلَىٰ سَفَرٍ أَوْ جَاءَ أَحَدٌ مِّنكُم
مِّنَ الْغَائِطِ أَوْ لَامَسْتُمُ النِّسَاءَ فَلَمْ تَجِدُوا مَاءً
فَتَيَمَّمُوا صَعِيدًا طَيِّبًا فَامْسَحُوا بِوُجُوهِكُمْ وَأَيْدِيكُمْ ۗ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَفُوًّا غَفُورًا﴿٤٣﴾
43. Enyi mloamini! Msikaribie Swalaah na hali mmelewa mpaka mjue mnayoyasema, na wala (msikaribie) hali mna janaba isipokuwa wapita njia (ya mahali pa kuswali) mpaka muoge ghuslu
(josho). Na mkiwa wagonjwa (mmekatazwa kutumia maji) au safarini au
mmoja wenu ametoka msalani au mmewagusa (mmewaingilia) wanawake kisha
hamkupata maji, basi mtayammamu (ikusudieni) ardhi safi ya mchanga,
pakeni nyuso zenu na mikono yenu. Hakika Allaah daima ni ‘Afuwwan Ghafuwraa (Mwingi wa kusamehe - Mwingi wa kughufuria).
أَلَمْ تَرَ إِلَى الَّذِينَ أُوتُوا نَصِيبًا مِّنَ الْكِتَابِ يَشْتَرُونَ الضَّلَالَةَ وَيُرِيدُونَ أَن تَضِلُّوا السَّبِيلَ﴿٤٤﴾
44. Je, huoni (huzingatii) wale waliopewa sehemu ya Kitabu wanakhiari upotofu na wanataka mpotee njia?
وَاللَّـهُ أَعْلَمُ بِأَعْدَائِكُمْ ۚ وَكَفَىٰ بِاللَّـهِ وَلِيًّا وَكَفَىٰ بِاللَّـهِ نَصِيرًا﴿٤٥﴾
45. Na Allaah Anawajua zaidi maadui zenu, na Allaah Anatosha kuwa Waliyyaa (Mlinzi, Msimamizi) na Allaah Anatosha kuwa Naswiyraa (Mwenye kunusuru).
مِّنَ
الَّذِينَ هَادُوا يُحَرِّفُونَ الْكَلِمَ عَن مَّوَاضِعِهِ وَيَقُولُونَ
سَمِعْنَا وَعَصَيْنَا وَاسْمَعْ غَيْرَ مُسْمَعٍ وَرَاعِنَا لَيًّا
بِأَلْسِنَتِهِمْ وَطَعْنًا فِي الدِّينِ ۚ
وَلَوْ أَنَّهُمْ قَالُوا سَمِعْنَا وَأَطَعْنَا وَاسْمَعْ وَانظُرْنَا
لَكَانَ خَيْرًا لَّهُمْ وَأَقْوَمَ وَلَـٰكِن لَّعَنَهُمُ اللَّـهُ
بِكُفْرِهِمْ فَلَا يُؤْمِنُونَ إِلَّا قَلِيلًا﴿٤٦﴾
46. Katika Mayahudi wako
wanaobadilisha maneno kuyatoa mahali pake, na husema: “Tumesikia” na
“Tumeasi”; na (wanasema kumwambia Rasuli): “Sikia bila kusikilizwa.” Na
(hulitamka tamko la): “raa’inaa” kwa kuzipotoa ndimi zao na kutukana Dini. Na lau wangesema: “Tumesikia na tumetii na sikia na undhwurnaa” ingelikuwa kheri kwao na yenye kufaa zaidi. Lakini Allaah Amewalaani kwa kufru yao; basi hawaamini isipokuwa wachache tu.
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَقُولُوا رَاعِنَا وَقُولُوا انظُرْنَا وَاسْمَعُوا ۗ وَلِلْكَافِرِينَ عَذَابٌ أَلِيمٌ ﴿١٠٤﴾
104. Enyi mlioamini, msiseme (kumwambia Rasuli wa Allaah) “raa’inaa” lakini semeni “undhwurnaa” na sikilizeni. Na makafiri watapata adhabu iumizayo.
يَا
أَيُّهَا الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ آمِنُوا بِمَا نَزَّلْنَا
مُصَدِّقًا لِّمَا مَعَكُم مِّن قَبْلِ أَن نَّطْمِسَ وُجُوهًا
فَنَرُدَّهَا عَلَىٰ أَدْبَارِهَا أَوْ نَلْعَنَهُمْ كَمَا لَعَنَّا
أَصْحَابَ السَّبْتِ ۚ وَكَانَ أَمْرُ اللَّـهِ مَفْعُولًا﴿٤٧﴾
47. Enyi mliopewa Kitabu! Aminini yale Tuliyoyateremsha (kwa Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) yanayosadikisha yale mliyonayo, kabla hatujabadilisha nyuso Tukazirudisha kisogoni, au Tukawalaani kama Tulivyowalaani watu wa As-Sabt (waliovunja shariy’ah ya Jumamosi). Na amri ya Allaah ni ya kufanyika tu.
إِنَّ اللَّـهَ لَا يَغْفِرُ أَن يُشْرَكَ بِهِ وَيَغْفِرُ مَا دُونَ ذَٰلِكَ لِمَن يَشَاءُ ۚ وَمَن يُشْرِكْ بِاللَّـهِ فَقَدِ افْتَرَىٰ إِثْمًا عَظِيمًا﴿٤٨﴾
48. Hakika Allaah Haghufuri
kushirikishwa; lakini Anaghufuria yasiyokuwa hayo kwa Amtakae. Na
yeyote atakayemshirikisha Allaah basi kwa yakini amebuni dhambi kuu.
أَلَمْ تَرَ إِلَى الَّذِينَ يُزَكُّونَ أَنفُسَهُم ۚ بَلِ اللَّـهُ يُزَكِّي مَن يَشَاءُ وَلَا يُظْلَمُونَ فَتِيلًا﴿٤٩﴾
49. Je, hukuwaona wale wanaojitakasa nafsi zao? Bali Allaah Humtakasa Amtakaye; na wala hawatodhulumiwa fatiylaa (kadiri ya uzi katika kokwa ya tende).
انظُرْ كَيْفَ يَفْتَرُونَ عَلَى اللَّـهِ الْكَذِبَ ۖ وَكَفَىٰ بِهِ إِثْمًا مُّبِينًا﴿٥٠﴾
50. Tazama vipi wanavyomtungia uongo Allaah; na yatosha haya kuwa dhambi za dhahiri.
أَلَمْ
تَرَ إِلَى الَّذِينَ أُوتُوا نَصِيبًا مِّنَ الْكِتَابِ يُؤْمِنُونَ
بِالْجِبْتِ وَالطَّاغُوتِ وَيَقُولُونَ لِلَّذِينَ كَفَرُوا هَـٰؤُلَاءِ
أَهْدَىٰ مِنَ الَّذِينَ آمَنُوا سَبِيلًا﴿٥١﴾
51. Je, huwaoni wale waliopewa sehemu ya Kitabu wanaamini al-jibt (mazimwi, itikadi potofu, sanamu) na atw-twaaghuwt (miungu ya uongo) na wanasema juu ya wale waliokufuru kuwa: “Hawa wameongoka zaidi katika njia kuliko wale walioamini.”
أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ لَعَنَهُمُ اللَّـهُ ۖ وَمَن يَلْعَنِ اللَّـهُ فَلَن تَجِدَ لَهُ نَصِيرًا﴿٥٢﴾
52. Hao ndio wale Allaah Aliowalaani. Na ambaye Allaah Amemlaani basi hatopata wa kumnusuru.
أَمْ لَهُمْ نَصِيبٌ مِّنَ الْمُلْكِ فَإِذًا لَّا يُؤْتُونَ النَّاسَ نَقِيرًا﴿٥٣﴾
53. Au wanayo sehemu ya ufalme (wa Allaah?) Basi, (ingelikuwa ni hivyo) wasingeliwapa watu naqiyraa (kadiri ya kitone cha kokwa ya tende).
أَمْ يَحْسُدُونَ النَّاسَ عَلَىٰ مَا آتَاهُمُ اللَّـهُ مِن فَضْلِهِ ۖ فَقَدْ آتَيْنَا آلَ إِبْرَاهِيمَ الْكِتَابَ وَالْحِكْمَةَ وَآتَيْنَاهُم مُّلْكًا عَظِيمًا﴿٥٤﴾
54. Au wanawahusudu watu (Nabiy Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) na
Waumini) kwa yale Aliyowapa Allaah katika fadhila Zake? Basi kwa yakini
Tuliwapa kizazi cha Ibraahiym; Kitabu na Hikmah na Tukawapa ufalme
adhimu.
فَمِنْهُم مَّنْ آمَنَ بِهِ وَمِنْهُم مَّن صَدَّ عَنْهُ ۚ وَكَفَىٰ بِجَهَنَّمَ سَعِيرًا﴿٥٥﴾
55. Basi miongoni mwao wako waliomuamini (Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) na miongoni mwao wako waliomkengeuka. Na Jahannam inatosheleza kuwa ni (Moto wa) Sa’iyraa (uwakao kwa nguvu).”
إِنَّ
الَّذِينَ كَفَرُوا بِآيَاتِنَا سَوْفَ نُصْلِيهِمْ نَارًا كُلَّمَا
نَضِجَتْ جُلُودُهُم بَدَّلْنَاهُمْ جُلُودًا غَيْرَهَا لِيَذُوقُوا
الْعَذَابَ ۗ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَزِيزًا حَكِيمًا﴿٥٦﴾
56. Hakika wale waliokanusha Aayaat
(na ishara, dalili n.k) Zetu Tutawaingiza Motoni. Kila ngozi zao
zitakapobanikika (zikaungua) Tutawabadilishia ngozi nyingine ili waionje
adhabu. Hakika Allaah ni ‘Aziyzan-Hakiymaa (Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika - Mwenye hikmah wa yote).
وَالَّذِينَ
آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ سَنُدْخِلُهُمْ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن
تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا أَبَدًا ۖ لَّهُمْ فِيهَا أَزْوَاجٌ مُّطَهَّرَةٌ ۖ وَنُدْخِلُهُمْ ظِلًّا ظَلِيلًا﴿٥٧﴾
57. Na wale walioamini na wakatenda mema Tutawaingiza Jannaat zipitazo chini yake mito, ni wenye kudumu humo abadi. Watapata humo wake waliotakasika na Tutawaingiza katika vivuli vya kina.
إِنَّ
اللَّـهَ يَأْمُرُكُمْ أَن تُؤَدُّوا الْأَمَانَاتِ إِلَىٰ أَهْلِهَا
وَإِذَا حَكَمْتُم بَيْنَ النَّاسِ أَن تَحْكُمُوا بِالْعَدْلِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ نِعِمَّا يَعِظُكُم بِهِ ۗ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ سَمِيعًا بَصِيرًا﴿٥٨﴾
58. Hakika Allaah Anakuamrisheni kurudisha amana kwa wenyewe. Na mtakapohukumu baina ya watu mhukumu kwa uadilifu. Hakika uzuri ulioje (wa mawaidha) Anayokuwaidhini nayo Allaah; hakika Allaah daima ni Samiy’an-Baswiyraa (Mwenye kusikia yote – Mwenye kuona yote)
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا أَطِيعُوا اللَّـهَ وَأَطِيعُوا الرَّسُولَ وَأُولِي الْأَمْرِ مِنكُمْ ۖ فَإِن تَنَازَعْتُمْ فِي شَيْءٍ فَرُدُّوهُ إِلَى اللَّـهِ وَالرَّسُولِ إِن كُنتُمْ تُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ ۚ ذَٰلِكَ خَيْرٌ وَأَحْسَنُ تَأْوِيلًا﴿٥٩﴾
59. Enyi mlioamini!
Mtiini Allaah na mtiini Rasuli na wenye madaraka katika nyinyi.
Mkizozana katika jambo basi lirudisheni kwa Allaah na Rasuli mkiwa
mnamwamini Allaah na Siku ya Mwisho. Hivyo ni (njia) bora na matokeo
mazuri zaidi.
أَلَمْ
تَرَ إِلَى الَّذِينَ يَزْعُمُونَ أَنَّهُمْ آمَنُوا بِمَا أُنزِلَ
إِلَيْكَ وَمَا أُنزِلَ مِن قَبْلِكَ يُرِيدُونَ أَن يَتَحَاكَمُوا إِلَى
الطَّاغُوتِ وَقَدْ أُمِرُوا أَن يَكْفُرُوا بِهِ وَيُرِيدُ الشَّيْطَانُ
أَن يُضِلَّهُمْ ضَلَالًا بَعِيدًا﴿٦٠﴾
60. Je, huoni wale wanaodai kwamba wao wameamini yaliyoteremshwa kwako (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) na yale yaliyoteremshwa kabla yako; wanataka wahukumiane kwa atw-twaaghuwt (ubatilifu, yasiyo katika shariy’ah) na hali wameamrishwa wakanushe hiyo. Na shaytwaan anataka awapoteze upotofu wa mbali.
وَإِذَا
قِيلَ لَهُمْ تَعَالَوْا إِلَىٰ مَا أَنزَلَ اللَّـهُ وَإِلَى الرَّسُولِ
رَأَيْتَ الْمُنَافِقِينَ يَصُدُّونَ عَنكَ صُدُودًا﴿٦١﴾
61. Na wanapoambiwa: “Njooni kwenye
yale Aliyoyateremsha Allaah na kwa Rasuli; utawaona wanafiki
wanakugeukilia mbali kwa mkengeuko.
فَكَيْفَ
إِذَا أَصَابَتْهُم مُّصِيبَةٌ بِمَا قَدَّمَتْ أَيْدِيهِمْ ثُمَّ
جَاءُوكَ يَحْلِفُونَ بِاللَّـهِ إِنْ أَرَدْنَا إِلَّا إِحْسَانًا
وَتَوْفِيقًا﴿٦٢﴾
62. Basi itakuwaje utakapowafika msiba
kwa sababu ya yale iliyotanguliza mikono yao? Kisha wakakujia wakiapa:
“Wa-Allaahi hatukutaka ila mazuri na mapatano.”
أُولَـٰئِكَ
الَّذِينَ يَعْلَمُ اللَّـهُ مَا فِي قُلُوبِهِمْ فَأَعْرِضْ عَنْهُمْ
وَعِظْهُمْ وَقُل لَّهُمْ فِي أَنفُسِهِمْ قَوْلًا بَلِيغًا﴿٦٣﴾
63. Hao ndio ambao Allaah Anayajua yaliyomo ndani ya nyoyo zao. Basi waachilie mbali na wape mawaidha na uwaambie maneno yatakayofikia kuathiri (nafsi zao).
وَمَا أَرْسَلْنَا مِن رَّسُولٍ إِلَّا لِيُطَاعَ بِإِذْنِ اللَّـهِ ۚ
وَلَوْ أَنَّهُمْ إِذ ظَّلَمُوا أَنفُسَهُمْ جَاءُوكَ فَاسْتَغْفَرُوا
اللَّـهَ وَاسْتَغْفَرَ لَهُمُ الرَّسُولُ لَوَجَدُوا اللَّـهَ تَوَّابًا
رَّحِيمًا﴿٦٤﴾
64. Na Hatukutuma Rasuli yeyote ila
atiiwe kwa idhini ya Allaah. Na lau wao pale walipojidhulumu nafsi zao
wangelikujia (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) wakamwomba Allaah maghfirah na Rasuli akawaombea maghfirah, basi wangelimkuta Allaah ni Tawwaabar-Rahiymaa (Mwingi wa kupokea tawbah – Mwenye kurehemu).
فَلَا
وَرَبِّكَ لَا يُؤْمِنُونَ حَتَّىٰ يُحَكِّمُوكَ فِيمَا شَجَرَ بَيْنَهُمْ
ثُمَّ لَا يَجِدُوا فِي أَنفُسِهِمْ حَرَجًا مِّمَّا قَضَيْتَ
وَيُسَلِّمُوا تَسْلِيمًا﴿٦٥﴾
65. Basi Naapa kwa Rabb (Mola) wako, hawatoamini
mpaka wakufanye wewe ni mwamuzi katika yale wanayozozanabaina yao,
kisha wasipate katika nyoyo zao karaha katika yale uliyohukumu na
wajisalimishe, kwa kujisalimisha (kikamilifu).
وَلَوْ
أَنَّا كَتَبْنَا عَلَيْهِمْ أَنِ اقْتُلُوا أَنفُسَكُمْ أَوِ اخْرُجُوا
مِن دِيَارِكُم مَّا فَعَلُوهُ إِلَّا قَلِيلٌ مِّنْهُمْ ۖ وَلَوْ أَنَّهُمْ فَعَلُوا مَا يُوعَظُونَ بِهِ لَكَانَ خَيْرًا لَّهُمْ وَأَشَدَّ تَثْبِيتًا﴿٦٦﴾
66. Na lau Tungeliwaamrisha: “Jiueni nafsi zenu na tokeni katika majumba yenu”; wasingelifanya hayo ila wachache miongoni mwao. Na lau wangelifanya yale waliyowaidhiwa nayo ingelikuwa kheri kwao na uthibitisho wa nguvu zaidi (wa iymaan zao).
وَإِذًا لَّآتَيْنَاهُم مِّن لَّدُنَّا أَجْرًا عَظِيمًا﴿٦٧﴾
67. Na hapo Tungeliwapa kutoka Kwetu ujira adhimu.
وَلَهَدَيْنَاهُمْ صِرَاطًا مُّسْتَقِيمًا﴿٦٨﴾
68. Na Tungewaongoza njia iliyonyooka.
وَمَن
يُطِعِ اللَّـهَ وَالرَّسُولَ فَأُولَـٰئِكَ مَعَ الَّذِينَ أَنْعَمَ
اللَّـهُ عَلَيْهِم مِّنَ النَّبِيِّينَ وَالصِّدِّيقِينَ وَالشُّهَدَاءِ
وَالصَّالِحِينَ ۚ وَحَسُنَ أُولَـٰئِكَ رَفِيقًا﴿٦٩﴾
69. Na atakayemtii Allaah na Rasuli, basi hao watakuwa pamoja na wale Allaah Aliowaneemesha miongoni mwa Manabii na asw-Swiddiqiyna na Mashuhadaa na Swalihina, na uzuri ulioje hao kuwa ni rafiki (zake).
ذَٰلِكَ الْفَضْلُ مِنَ اللَّـهِ ۚ وَكَفَىٰ بِاللَّـهِ عَلِيمًا﴿٧٠﴾
70. Hiyo ni fadhila kutoka kwa Allaah. Na inatosheleza Allaah kuwa ni ‘Aliymaa (Mjuzi wa yote).
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا خُذُوا حِذْرَكُمْ فَانفِرُوا ثُبَاتٍ أَوِ انفِرُوا جَمِيعًا﴿٧١﴾
71. Enyi mlioamini! Shikeni hadhari yenu; tokeni kwa vikosi vikosi au tokeni kwa pamoja.
وَإِنَّ
مِنكُمْ لَمَن لَّيُبَطِّئَنَّ فَإِنْ أَصَابَتْكُم مُّصِيبَةٌ قَالَ قَدْ
أَنْعَمَ اللَّـهُ عَلَيَّ إِذْ لَمْ أَكُن مَّعَهُمْ شَهِيدًا﴿٧٢﴾
72. Na hakika miongoni mwenu wako
wanaobakia nyuma (wakati wa kwenda vitani); inapokusibuni msiba husema:
“Kwa yakini Allaah Amenineemesha nilivyokuwa sikuhudhuria pamoja nao.”
وَلَئِنْ
أَصَابَكُمْ فَضْلٌ مِّنَ اللَّـهِ لَيَقُولَنَّ كَأَن لَّمْ تَكُن
بَيْنَكُمْ وَبَيْنَهُ مَوَدَّةٌ يَا لَيْتَنِي كُنتُ مَعَهُمْ فَأَفُوزَ
فَوْزًا عَظِيمًا﴿٧٣﴾
73. Na ikikufikieni fadhila kutoka kwa Allaah husema; kama kwamba hakukuwa baina yenu na yake pendo (husema): “Laiti ningelikuwa pamoja nao nikapata kufuzu mafanikio adhimu.”
فَلْيُقَاتِلْ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ الَّذِينَ يَشْرُونَ الْحَيَاةَ الدُّنْيَا بِالْآخِرَةِ ۚ وَمَن يُقَاتِلْ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ فَيُقْتَلْ أَوْ يَغْلِبْ فَسَوْفَ نُؤْتِيهِ أَجْرًا عَظِيمًا﴿٧٤﴾
74. Basi wapigane katika njia ya Allaah wale wanaouza
uhai (wao) wa dunia kwa Aakhirah. Na atakayepigana katika njia ya
Allaah akauliwa au akashinda basi Tutampa ujira adhimu.
وَمَا
لَكُمْ لَا تُقَاتِلُونَ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ وَالْمُسْتَضْعَفِينَ مِنَ
الرِّجَالِ وَالنِّسَاءِ وَالْوِلْدَانِ الَّذِينَ يَقُولُونَ رَبَّنَا
أَخْرِجْنَا مِنْ هَـٰذِهِ الْقَرْيَةِ الظَّالِمِ أَهْلُهَا وَاجْعَل
لَّنَا مِن لَّدُنكَ وَلِيًّا وَاجْعَل لَّنَا مِن لَّدُنكَ نَصِيرًا﴿٧٥﴾
75. Na mna nini (mpaka
mkawa) hampigani katika njia ya Allaah, na walio wanyonge kati ya
wanaume na wanawake na watoto ambao husema: “Rabb (Mola) wetu Tutoe kutoka katika mji huu ambao watu wake ni dhalimu, na Tujaalie kutoka Kwako mlinzi na Tujaalie kutoka Kwako mwenye kunusuru.
الَّذِينَ آمَنُوا يُقَاتِلُونَ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ ۖ وَالَّذِينَ كَفَرُوا يُقَاتِلُونَ فِي سَبِيلِ الطَّاغُوتِ فَقَاتِلُوا أَوْلِيَاءَ الشَّيْطَانِ ۖ إِنَّ كَيْدَ الشَّيْطَانِ كَانَ ضَعِيفًا﴿٧٦﴾
76. Wale walioamini hupigana katika njia ya Allaah. Na wale waliokufuru hupigana katika njia ya atw-twaaghuwt (uvukaji mipaka, ufisadi). Basi wapigeni marafiki wandani wa shaytwaan. Hakika hila za shaytwaan ni dhaifu.
أَلَمْ
تَرَ إِلَى الَّذِينَ قِيلَ لَهُمْ كُفُّوا أَيْدِيَكُمْ وَأَقِيمُوا
الصَّلَاةَ وَآتُوا الزَّكَاةَ فَلَمَّا كُتِبَ عَلَيْهِمُ الْقِتَالُ
إِذَا فَرِيقٌ مِّنْهُمْ يَخْشَوْنَ النَّاسَ كَخَشْيَةِ اللَّـهِ أَوْ
أَشَدَّ خَشْيَةً ۚ وَقَالُوا رَبَّنَا لِمَ كَتَبْتَ عَلَيْنَا الْقِتَالَ لَوْلَا أَخَّرْتَنَا إِلَىٰ أَجَلٍ قَرِيبٍ ۗ قُلْ مَتَاعُ الدُّنْيَا قَلِيلٌ وَالْآخِرَةُ خَيْرٌ لِّمَنِ اتَّقَىٰ وَلَا تُظْلَمُونَ فَتِيلًا﴿٧٧﴾
77. Je, huoni wale
walioambiwa: “Zuieni mikono yenu (msipigane) na simamisheni Swalaah na
toeni Zakaah.” Basi walipoandikiwa amri kupigana (vita), mara kundi
miongoni mwao linakhofu watu kama kumkhofu Allaah au khofu zaidi (ya
hiyo). Na husema: “Rabb
(Mola) wetu! Kwa nini Umetuamrisha kupigana? Lau Ungelituakhirishia
hadi muda kidogo hivi!” Sema: “Starehe za dunia ni chache; na Aakhirah
ni bora zaidi kwa mwenye kuwa na taqwa; wala hamtodhulumiwa fatiylaa (kadiri ya uzi katika kokwa ya tende).”
أَيْنَمَا تَكُونُوا يُدْرِككُّمُ الْمَوْتُ وَلَوْ كُنتُمْ فِي بُرُوجٍ مُّشَيَّدَةٍ ۗ وَإِن تُصِبْهُمْ حَسَنَةٌ يَقُولُوا هَـٰذِهِ مِنْ عِندِ اللَّـهِ ۖ وَإِن تُصِبْهُمْ سَيِّئَةٌ يَقُولُوا هَـٰذِهِ مِنْ عِندِكَ ۚ قُلْ كُلٌّ مِّنْ عِندِ اللَّـهِ ۖ فَمَالِ هَـٰؤُلَاءِ الْقَوْمِ لَا يَكَادُونَ يَفْقَهُونَ حَدِيثًا﴿٧٨﴾
78. Popote mtakapokuwa yatakufikieni
mauti, japo mkiwa katika minara ilojengwa kifakhari (na madhubuti). Na
likiwafikia (jambo) zuri husema: “Hili ni kutoka kwa Allaah.” Na
likiwasibu ovu husema: “Hili kutoka kwako (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم).” Sema: “Yote ni kutoka kwa Allaah.” Basi wana nini hawa watu hawakaribi kufahamu hadiyth (kauli)?
مَّا أَصَابَكَ مِنْ حَسَنَةٍ فَمِنَ اللَّـهِ ۖ وَمَا أَصَابَكَ مِن سَيِّئَةٍ فَمِن نَّفْسِكَ ۚ وَأَرْسَلْنَاكَ لِلنَّاسِ رَسُولًا ۚ وَكَفَىٰ بِاللَّـهِ شَهِيدًا﴿٧٩﴾
79. Zuri lilokufikia ni kutoka kwa Allaah. Na ubaya uliokusibu (ee bin-Aadam) ni kutokana na nafsi yako. Na Tumekutuma (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) kwa watu uwe Rasuli na inatosheleza Allaah kuwa ni Shahiydaa (Mwenye kushuhudia yote).
مَّن يُطِعِ الرَّسُولَ فَقَدْ أَطَاعَ اللَّـهَ ۖ وَمَن تَوَلَّىٰ فَمَا أَرْسَلْنَاكَ عَلَيْهِمْ حَفِيظًا﴿٨٠﴾
80. Atakayemtii Rasuli basi kwa yakini amemtii Allaah. Na atakayekengeuka basi Hatukukutuma kuwa mlinzi juu yao.
وَيَقُولُونَ طَاعَةٌ فَإِذَا بَرَزُوا مِنْ عِندِكَ بَيَّتَ طَائِفَةٌ مِّنْهُمْ غَيْرَ الَّذِي تَقُولُ ۖ وَاللَّـهُ يَكْتُبُ مَا يُبَيِّتُونَ ۖ فَأَعْرِضْ عَنْهُمْ وَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّـهِ ۚ وَكَفَىٰ بِاللَّـهِ وَكِيلًا﴿٨١﴾
81. Na husema: “Tunatii.”
Lakini wanapotoka kutoka kwako, kundi miongoni mwao hukesha kushauriana
kinyume na unayoyasema. Na Allaah Anayaandika yale wanayokeshea. Basi
waachilie mbali na tawakali kwa Allaah. Na inatosheleza Allaah kuwa Wakiylaa (Mdhamini Anayetegemewa kwa yote).
أَفَلَا يَتَدَبَّرُونَ الْقُرْآنَ ۚ وَلَوْ كَانَ مِنْ عِندِ غَيْرِ اللَّـهِ لَوَجَدُوا فِيهِ اخْتِلَافًا كَثِيرًا﴿٨٢﴾
82. Je hawaizingatii Qur-aan? Na lau
ingelikuwa imetoka kwa ghairi ya Allaah, bila shaka wangelikuta ndani
yake khitilafu nyingi.
وَإِذَا جَاءَهُمْ أَمْرٌ مِّنَ الْأَمْنِ أَوِ الْخَوْفِ أَذَاعُوا بِهِ ۖ وَلَوْ رَدُّوهُ إِلَى الرَّسُولِ وَإِلَىٰ أُولِي الْأَمْرِ مِنْهُمْ لَعَلِمَهُ الَّذِينَ يَسْتَنبِطُونَهُ مِنْهُمْ ۗ وَلَوْلَا فَضْلُ اللَّـهِ عَلَيْكُمْ وَرَحْمَتُهُ لَاتَّبَعْتُمُ الشَّيْطَانَ إِلَّا قَلِيلًا﴿٨٣﴾
83. Na linapowafikia jambo lolote la amani au la khofu hulitangaza. Na lau wangelirudisha kwa Rasuli
na kwa wenye madaraka kati yao, wale (Wanavyuoni) wanaotafiti miongoni
mwao wangelilijua. Na lau si fadhila ya Allaah juu yenu na Rahmah Yake kwa yakini mngelimfuata shaytwaan (nyote) ila wachache tu.
فَقَاتِلْ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ لَا تُكَلَّفُ إِلَّا نَفْسَكَ ۚ وَحَرِّضِ الْمُؤْمِنِينَ ۖ عَسَى اللَّـهُ أَن يَكُفَّ بَأْسَ الَّذِينَ كَفَرُوا ۚ وَاللَّـهُ أَشَدُّ بَأْسًا وَأَشَدُّ تَنكِيلًا﴿٨٤﴾
84. Basi pigana (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) katika njia ya Allaah, hukalifishwi ila nafsi yako. Na wahimize Waumini (wakuunge). Huenda Allaah Akazuia mashambulizi ya nguvu ya waliokufuru. Na Allaah ni Mkali zaidi wa kushambulia na Mkali zaidi wa kuadhibu (adhabu ya funzo).
مَّن يَشْفَعْ شَفَاعَةً حَسَنَةً يَكُن لَّهُ نَصِيبٌ مِّنْهَا ۖ وَمَن يَشْفَعْ شَفَاعَةً سَيِّئَةً يَكُن لَّهُ كِفْلٌ مِّنْهَا ۗ وَكَانَ اللَّـهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ مُّقِيتًا﴿٨٥﴾
85. Atakayeombea shafaa’ah (uombezi wa aina yoyote ule) nzuri atapata fungu lake (la thawabu) katika hayo. Na atakayeombea shafaa’ah mbaya atapata sehemu (ya dhambi) katika hayo. Na Allaah daima juu ya kila kitu ni Muqiytaa (Mwenye kudhitibi, Mwangalizi wa kila kitu).
وَإِذَا حُيِّيتُم بِتَحِيَّةٍ فَحَيُّوا بِأَحْسَنَ مِنْهَا أَوْ رُدُّوهَا ۗ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ حَسِيبًا﴿٨٦﴾
86. Na mtapoamkiwa kwa maamkizi yoyote, basi itikieni kwa yaliyo mazuri zaidi kuliko hayo au yarudisheni hayo hayo (kama mlivyoamkiwa). Hakika Allaah daima juu ya kila kitu ni Hasiybaa (Mwenye kuhesabu, kutosheleza).
اللَّـهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ ۚ لَيَجْمَعَنَّكُمْ إِلَىٰ يَوْمِ الْقِيَامَةِ لَا رَيْبَ فِيهِ ۗ وَمَنْ أَصْدَقُ مِنَ اللَّـهِ حَدِيثًا﴿٨٧﴾
87. Allaahu hapana ilaaha (muabudiwa wa haki) ila Yeye. Bila ya shaka Atakukusanyeni Siku ya Qiyaamah haina shaka ndani yake. Na nani mkweli zaidi katika hadiythaa (maneno) kuliko Allaah?
فَمَا لَكُمْ فِي الْمُنَافِقِينَ فِئَتَيْنِ وَاللَّـهُ أَرْكَسَهُم بِمَا كَسَبُوا ۚ أَتُرِيدُونَ أَن تَهْدُوا مَنْ أَضَلَّ اللَّـهُ ۖ وَمَن يُضْلِلِ اللَّـهُ فَلَن تَجِدَ لَهُ سَبِيلًا﴿٨٨﴾
88. Basi mna nini (hata) mkawa makundi mawili kuhusu wanafiki; na Allaah Amewageuza (warudie ukafiri au maovu) kwa sababu waliyoyachuma. Je, mnataka kumwongoa ambaye Allaah Amempotoa? Na aliyepotozwa na Allaah basi hutompatia kamwe njia (ya kumwongoa).
وَدُّوا لَوْ تَكْفُرُونَ كَمَا كَفَرُوا فَتَكُونُونَ سَوَاءً ۖ فَلَا تَتَّخِذُوا مِنْهُمْ أَوْلِيَاءَ حَتَّىٰ يُهَاجِرُوا فِي سَبِيلِ اللَّـهِ ۚ فَإِن تَوَلَّوْا فَخُذُوهُمْ وَاقْتُلُوهُمْ حَيْثُ وَجَدتُّمُوهُمْ ۖ وَلَا تَتَّخِذُوا مِنْهُمْ وَلِيًّا وَلَا نَصِيرًا﴿٨٩﴾
89. Wanatamani kama mtakufuru kama walivyokufuru wao, ili muwe
sawa sawa. Basi msifanye miongoni mwao marafiki wandani na ushirikiano
mpaka wahajiri katika njia ya Allaah. Wakikengeuka basi wakamateni na
waueni popote muwapatapo. Wala misfanye miongoni mwao marafiki wandani
na ushirikiano wala mwenye kunusuru.
إِلَّا الَّذِينَ يَصِلُونَ إِلَىٰ قَوْمٍ بَيْنَكُمْ وَبَيْنَهُم مِّيثَاقٌ أَوْ جَاءُوكُمْ حَصِرَتْ صُدُورُهُمْ أَن يُقَاتِلُوكُمْ أَوْ يُقَاتِلُوا قَوْمَهُمْ ۚ وَلَوْ شَاءَ اللَّـهُ لَسَلَّطَهُمْ عَلَيْكُمْ فَلَقَاتَلُوكُمْ ۚ فَإِنِ اعْتَزَلُوكُمْ فَلَمْ يُقَاتِلُوكُمْ وَأَلْقَوْا إِلَيْكُمُ السَّلَمَ فَمَا جَعَلَ اللَّـهُ لَكُمْ عَلَيْهِمْ سَبِيلًا﴿٩٠﴾
90. Isipokuwa wale waliochukua
kimbilio kwa watu ambao baina yenu na baina yao mna mkataba au
wamekujieni vifua vyao vimedhikika kupigana nanyi au kupigana na watu
wao, (hao msiwapige). Na lau Allaah Angelitaka, Angeliwasaliti juu yenu,
wakapigana nanyi. Basi wakijitenga nanyi na wasipigane nanyi, na
wakakuwekeeni amani, basi Allaah Hakukufanyieni njia juu yao (ya
kuwapiga vita).
سَتَجِدُونَ آخَرِينَ يُرِيدُونَ أَن يَأْمَنُوكُمْ وَيَأْمَنُوا قَوْمَهُمْ كُلَّ مَا رُدُّوا إِلَى الْفِتْنَةِ أُرْكِسُوا فِيهَا ۚ
فَإِن لَّمْ يَعْتَزِلُوكُمْ وَيُلْقُوا إِلَيْكُمُ السَّلَمَ وَيَكُفُّوا
أَيْدِيَهُمْ فَخُذُوهُمْ وَاقْتُلُوهُمْ حَيْثُ ثَقِفْتُمُوهُمْ ۚ وَأُولَـٰئِكُمْ جَعَلْنَا لَكُمْ عَلَيْهِمْ سُلْطَانًا مُّبِينًا﴿٩١﴾
91. Mtawakuta wengine wanaotaka kupata amani kwenu na kupata amani kwa watu wao; kila wanaporudishwa katika fitnah
(kushawishiwa ukafiri na unafiki wao) huangushwa humo. Wasipojitenga
nanyi na wakakuleteeni amani na wakazuia mikono yao (kukupigeni), basi
wachukuweni na wauweni popote muwapatapo. Na hao Tumekufanyieni dhidi
yao hoja zilizo bayana (ya kujuzu kupigana nao).
وَمَا كَانَ لِمُؤْمِنٍ أَن يَقْتُلَ مُؤْمِنًا إِلَّا خَطَأً ۚ وَمَن قَتَلَ مُؤْمِنًا خَطَأً فَتَحْرِيرُ رَقَبَةٍ مُّؤْمِنَةٍ وَدِيَةٌ مُّسَلَّمَةٌ إِلَىٰ أَهْلِهِ إِلَّا أَن يَصَّدَّقُوا ۚ فَإِن كَانَ مِن قَوْمٍ عَدُوٍّ لَّكُمْ وَهُوَ مُؤْمِنٌ فَتَحْرِيرُ رَقَبَةٍ مُّؤْمِنَةٍ ۖ وَإِن كَانَ مِن قَوْمٍ بَيْنَكُمْ وَبَيْنَهُم مِّيثَاقٌ فَدِيَةٌ مُّسَلَّمَةٌ إِلَىٰ أَهْلِهِ وَتَحْرِيرُ رَقَبَةٍ مُّؤْمِنَةٍ ۖ فَمَن لَّمْ يَجِدْ فَصِيَامُ شَهْرَيْنِ مُتَتَابِعَيْنِ تَوْبَةً مِّنَ اللَّـهِ ۗ وَكَانَ اللَّـهُ عَلِيمًا حَكِيمًا﴿٩٢﴾
92. Na haiwi kwa Muumin amuue Muumin
ila kwa kukosea tu. Na atakayemuua Muumin kwa kukosea basi aachilie huru
mtumwa Muumin na atoe diya kwa kuifikisha kwa watu wake (ahli wa maiti)
isipokuwa watolee swadaqah (wasamehe haki yao). Na ikiwa ni miongoni
mwa watu wa maadui zenu naye ni Muumin, basi (aliyeua) aachilie huru
mtumwa Muumin. Na ikiwa ni miongoni mwa watu ambao kuna mkataba baina
yenu na baina yao; basi wapewe diya kuifikisha kwa watu wake na
aachiliwe huru mtumwa Muumin. Asiyepata (au asiyekuwa na uwezo), afunge Swiyaam (badala yake) miezi miwili mfululizo; kuwa ni tawbah kwa Allaah. Na Allaah daima ni ‘Aliyman Hakiymaa (Mjuzi wa yote – Mwenye hikmah wa yote).
وَمَن
يَقْتُلْ مُؤْمِنًا مُّتَعَمِّدًا فَجَزَاؤُهُ جَهَنَّمُ خَالِدًا فِيهَا
وَغَضِبَ اللَّـهُ عَلَيْهِ وَلَعَنَهُ وَأَعَدَّ لَهُ عَذَابًا عَظِيمًا﴿٩٣﴾
93. Na atakayemuua Muumini kwa kusudi, basi jazaa yake ni (Moto wa) Jahannam, ni mwenye kudumu humo na Allaah Atamghadhibikia na Atamlaani na Atamuandalia adhabu kuu.
يَا
أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا ضَرَبْتُمْ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ
فَتَبَيَّنُوا وَلَا تَقُولُوا لِمَنْ أَلْقَىٰ إِلَيْكُمُ السَّلَامَ
لَسْتَ مُؤْمِنًا تَبْتَغُونَ عَرَضَ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا فَعِندَ
اللَّـهِ مَغَانِمُ كَثِيرَةٌ ۚ كَذَٰلِكَ كُنتُم مِّن قَبْلُ فَمَنَّ اللَّـهُ عَلَيْكُمْ فَتَبَيَّنُوا ۚ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ بِمَا تَعْمَلُونَ خَبِيرًا﴿٩٤﴾
94. Enyi mlioamini! Mnaposafiri
(kupigana jihaad) katika njia ya Allaah thibitisheni Wala msimwambie
anayekutoleeni (maamkizi ya) salamu (kwamba): “Wewe si Muumin”
kwakutamani mafao yapitayo ya uhai wa dunia na hali kwa Allaah kuna
ghanima nyingi. Hivyo ndivyo mlivyokuwa kabla na Allaah Akakufanyieni
ihsaan basi hakikisheni. Hakika Allaah daima kwa myatendayo ni Khabiyraa (Mjuzi wa yaliyodhahiri na yaliyofichikana).
لَّا
يَسْتَوِي الْقَاعِدُونَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ غَيْرُ أُولِي الضَّرَرِ
وَالْمُجَاهِدُونَ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ بِأَمْوَالِهِمْ وَأَنفُسِهِمْ ۚ فَضَّلَ اللَّـهُ الْمُجَاهِدِينَ بِأَمْوَالِهِمْ وَأَنفُسِهِمْ عَلَى الْقَاعِدِينَ دَرَجَةً ۚ وَكُلًّا وَعَدَ اللَّـهُ الْحُسْنَىٰ ۚ وَفَضَّلَ اللَّـهُ الْمُجَاهِدِينَ عَلَى الْقَاعِدِينَ أَجْرًا عَظِيمًا﴿٩٥﴾
95. Hawawi sawa kati ya Waumini wanaokaa (nyumbani kutokwenda vitani) wasiokuwa na dharura na Mujaahiduwna katika njia ya Allaah kwa mali zao na nafsi zao. Allaah Amewafadhilisha kwa cheo Mujaahidiyna kwa mali zao na nafsi zao kuliko waliokaaa nyuma. Na wote Allaah Amewaahidi Al-Husnaa (thawabu na Jannah). Na Allaah Amewafadhilisha Mujaahidiyna kwa ujira adhimu kuliko wanaokaa (nyuma).
دَرَجَاتٍ مِّنْهُ وَمَغْفِرَةً وَرَحْمَةً ۚ وَكَانَ اللَّـهُ غَفُورًا رَّحِيمًا﴿٩٦﴾
96. Ni vyeo (vya juu kabisa) kutoka Kwake na maghfirah na Rahmah. Na Allaah daima ni Ghafuwrar-Rahiymaa (Mwingi wa kughufuria – Mwenye kurehemu).
إِنَّ الَّذِينَ تَوَفَّاهُمُ الْمَلَائِكَةُ ظَالِمِي أَنفُسِهِمْ قَالُوا فِيمَ كُنتُمْ ۖ قَالُوا كُنَّا مُسْتَضْعَفِينَ فِي الْأَرْضِ ۚ قَالُوا أَلَمْ تَكُنْ أَرْضُ اللَّـهِ وَاسِعَةً فَتُهَاجِرُوا فِيهَا ۚ فَأُولَـٰئِكَ مَأْوَاهُمْ جَهَنَّمُ ۖ وَسَاءَتْ مَصِيرًا﴿٩٧﴾
97. Hakika wale ambao Malaika
wamewafisha, hali wamejidhulumu nafsi zao; (Malaika) watawaambia:
“Mlikuwa katika hali gani?” Watasema: “Tulikuwa tukikandamizwa katika
ardhi.” (Malaika) Watasema: “Je, kwani ardhi ya Allaah haikuwa ya wasaa
mkahajiri? Basi hao makazi yao yatakuwa ni (Moto wa) Jahannam, na uovu ulioje mahali pa kuishia.
إِلَّا الْمُسْتَضْعَفِينَ مِنَ الرِّجَالِ وَالنِّسَاءِ وَالْوِلْدَانِ لَا يَسْتَطِيعُونَ حِيلَةً وَلَا يَهْتَدُونَ سَبِيلًا﴿٩٨﴾
98. Isipokuwa wale waliokandamizwa
kati ya wanaume na wanawake na watoto ambao hawakuweza kupata (mpango
wa) hila yoyote wala hawawezi kuongoza njia.
فَأُولَـٰئِكَ عَسَى اللَّـهُ أَن يَعْفُوَ عَنْهُمْ ۚ وَكَانَ اللَّـهُ عَفُوًّا غَفُورًا﴿٩٩﴾
99. Basi hao huenda Allaah Akawasamehe. Na Allaah daima ni ‘Afuwwan-Ghafuwraa (Mwingi wa kusamehe - Mwingi wa kughufuria).
وَمَن يُهَاجِرْ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ يَجِدْ فِي الْأَرْضِ مُرَاغَمًا كَثِيرًا وَسَعَةً ۚ
وَمَن يَخْرُجْ مِن بَيْتِهِ مُهَاجِرًا إِلَى اللَّـهِ وَرَسُولِهِ ثُمَّ
يُدْرِكْهُ الْمَوْتُ فَقَدْ وَقَعَ أَجْرُهُ عَلَى اللَّـهِ ۗ وَكَانَ اللَّـهُ غَفُورًا رَّحِيمًا﴿١٠٠﴾
100. Na anayehajiri katika njia ya
Allaah atapata katika ardhi mahali pengi pa kukimbilia na wasaa. Na
atakayetoka nyumbani kwake akiwa ni mwenye kuhajiri kwa ajili ya Allaah
na Rasuli Wake, kisha mauti yakamfikia, basi ujira wake umehakikika kwa
Allaah. Na Allaah daima ni Ghafuwrar-Rahiymaa (Mwingi wa kughufuria – Mwenye kurehemu).
وَإِذَا
ضَرَبْتُمْ فِي الْأَرْضِ فَلَيْسَ عَلَيْكُمْ جُنَاحٌ أَن تَقْصُرُوا
مِنَ الصَّلَاةِ إِنْ خِفْتُمْ أَن يَفْتِنَكُمُ الَّذِينَ كَفَرُوا ۚ إِنَّ الْكَافِرِينَ كَانُوا لَكُمْ عَدُوًّا مُّبِينًا﴿١٠١﴾
101. Na mtakaposafiri katika ardhi
basi si dhambi kwenu kufupisha Swalaah mkikhofu kwamba waliokufuru
watakufitinisheni. Hakika makafiri wamekuwa kwenu ni maadui dhahiri.
وَإِذَا
كُنتَ فِيهِمْ فَأَقَمْتَ لَهُمُ الصَّلَاةَ فَلْتَقُمْ طَائِفَةٌ
مِّنْهُم مَّعَكَ وَلْيَأْخُذُوا أَسْلِحَتَهُمْ فَإِذَا سَجَدُوا
فَلْيَكُونُوا مِن وَرَائِكُمْ وَلْتَأْتِ طَائِفَةٌ أُخْرَىٰ لَمْ
يُصَلُّوا فَلْيُصَلُّوا مَعَكَ وَلْيَأْخُذُوا حِذْرَهُمْ
وَأَسْلِحَتَهُمْ ۗ وَدَّ الَّذِينَ كَفَرُوا لَوْ تَغْفُلُونَ عَنْ أَسْلِحَتِكُمْ وَأَمْتِعَتِكُمْ فَيَمِيلُونَ عَلَيْكُم مَّيْلَةً وَاحِدَةً ۚ وَلَا جُنَاحَ عَلَيْكُمْ إِن كَانَ بِكُمْ أَذًى مِّن مَّطَرٍ أَوْ كُنتُم مَّرْضَىٰ أَن تَضَعُوا أَسْلِحَتَكُمْ ۖ وَخُذُوا حِذْرَكُمْ ۗ إِنَّ اللَّـهَ أَعَدَّ لِلْكَافِرِينَ عَذَابًا مُّهِينًا﴿١٠٢﴾
102. Na utapokuwa upo kati yao,
ukawaswalisha, basi lisimame kundi miongoni mwao pamoja nawe, na
wachukue silaha zao. Watakaposujudu basi wawe nyuma yenu (kuwalinda). Na
lije kundi jengine ambalo halikuswali, liswali pamoja nawe, nao washike
hadhari na silaha zao. Wale waliokufuru wanatamani kama mtaghafilika na
silaha zenu na vifaa vyenu wakuvamieni mvamio mmoja. Na wala si dhambi
kwenu ikiwa mna maudhiko kutokana na mvua au mkiwa wagonjwa kuweka
(chini) silaha zenu. Na mshike hadhari zenu. Hakika Allaah Amewaandalia
makafiri adhabu ya kudhalilisha.
فَإِذَا قَضَيْتُمُ الصَّلَاةَ فَاذْكُرُوا اللَّـهَ قِيَامًا وَقُعُودًا وَعَلَىٰ جُنُوبِكُمْ ۚ فَإِذَا اطْمَأْنَنتُمْ فَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ ۚ إِنَّ الصَّلَاةَ كَانَتْ عَلَى الْمُؤْمِنِينَ كِتَابًا مَّوْقُوتًا﴿١٠٣﴾
103. Mtakapomaliza Swalaah, mdhukuruni
Allaah msimamapo, na mkaapo na (mnapojinyosha) ubavuni mwenu
Mtakapopata utulivu, simamisheni Swalaah (kama desturi bila ya
kuzifupisha). Hakika Swalaah kwa Waumini ni fardhi iliyowekwa nyakati
maalumu.
وَلَا تَهِنُوا فِي ابْتِغَاءِ الْقَوْمِ ۖ إِن تَكُونُوا تَأْلَمُونَ فَإِنَّهُمْ يَأْلَمُونَ كَمَا تَأْلَمُونَ ۖ وَتَرْجُونَ مِنَ اللَّـهِ مَا لَا يَرْجُونَ ۗ وَكَانَ اللَّـهُ عَلِيمًا حَكِيمًا﴿١٠٤﴾
104. Wala msilegee kuwaandama watu
(walio maadui). Mkiwa mnaumia (kwa majeraha, tabu n.k) basi nao (pia)
wanaumia kama mnavyoumia. Na mnataraji kutoka kwa Allaah wasiyoyataraji
wao. Na Allaah daima ni ‘Aliyman-Hakiymaa (Mjuzi wa yote – Mwenye hikmah wa yote).
إِنَّا أَنزَلْنَا إِلَيْكَ الْكِتَابَ بِالْحَقِّ لِتَحْكُمَ بَيْنَ النَّاسِ بِمَا أَرَاكَ اللَّـهُ ۚ وَلَا تَكُن لِّلْخَائِنِينَ خَصِيمًا﴿١٠٥﴾
105. Hakika Sisi Tumekuteremshia (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) Kitabu kwa haki ili uhukumu baina ya watu kwa Aliyokuonyesha Allaah. Wala usiwe mtetezi kwa makhaini.
وَاسْتَغْفِرِ اللَّـهَ ۖ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ غَفُورًا رَّحِيمًا﴿١٠٦﴾
106. Na muombe Allaah maghfirah. Hakika Allaah daima ni Ghafuwrar-Rahiymaa (Mwingi wa kughufuria – Mwenye kurehemu).
وَلَا تُجَادِلْ عَنِ الَّذِينَ يَخْتَانُونَ أَنفُسَهُمْ ۚ إِنَّ اللَّـهَ لَا يُحِبُّ مَن كَانَ خَوَّانًا أَثِيمًا﴿١٠٧﴾
107. Wala usiwatetee wale wanaokhini nafsi zao. Hakika Allaah Hampendi aliye mwingi wa kukhini na kutenda dhambi.
يَسْتَخْفُونَ مِنَ النَّاسِ وَلَا يَسْتَخْفُونَ مِنَ اللَّـهِ وَهُوَ مَعَهُمْ إِذْ يُبَيِّتُونَ مَا لَا يَرْضَىٰ مِنَ الْقَوْلِ ۚ وَكَانَ اللَّـهُ بِمَا يَعْمَلُونَ مُحِيطًا﴿١٠٨﴾
108. Wanaficha kwa watu (niyyah
mbaya zao na maouvu) na wala hawawezi kuficha kwa Allaah, Naye Yu
pamoja nao (kwa ujuzi Wake) pale wanapokesha kupanga njama kwa zile
kauli Asizozikubali. Na Allaah daima kwa wayatendayo ni Muhiytwaa (Mwenye kuzunguka vyote kwa ujuzi).
هَا
أَنتُمْ هَـٰؤُلَاءِ جَادَلْتُمْ عَنْهُمْ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا
فَمَن يُجَادِلُ اللَّـهَ عَنْهُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ أَم مَّن يَكُونُ
عَلَيْهِمْ وَكِيلًا﴿١٠٩﴾
109. Ha! Nyinyi ndio hawa
mliowatetea katika uhai wa dunia. Basi nani atakayemjadili Allaah kwa
ajili yao Siku ya Qiyaamah au nani atakayekuwa mwakilishi wao?
وَمَن يَعْمَلْ سُوءًا أَوْ يَظْلِمْ نَفْسَهُ ثُمَّ يَسْتَغْفِرِ اللَّـهَ يَجِدِ اللَّـهَ غَفُورًا رَّحِيمًا﴿١١٠﴾
110. Na atakayetenda ovu au akajidhulumu nafsi yake; kisha akamwomba Allaah maghfirah; atamkuta Allaah ni Ghafuwrar-Rahiymaa (Mwingi wa kughufuria – Mwenye kurehemu).
وَمَن يَكْسِبْ إِثْمًا فَإِنَّمَا يَكْسِبُهُ عَلَىٰ نَفْسِهِ ۚ وَكَانَ اللَّـهُ عَلِيمًا حَكِيمًا﴿١١١﴾
111. Na atakayechuma dhambi, basi hakika anaichumia nafsi yake. Na Allaah daima ni ‘Aliyman Hakiymaa (Mjuzi wa yote – Mwenye hikmah wa yote).
وَمَن يَكْسِبْ خَطِيئَةً أَوْ إِثْمًا ثُمَّ يَرْمِ بِهِ بَرِيئًا فَقَدِ احْتَمَلَ بُهْتَانًا وَإِثْمًا مُّبِينًا﴿١١٢﴾
112. Na atakayechuma kosa au dhambi kisha akamtupia asiye na hatia; basi kwa yakini atajitweka buhtaan (usingiziaji wa dhulma) na dhambi zilizo bayana.
وَلَوْلَا فَضْلُ اللَّـهِ عَلَيْكَ وَرَحْمَتُهُ لَهَمَّت طَّائِفَةٌ مِّنْهُمْ أَن يُضِلُّوكَ وَمَا يُضِلُّونَ إِلَّا أَنفُسَهُمْ ۖ وَمَا يَضُرُّونَكَ مِن شَيْءٍ ۚ وَأَنزَلَ اللَّـهُ عَلَيْكَ الْكِتَابَ وَالْحِكْمَةَ وَعَلَّمَكَ مَا لَمْ تَكُن تَعْلَمُ ۚ وَكَانَ فَضْلُ اللَّـهِ عَلَيْكَ عَظِيمًا﴿١١٣﴾
113. Na lau kuwa si fadhila ya Allaah na Rahmah Yake juu yako (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم);
bila shaka kundi miongoni mwao lingefanya hima (kudhamiria) kukupoteza.
Na hawazipotezi ila nafsi zao, na hawakudhuru kwa chochote. Na Allaah
Amekuteremshia Kitabu na Hikmah na Akakufunza yale ambayo hukuwa
unayajua. Na fadhila za Allaah juu yako ni adhimu.
لَّا خَيْرَ فِي كَثِيرٍ مِّن نَّجْوَاهُمْ إِلَّا مَنْ أَمَرَ بِصَدَقَةٍ أَوْ مَعْرُوفٍ أَوْ إِصْلَاحٍ بَيْنَ النَّاسِ ۚ وَمَن يَفْعَلْ ذَٰلِكَ ابْتِغَاءَ مَرْضَاتِ اللَّـهِ فَسَوْفَ نُؤْتِيهِ أَجْرًا عَظِيمًا﴿١١٤﴾
114. Hakuna kheri katika minong’ono yao mingi isipokuwa anayeamrisha swadaqah, au (kuamrisha) ma’-ruwf (mema), au kupatanisha baina ya watu. Na atakayefanya hivyo kutaka Radhi za Allaah, basi Tutampa ujira adhimu.
وَمَن
يُشَاقِقِ الرَّسُولَ مِن بَعْدِ مَا تَبَيَّنَ لَهُ الْهُدَىٰ
وَيَتَّبِعْ غَيْرَ سَبِيلِ الْمُؤْمِنِينَ نُوَلِّهِ مَا تَوَلَّىٰ
وَنُصْلِهِ جَهَنَّمَ ۖ وَسَاءَتْ مَصِيرًا﴿١١٥﴾
115. Na atakayempinga
Rasuli baada ya kuwa imeshambainikia Uongofu na akaifuata njia
isiyokuwa ya Waumini; Tutamgeuza alikogeukia (mwenyewe upotofuni) na
Tutamuingiza (Moto wa) Jahannam. Na uovu ulioje mahali pa kuishia.
إِنَّ اللَّـهَ لَا يَغْفِرُ أَن يُشْرَكَ بِهِ وَيَغْفِرُ مَا دُونَ ذَٰلِكَ لِمَن يَشَاءُ ۚ وَمَن يُشْرِكْ بِاللَّـهِ فَقَدْ ضَلَّ ضَلَالًا بَعِيدًا﴿١١٦﴾
116. Hakika
Allaah Haghufuri kushirikishwa; lakini Anaghufuria yasiyokuwa hayo kwa
Amtakae. Na yeyote atakayemshirikisha Allaah basi kwa yakini amepotoka upotofu wa mbali.
إِن يَدْعُونَ مِن دُونِهِ إِلَّا إِنَاثًا وَإِن يَدْعُونَ إِلَّا شَيْطَانًا مَّرِيدًا﴿١١٧﴾
117. Hawaombi badala Yake isipokuwa (miungu ya) kike na hawaombi (hakika) isipokuwa shaytwaan muasi.
لَّعَنَهُ اللَّـهُ ۘ وَقَالَ لَأَتَّخِذَنَّ مِنْ عِبَادِكَ نَصِيبًا مَّفْرُوضًا﴿١١٨﴾
118. Allaah Amemlaani. Na (shaytwaan) akasema: “Kwa hakika nitashika katika waja Wako sehemu maalumu.
وَلَأُضِلَّنَّهُمْ
وَلَأُمَنِّيَنَّهُمْ وَلَآمُرَنَّهُمْ فَلَيُبَتِّكُنَّ آذَانَ
الْأَنْعَامِ وَلَآمُرَنَّهُمْ فَلَيُغَيِّرُنَّ خَلْقَ اللَّـهِ ۚ وَمَن يَتَّخِذِ الشَّيْطَانَ وَلِيًّا مِّن دُونِ اللَّـهِ فَقَدْ خَسِرَ خُسْرَانًا مُّبِينًا﴿١١٩﴾
119. Na hakika nitawapoteza, na nitawashawishi matamanio (ya dhambi) na
nitawaamrisha. Basi watakata masikio ya wanyama (wawafanye kuwa hao ni
wanyama watukufu), na nitawaamrisha watabadili maumbile ya Allaah. Na
atakayemfanya shaytwaan kuwa rafiki mwandani na mlinzi badala ya Allaah basi kwa yakini amekhasirika khasara bayana.
يَعِدُهُمْ وَيُمَنِّيهِمْ ۖ وَمَا يَعِدُهُمُ الشَّيْطَانُ إِلَّا غُرُورًا﴿١٢٠﴾
120. Anawaahidi na anawashawishi matamanio ya uongo. Na shaytwaan hawaahidi isipokuwa ghururi (udanganyifu).
أُولَـٰئِكَ مَأْوَاهُمْ جَهَنَّمُ وَلَا يَجِدُونَ عَنْهَا مَحِيصًا﴿١٢١﴾
121. Hao makaazi yao ni (Moto wa) Jahannam, na wala hawatopata makimbilio ya kutoka humo.
وَالَّذِينَ
آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ سَنُدْخِلُهُمْ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن
تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا أَبَدًا ۖ وَعْدَ اللَّـهِ حَقًّا ۚ وَمَنْ أَصْدَقُ مِنَ اللَّـهِ قِيلًا﴿١٢٢﴾
122. Na wale walioamini na wakatenda mema Tutawaingiza Jannaat
zipitazo chini yake mito, ni wenye kudumu humo abadi. Ahadi ya Allaah
ni haki. Na nani aliye mkweli zaidi kwa kauli kuliko Allaah?
لَّيْسَ بِأَمَانِيِّكُمْ وَلَا أَمَانِيِّ أَهْلِ الْكِتَابِ ۗ مَن يَعْمَلْ سُوءًا يُجْزَ بِهِ وَلَا يَجِدْ لَهُ مِن دُونِ اللَّـهِ وَلِيًّا وَلَا نَصِيرًا﴿١٢٣﴾
123. “(Kuipata Jannah) Si kwa matamanio yenu wala si (kwa) matamanio ya Ahlil-Kitaab. Atakayefanya uovu atalipwa kwayo, na wala hatapata pasi na Allaah mlinzi wala mwenye kunusuru.
وَمَن
يَعْمَلْ مِنَ الصَّالِحَاتِ مِن ذَكَرٍ أَوْ أُنثَىٰ وَهُوَ مُؤْمِنٌ
فَأُولَـٰئِكَ يَدْخُلُونَ الْجَنَّةَ وَلَا يُظْلَمُونَ نَقِيرًا﴿١٢٤﴾
124. Na atakayefanya mema akiwa
mwanamume au mwanamke hali yeye ni Muumin; basi hao wataingia Jannah na
wala hawatodhulumiwa watu naqiyraa (kadiri ya kitone cha kokwa ya tende).
وَمَنْ أَحْسَنُ دِينًا مِّمَّنْ أَسْلَمَ وَجْهَهُ لِلَّـهِ وَهُوَ مُحْسِنٌ وَاتَّبَعَ مِلَّةَ إِبْرَاهِيمَ حَنِيفًا ۗ وَاتَّخَذَ اللَّـهُ إِبْرَاهِيمَ خَلِيلًا﴿١٢٥﴾
125. Na nani aliye bora zaidi kwa Dini kuliko yule aliyesjisalimisha kwa Allaah naye ni mtendaji mazuri na akafuata millah ya Ibraahiym haniyfaa (aliyejiengua na upotofu akaelemea Dini ya haki). Na Allaah Amemchukua Ibraahiym kuwa ni khaliylaa (kipenzi).
وَلِلَّـهِ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ ۚ وَكَانَ اللَّـهُ بِكُلِّ شَيْءٍ مُّحِيطًا﴿١٢٦﴾
126. Na ni vya Allaah Pekee vilivyomo katika mbingu na katika ardhi. Na Allaah daima kwa kila kitu ni Muhiytwaa (Mwenye kuzunguka vyote kwa ujuzi).
وَيَسْتَفْتُونَكَ فِي النِّسَاءِ ۖ
قُلِ اللَّـهُ يُفْتِيكُمْ فِيهِنَّ وَمَا يُتْلَىٰ عَلَيْكُمْ فِي
الْكِتَابِ فِي يَتَامَى النِّسَاءِ اللَّاتِي لَا تُؤْتُونَهُنَّ مَا
كُتِبَ لَهُنَّ وَتَرْغَبُونَ أَن تَنكِحُوهُنَّ وَالْمُسْتَضْعَفِينَ مِنَ
الْوِلْدَانِ وَأَن تَقُومُوا لِلْيَتَامَىٰ بِالْقِسْطِ ۚ وَمَا تَفْعَلُوا مِنْ خَيْرٍ فَإِنَّ اللَّـهَ كَانَ بِهِ عَلِيمًا﴿١٢٧﴾
127. Na wanatafuta kwako (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) fatwa kuhusu wanawake. Sema: “Allaah Atakupeni hukmu kuhusu wao na yale mnayosomewa kwenu katika Kitabu kuhusu mayatima wanawake ambao hamuwapi (mahari yao) waliyoandikiwa; na mna raghba ya kuwaoa. Na juu ya wanaokandamizwa miongoni mwa watoto. Na kwamba muwasimamie mayatima kwa uadilifu. Na lolote mlifanyalo katika la kheri basi hakika Allaah daima kwa hilo ni ‘Aliymaa (Mjuzi).
وَإِنِ امْرَأَةٌ خَافَتْ مِن بَعْلِهَا نُشُوزًا أَوْ إِعْرَاضًا فَلَا جُنَاحَ عَلَيْهِمَا أَن يُصْلِحَا بَيْنَهُمَا صُلْحًا ۚ وَالصُّلْحُ خَيْرٌ ۗ وَأُحْضِرَتِ الْأَنفُسُ الشُّحَّ ۚ وَإِن تُحْسِنُوا وَتَتَّقُوا فَإِنَّ اللَّـهَ كَانَ بِمَا تَعْمَلُونَ خَبِيرًا﴿١٢٨﴾
128. Na ikiwa mke atakhofia kutoka kwa mumewe nushuwzaa
(uonevu wa ndoa) au kutengwa, basi si vibaya juu yake wakisikilizana
baina yao kwa sulhu Na sulhu ni bora. Na nafsi zimewekewa uchoyo (mbele ya macho yake) Na mkifanya ihsaan na mkawa na taqwa, basi hakika Allaah daima kwa mfanyao ni Khabiyraa (Mjuzi wa yaliyodhahiri na yaliyofichikana).
وَلَن تَسْتَطِيعُوا أَن تَعْدِلُوا بَيْنَ النِّسَاءِ وَلَوْ حَرَصْتُمْ ۖ فَلَا تَمِيلُوا كُلَّ الْمَيْلِ فَتَذَرُوهَا كَالْمُعَلَّقَةِ ۚ وَإِن تُصْلِحُوا وَتَتَّقُوا فَإِنَّ اللَّـهَ كَانَ غَفُورًا رَّحِيمًا﴿١٢٩﴾
129. Na wala hamtaweza
kuadilisha baina ya wake japokuwa mkipania. Basi msielemee muelemeo
wote (kwa mke mmoja) mkamuacha (mke mwengine (msiyempenda) kama
kining’inio (aliyetundikwa). Na mkisuluhisha na mkawa na taqwa, basi
hakika Allaah daima ni Ghafuwrar-Rahiymaa (Mwingi wa kughufuria – Mwenye kurehemu).
وَإِن يَتَفَرَّقَا يُغْنِ اللَّـهُ كُلًّا مِّن سَعَتِهِ ۚ وَكَانَ اللَّـهُ وَاسِعًا حَكِيمًا﴿١٣٠﴾
130. Na wakifarikiana (kwa talaka) basi Allaah Atampa utajiri kila mmoja katika wasaa Wake. Na Allaah daima ni Waasi‘an-Hakiymaa (Mwenye wasaa – Mwenye hikmah wa yote).
وَلِلَّـهِ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ ۗ وَلَقَدْ وَصَّيْنَا الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ مِن قَبْلِكُمْ وَإِيَّاكُمْ أَنِ اتَّقُوا اللَّـهَ ۚ وَإِن تَكْفُرُوا فَإِنَّ لِلَّـهِ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ ۚ وَكَانَ اللَّـهُ غَنِيًّا حَمِيدًا﴿١٣١﴾
131. Na ni vya Allaah
Pekee vyote vilivyomo katika mbingu na vilivyomo katika ardhi. Na kwa
yakini Tumewausia wale waliopewa Kitabu kabla yenu na (Tumewausia) nanyi
(pia), kwamba: “Mcheni Allaah.” Na mkikufuru basi hakika ni vya Allaah
Pekee vyote vilivyomo katika mbingu na vilivyomo katika ardhi. Na Allaah daima ni Ghaniyyan-Hamiydaa (Mkwasi – Mwenye kustahiki kuhimidiwa).
وَلِلَّـهِ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ ۚ وَكَفَىٰ بِاللَّـهِ وَكِيلًا﴿١٣٢﴾
132. Na ni vya Allaah Pekee vyote vilivyomo katika mbingu na vilivyomo katika ardhi. Na inatosheleza Allaah kuwa ni Wakiylaa (Mdhamini Anayetegemewa kwa yote).
إِن يَشَأْ يُذْهِبْكُمْ أَيُّهَا النَّاسُ وَيَأْتِ بِآخَرِينَ ۚ وَكَانَ اللَّـهُ عَلَىٰ ذَٰلِكَ قَدِيرًا﴿١٣٣﴾
133. Akitaka, Atakuondoeni mbali enyi watu, na Ataleta wengine. Na Allaah daima kwa hayo ni Qadiyraa (Muweza wa yote).
مَّن كَانَ يُرِيدُ ثَوَابَ الدُّنْيَا فَعِندَ اللَّـهِ ثَوَابُ الدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ ۚ وَكَانَ اللَّـهُ سَمِيعًا بَصِيرًا﴿١٣٤﴾
134. Anayetaka thawabu za dunia basi kwa Allaah kuna thawabu za dunia na Aakhirah. Na Allaah daima ni Samiy’an-Baswiyraa (Mwenye kusikia yote – Mwenye kuona yote).
يَا
أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُونُوا قَوَّامِينَ بِالْقِسْطِ شُهَدَاءَ
لِلَّـهِ وَلَوْ عَلَىٰ أَنفُسِكُمْ أَوِ الْوَالِدَيْنِ وَالْأَقْرَبِينَ ۚ إِن يَكُنْ غَنِيًّا أَوْ فَقِيرًا فَاللَّـهُ أَوْلَىٰ بِهِمَا ۖ فَلَا تَتَّبِعُوا الْهَوَىٰ أَن تَعْدِلُوا ۚ وَإِن تَلْوُوا أَوْ تُعْرِضُوا فَإِنَّ اللَّـهَ كَانَ بِمَا تَعْمَلُونَ خَبِيرًا﴿١٣٥﴾
135. Enyi mlioamini! Kuweni
wenye kusimamisha uadilifu mtoapo ushahidi kwa ajili ya Allaah japokuwa
ni dhidi ya nafsi zenu au wazazi wawili, au jamaa wa karibu. Akiwa
tajiri au maskini Allaah Anawastahikia zaidi. Basi msifuate hawaa
(matamanio) mkaacha kufanya uadilifu. Na mkipotoa (ushahidi wenu) au
mkijitenga (kuepuka au kukataa kutoa ushahidi), basi hakika Allaah daima
kwa myatendayo ni Khabiyraa (Mjuzi wa yaliyodhahiri na yaliyofichikana).
يَا
أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا آمِنُوا بِاللَّـهِ وَرَسُولِهِ وَالْكِتَابِ
الَّذِي نَزَّلَ عَلَىٰ رَسُولِهِ وَالْكِتَابِ الَّذِي أَنزَلَ مِن قَبْلُ ۚ وَمَن يَكْفُرْ بِاللَّـهِ وَمَلَائِكَتِهِ وَكُتُبِهِ وَرُسُلِهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ فَقَدْ ضَلَّ ضَلَالًا بَعِيدًا﴿١٣٦﴾
136. Enyi mlioamini!
Mwaminini Allaah na Rasuli Wake na Kitabu Alichokiteremsha kwa Rasuli
Wake na Kitabu Alichokiteremsha kabla. Na atakayemkufuru Allaah na
Malaika Wake, na Vitabu Vyake na Rasuli Wake na Siku ya Mwisho, basi kwa
yakini amepotoka upotofu wa mbali.
إِنَّ
الَّذِينَ آمَنُوا ثُمَّ كَفَرُوا ثُمَّ آمَنُوا ثُمَّ كَفَرُوا ثُمَّ
ازْدَادُوا كُفْرًا لَّمْ يَكُنِ اللَّـهُ لِيَغْفِرَ لَهُمْ وَلَا
لِيَهْدِيَهُمْ سَبِيلًا﴿١٣٧﴾
137. Hakika wale walioamini kisha wakakufuru kisha wakaamini kisha wakakufuru, kisha wakazidi kufru, Allaah Hatowaghufiria na wala Hatowaongoa njia.
بَشِّرِ الْمُنَافِقِينَ بِأَنَّ لَهُمْ عَذَابًا أَلِيمًا﴿١٣٨﴾
138. Wabashirie wanafiki kwamba watapata adhabu iumizayo.
الَّذِينَ يَتَّخِذُونَ الْكَافِرِينَ أَوْلِيَاءَ مِن دُونِ الْمُؤْمِنِينَ ۚ أَيَبْتَغُونَ عِندَهُمُ الْعِزَّةَ فَإِنَّ الْعِزَّةَ لِلَّـهِ جَمِيعًا﴿١٣٩﴾
139. Wale wanaofanya makafiri kuwa ni marafiki wandani na ushirikiano badala ya Waumini. Je wanatafuta utukufu (wa nguvu) kutoka kwao? Basi hakika utukufu wote ni wa Allaah Pekee.
وَقَدْ
نَزَّلَ عَلَيْكُمْ فِي الْكِتَابِ أَنْ إِذَا سَمِعْتُمْ آيَاتِ اللَّـهِ
يُكْفَرُ بِهَا وَيُسْتَهْزَأُ بِهَا فَلَا تَقْعُدُوا مَعَهُمْ حَتَّىٰ
يَخُوضُوا فِي حَدِيثٍ غَيْرِهِ ۚ إِنَّكُمْ إِذًا مِّثْلُهُمْ ۗ إِنَّ اللَّـهَ جَامِعُ الْمُنَافِقِينَ وَالْكَافِرِينَ فِي جَهَنَّمَ جَمِيعًا﴿١٤٠﴾
140. (Naye) Amekwishakuteremshieni katika Kitabu kwamba mnaposikia Aayaat za Allaah zinakanushwa na zinafanyiwa istihzai, basi msikae pamoja nao mpaka waingie katika hadiyth (mazungumzo) mengineyo. Au sivyo mtakuwa kama wao. Hakika Allaah Atawakusanya wanafiki na makafiri wote pamoja katika (Moto wa) Jahannam.
الَّذِينَ
يَتَرَبَّصُونَ بِكُمْ فَإِن كَانَ لَكُمْ فَتْحٌ مِّنَ اللَّـهِ قَالُوا
أَلَمْ نَكُن مَّعَكُمْ وَإِن كَانَ لِلْكَافِرِينَ نَصِيبٌ قَالُوا أَلَمْ
نَسْتَحْوِذْ عَلَيْكُمْ وَنَمْنَعْكُم مِّنَ الْمُؤْمِنِينَ ۚ فَاللَّـهُ يَحْكُمُ بَيْنَكُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ ۗ وَلَن يَجْعَلَ اللَّـهُ لِلْكَافِرِينَ عَلَى الْمُؤْمِنِينَ سَبِيلًا﴿١٤١﴾
141. Wale (wanafiki)
wanaokungojeeni na kuangaza (mpate msiba). Inapokuwa ni ushindi kwenu
kutoka kwa Allaah; husema: “Je, hatukuwa pamoja nanyi?” Na inapokuwa kwa
makafiri sehemu (ya ushindi); husema: “Hatukukudhibitini (tulipokuwa
katika jeshi la Waislamu) na tukakuzuilieni (kukukingeni) na Waumini?”
Basi Allaah Atawahukumu baina yenu Siku ya Qiyaamah. Na Allaah
Hatojaalia kwa makafiri njia dhidi ya Waumini (ya kuwashinda).
إِنَّ
الْمُنَافِقِينَ يُخَادِعُونَ اللَّـهَ وَهُوَ خَادِعُهُمْ وَإِذَا
قَامُوا إِلَى الصَّلَاةِ قَامُوا كُسَالَىٰ يُرَاءُونَ النَّاسَ وَلَا
يَذْكُرُونَ اللَّـهَ إِلَّا قَلِيلًا﴿١٤٢﴾
142. Hakika wanafiki (wanadhani) wanamhadaa Allaah, na hali Yeye (Allaah) Anawahadaa (kuwalipiza). Na wanaposimama kuswali husimama kwa uvivu, riyaa-a (wakijionyesha) kwa watu na wala hawamdhukuru Allaah isipokuwa kidogo tu
مُّذَبْذَبِينَ بَيْنَ ذَٰلِكَ لَا إِلَىٰ هَـٰؤُلَاءِ وَلَا إِلَىٰ هَـٰؤُلَاءِ ۚ وَمَن يُضْلِلِ اللَّـهُ فَلَن تَجِدَ لَهُ سَبِيلًا﴿١٤٣﴾
143. Madhabidhabina baina ya huko (kwa Waislamu na huko kwa makafiri), huku hawako wala huko hawako. Na ambaye Allaah Amempotoa huwezi kumpatia njia (ya kumwongoa).
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَتَّخِذُوا الْكَافِرِينَ أَوْلِيَاءَ مِن دُونِ الْمُؤْمِنِينَ ۚ أَتُرِيدُونَ أَن تَجْعَلُوا لِلَّـهِ عَلَيْكُمْ سُلْطَانًا مُّبِينًا﴿١٤٤﴾
144. Enyi mlioamini! Msiwafanye makafiri kuwa marafiki wandani na ushirikiano badala ya Waumini. Je, mnataka Allaah Awe na hoja bayana dhidi yenu? (iwe sababu ya kukuadhibuni?).
إِنَّ الْمُنَافِقِينَ فِي الدَّرْكِ الْأَسْفَلِ مِنَ النَّارِ وَلَن تَجِدَ لَهُمْ نَصِيرًا﴿١٤٥﴾
145. Hakika wanafiki watakuwa katika tabaka la chini kabisa katika Moto; na wala hutompata kwa ajili yao mwenye kunusuru.
إِلَّا الَّذِينَ تَابُوا وَأَصْلَحُوا وَاعْتَصَمُوا بِاللَّـهِ وَأَخْلَصُوا دِينَهُمْ لِلَّـهِ فَأُولَـٰئِكَ مَعَ الْمُؤْمِنِينَ ۖ وَسَوْفَ يُؤْتِ اللَّـهُ الْمُؤْمِنِينَ أَجْرًا عَظِيمًا﴿١٤٦﴾
146. Isipokuwa wale waliotubu na wakatengenea
na wakashikamana na Allaah na wakakhalisisha Dini yao kwa ajili ya
Allaah; basi hao watakuwa pamoja na Waumini. Na Allaah Atawapa Waumini
ujira adhimu.
مَّا يَفْعَلُ اللَّـهُ بِعَذَابِكُمْ إِن شَكَرْتُمْ وَآمَنتُمْ ۚ وَكَانَ اللَّـهُ شَاكِرًا عَلِيمًا﴿١٤٧﴾
147. Allaah Hatokuadhibuni ikiwa mtashukuru na mtaamini. Na Allaah daima ni Shaakiran ‘Aliymaa (Mwenye kupokea shukurani – Mjuzi wa yote).
لَّا يُحِبُّ اللَّـهُ الْجَهْرَ بِالسُّوءِ مِنَ الْقَوْلِ إِلَّا مَن ظُلِمَ ۚ وَكَانَ اللَّـهُ سَمِيعًا عَلِيمًا﴿١٤٨﴾
148. Allaah Hapendi uovu utajwe hadharani isipokuwa kwa yule aliyedhulumiwa. Na Allaah daima ni Samiy’an-‘Aliymaa (Mwenye kusikia yote – Mjuzi wa yote).
إِن تُبْدُوا خَيْرًا أَوْ تُخْفُوهُ أَوْ تَعْفُوا عَن سُوءٍ فَإِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَفُوًّا قَدِيرًا﴿١٤٩﴾
149. Mkidhihirisha kheri au mkiificha au mkisamehe uovu; basi hakika Allaah daima ni ‘Afuwwan-Qadiyraa (Mwingi wa kusamehe – Muweza wa yote).
إِنَّ
الَّذِينَ يَكْفُرُونَ بِاللَّـهِ وَرُسُلِهِ وَيُرِيدُونَ أَن
يُفَرِّقُوا بَيْنَ اللَّـهِ وَرُسُلِهِ وَيَقُولُونَ نُؤْمِنُ بِبَعْضٍ
وَنَكْفُرُ بِبَعْضٍ وَيُرِيدُونَ أَن يَتَّخِذُوا بَيْنَ ذَٰلِكَ سَبِيلًا﴿١٥٠﴾
150. Hakika wale waliomkufuru Allaah na Rasuli Wake; na wanataka kufarikisha baina ya Allaah na Rasuli Wake; na wanasema: “Tunaamini baadhi (ya Rasuli) na tunawakanusha baadhi”; na wanataka kuchukua njia iliyo baina ya hayo.
أُولَـٰئِكَ هُمُ الْكَافِرُونَ حَقًّا ۚ وَأَعْتَدْنَا لِلْكَافِرِينَ عَذَابًا مُّهِينًا﴿١٥١﴾
151. Hao ndio makafiri wa kweli. Na Tumewaandalia makafiri adhabu ya kudhalilisha.
وَالَّذِينَ آمَنُوا بِاللَّـهِ وَرُسُلِهِ وَلَمْ يُفَرِّقُوا بَيْنَ أَحَدٍ مِّنْهُمْ أُولَـٰئِكَ سَوْفَ يُؤْتِيهِمْ أُجُورَهُمْ ۗ وَكَانَ اللَّـهُ غَفُورًا رَّحِيمًا﴿١٥٢﴾
152. Na wale waliomwamini Allaah na Rasuli Wake na hawakumfarikisha yeyote baina yao; hao Atawapa ujira wao. Na Allaah daima ni Ghafuwrar-Rahiymaa (Mwingi wa kughufuria - Mwenye kurehemu).
يَسْأَلُكَ أَهْلُ الْكِتَابِ أَن تُنَزِّلَ عَلَيْهِمْ كِتَابًا مِّنَ السَّمَاءِ ۚ فَقَدْ سَأَلُوا مُوسَىٰ أَكْبَرَ مِن ذَٰلِكَ فَقَالُوا أَرِنَا اللَّـهَ جَهْرَةً فَأَخَذَتْهُمُ الصَّاعِقَةُ بِظُلْمِهِمْ ۚ ثُمَّ اتَّخَذُوا الْعِجْلَ مِن بَعْدِ مَا جَاءَتْهُمُ الْبَيِّنَاتُ فَعَفَوْنَا عَن ذَٰلِكَ ۚ وَآتَيْنَا مُوسَىٰ سُلْطَانًا مُّبِينًا﴿١٥٣﴾
153. Wanakuuliza Ahlul-Kitaabi (Mayahudi
na Manaswara) uwateremshie kitabu juu yao kutoka mbinguni. Kwa yakini
walimuuliza Muwsaa makubwa kuliko hayo. Walisema: “Tuonyeshe Allaah
waziwazi”. Basi iliwachukuwa radi na umeme angamizi kwa
dhulma yao. Kisha wakamchukua ndama (kumwabudu) baada ya kwisha kuwajia
hoja bayana. Tukawasamehe hayo; na Tukampa Muwsaa mamlaka bayana.
وَرَفَعْنَا
فَوْقَهُمُ الطُّورَ بِمِيثَاقِهِمْ وَقُلْنَا لَهُمُ ادْخُلُوا الْبَابَ
سُجَّدًا وَقُلْنَا لَهُمْ لَا تَعْدُوا فِي السَّبْتِ وَأَخَذْنَا مِنْهُم
مِّيثَاقًا غَلِيظًا﴿١٥٤﴾
154. Na Tukaunyanyua juu yao jabali
kwa (kukanusha) fungamano lao; na Tukawaambia: “Ingieni mlangoni hali
mkiwa mmeinama kwa kunyenyekea”; na Tukawaambia: “Msivunje mipaka ya As-Sabt (shariy’ah ya Jumamosi)”. Na Tukachukua kutoka kwao fungamano madhubuti.
فَبِمَا
نَقْضِهِم مِّيثَاقَهُمْ وَكُفْرِهِم بِآيَاتِ اللَّـهِ وَقَتْلِهِمُ
الْأَنبِيَاءَ بِغَيْرِ حَقٍّ وَقَوْلِهِمْ قُلُوبُنَا غُلْفٌ ۚ بَلْ طَبَعَ اللَّـهُ عَلَيْهَا بِكُفْرِهِمْ فَلَا يُؤْمِنُونَ إِلَّا قَلِيلًا﴿١٥٥﴾
155. Na (Tukawaalani) kwa kuvunja kwao fungamano lao, na kufru zao kwa Aayaat
(ishara, dalili n.k) za Allaah, na kuua kwao Nabiy bila ya haki, na
kauli yao: “Nyoyo zetu zimefumbwa”; bali Allaah Amezipiga chapa juu yake
kwa sababu ya kufuru zao; basi hawatoamini ila kidogo.
وَبِكُفْرِهِمْ وَقَوْلِهِمْ عَلَىٰ مَرْيَمَ بُهْتَانًا عَظِيمًا﴿١٥٦﴾
156. Na (Tukawaalani) kwa kufuru zao na kauli yao juu ya Maryam ni usingiziaji mkuu wa kashfa (kuwa amezini).
وَقَوْلِهِمْ
إِنَّا قَتَلْنَا الْمَسِيحَ عِيسَى ابْنَ مَرْيَمَ رَسُولَ اللَّـهِ
وَمَا قَتَلُوهُ وَمَا صَلَبُوهُ وَلَـٰكِن شُبِّهَ لَهُمْ ۚ وَإِنَّ الَّذِينَ اخْتَلَفُوا فِيهِ لَفِي شَكٍّ مِّنْهُ ۚ مَا لَهُم بِهِ مِنْ عِلْمٍ إِلَّا اتِّبَاعَ الظَّنِّ ۚ وَمَا قَتَلُوهُ يَقِينًا﴿١٥٧﴾
157. Na kauli yao: “Hakika sisi tumemuua Al-Masiyh ‘Iysaa mwana wa Maryam, Rasuli
wa Allaah.” Na wala hawakumuua wala hawakumsulubu lakini
walishabihishiwa (mtu mwengine wakadhani ni ‘Iysaa). Na hakika wale
waliokhitilafiana katika hayo (kuhusu kumuua Nabiy ‘Iysaa); kwa hakika
wamo katika shaka nalo. Hawana ujuzi nalo kabisa isipokuwa kufuata dhana
tu. Na kwa yakini hawakumuua.
بَل رَّفَعَهُ اللَّـهُ إِلَيْهِ ۚ وَكَانَ اللَّـهُ عَزِيزًا حَكِيمًا﴿١٥٨﴾
158. Bali Allaah Alimnyanyua Kwake. Na Allaah daima ni ‘Aziyzan-Hakiymaa (Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika - Mwenye hikmah wa yote).
وَإِن مِّنْ أَهْلِ الْكِتَابِ إِلَّا لَيُؤْمِنَنَّ بِهِ قَبْلَ مَوْتِهِ ۖ وَيَوْمَ الْقِيَامَةِ يَكُونُ عَلَيْهِمْ شَهِيدًا﴿١٥٩﴾
159. Na hakuna yeyote katika Ahlil-Kitaabi (Mayahudi na Manaswara) ila atamwamini kabla ya kufa kwake. Na Siku ya Qiyaamah atakuwa shahidi juu yao.
فَبِظُلْمٍ مِّنَ الَّذِينَ هَادُوا حَرَّمْنَا عَلَيْهِمْ طَيِّبَاتٍ أُحِلَّتْ لَهُمْ وَبِصَدِّهِمْ عَن سَبِيلِ اللَّـهِ كَثِيرًا﴿١٦٠﴾
160. Basi kwa dhulma ya Mayahudi;
Tuliwaharamishia vizuri yaliyohalalishwa kwao; na kwa sababu ya
kuwazuilia wengi njia ya Allaah.
وَأَخْذِهِمُ الرِّبَا وَقَدْ نُهُوا عَنْهُ وَأَكْلِهِمْ أَمْوَالَ النَّاسِ بِالْبَاطِلِ ۚ وَأَعْتَدْنَا لِلْكَافِرِينَ مِنْهُمْ عَذَابًا أَلِيمًا﴿١٦١﴾
161. Na kuchukua kwao ribaa na hali
walikatazwa kuichukua; na kula kwao mali za watu kwa ubatilifu. Na
Tumeandalia kwa makafiri miongoni mwao adhabu iumizayo.
لَّـٰكِنِ الرَّاسِخُونَ فِي الْعِلْمِ مِنْهُمْ وَالْمُؤْمِنُونَ يُؤْمِنُونَ بِمَا أُنزِلَ إِلَيْكَ وَمَا أُنزِلَ مِن قَبْلِكَ ۚ وَالْمُقِيمِينَ الصَّلَاةَ ۚ وَالْمُؤْتُونَ الزَّكَاةَ وَالْمُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ أُولَـٰئِكَ سَنُؤْتِيهِمْ أَجْرًا عَظِيمًا﴿١٦٢﴾
162. Lakini Ar-Raasikhuwn (wenye msingi madhubuti) katika elimu miongoni mwao, na Waumini wanaoamini yale aliyoteremshwa kwako (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم)
na yale yaliyoteremshwa kabla yako; na wasimamishao Swalaah, na watoao
Zakaah na wanaomwamini Allaah na Siku ya Mwisho. Hao Tutawapa ujira
adhimu.
إِنَّا أَوْحَيْنَا إِلَيْكَ كَمَا أَوْحَيْنَا إِلَىٰ نُوحٍ وَالنَّبِيِّينَ مِن بَعْدِهِ ۚ
وَأَوْحَيْنَا إِلَىٰ إِبْرَاهِيمَ وَإِسْمَاعِيلَ وَإِسْحَاقَ
وَيَعْقُوبَ وَالْأَسْبَاطِ وَعِيسَىٰ وَأَيُّوبَ وَيُونُسَ وَهَارُونَ
وَسُلَيْمَانَ ۚ وَآتَيْنَا دَاوُودَ زَبُورًا﴿١٦٣﴾
163. Hakika Tumekufunulia Wahy (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) kama Tulivyomfunulia Wahy Nuwh na Nabiy baada yake. Na Tumemfunulia Wahy Ibraahiym na Ismaa’iyl na Is-haaq na Ya’quwb na al-Asbaatw (Makabila ya wana wa Ya’quwb عليه السلام waliotoka Manabii) na ‘Iysaa na Ayyuwb na Yuwnus na Haaruwn, Na Sulaymaan. Na Tumempa Daawuwd Zabuwraa.
وَرُسُلًا قَدْ قَصَصْنَاهُمْ عَلَيْكَ مِن قَبْلُ وَرُسُلًا لَّمْ نَقْصُصْهُمْ عَلَيْكَ ۚ وَكَلَّمَ اللَّـهُ مُوسَىٰ تَكْلِيمًا﴿١٦٤﴾
164. Na (Tuliwafunulia Wahy) Rasuli Tuliokwishakusimulia (habari zao) kabla; na Rasuli (wengine) Hatukukusimulia (habari zao). Na bila shaka Allaah Alimsemesha Muwsaa maneno (moja kwa moja).
رُّسُلًا مُّبَشِّرِينَ وَمُنذِرِينَ لِئَلَّا يَكُونَ لِلنَّاسِ عَلَى اللَّـهِ حُجَّةٌ بَعْدَ الرُّسُلِ ۚ وَكَانَ اللَّـهُ عَزِيزًا حَكِيمًا﴿١٦٥﴾
165. Rasuli ni wabashiriajina waonyaji ili pasikuweko kutoka kwa watu hoja yoyote juu ya Allaah baada ya (kuletwa) Rasuli. Na Allaah daima ni ‘Aziyzan-Hakiymaa (Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika - Mwenye hikmah wa yote).
لَّـٰكِنِ اللَّـهُ يَشْهَدُ بِمَا أَنزَلَ إِلَيْكَ ۖ أَنزَلَهُ بِعِلْمِهِ ۖ وَالْمَلَائِكَةُ يَشْهَدُونَ ۚ وَكَفَىٰ بِاللَّـهِ شَهِيدًا﴿١٦٦﴾
166. Lakini Allaah Anayashuhudia
Aliyoyateremsha kwako; (kuwa) Ameyateremsha kwa elimu Yake; na Malaika
(pia) wanashuhudia. Na Anatosheleza Allaah kuwa Shahiydaa (Mwenye kushuhudia yote).
إِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا وَصَدُّوا عَن سَبِيلِ اللَّـهِ قَدْ ضَلُّوا ضَلَالًا بَعِيدًا﴿١٦٧﴾
167. Hakika wale waliokufuru na wakazuia (watu) njia ya Allaah, kwa yakini wamekwishapotea upotofu wa mbali.
إِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا وَظَلَمُوا لَمْ يَكُنِ اللَّـهُ لِيَغْفِرَ لَهُمْ وَلَا لِيَهْدِيَهُمْ طَرِيقًا﴿١٦٨﴾
168. Hakika wale waliokufuru na wakadhulumu; haitokuwa kwa Allaah kuwaghufuria wala kuwaongoza njia.
إِلَّا طَرِيقَ جَهَنَّمَ خَالِدِينَ فِيهَا أَبَدًا ۚ وَكَانَ ذَٰلِكَ عَلَى اللَّـهِ يَسِيرًا﴿١٦٩﴾
169. Isipokuwa njia ya (Moto wa) Jahannam ni wenye kudumu humo abadi. Na hayo kwa Allaah ni mepesi.
يَا أَيُّهَا النَّاسُ قَدْ جَاءَكُمُ الرَّسُولُ بِالْحَقِّ مِن رَّبِّكُمْ فَآمِنُوا خَيْرًا لَّكُمْ ۚ وَإِن تَكْفُرُوا فَإِنَّ لِلَّـهِ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ وَكَانَ اللَّـهُ عَلِيمًا حَكِيمًا﴿١٧٠﴾
170. Enyi watu! Kwa yakini amekujieni Rasuli kwa haki kutoka kwa Rabb (Mola)
wenu; basi aminini; ni bora kwenu. Na mkikufuru; basi hakika ni vya
Allaah Pekee viliyomo mbinguni na ardhini. Na Allaah daima ni ‘Aliyman-Hakiymaa (Mjuzi wa yote – Mwenye hikmah wa yote).
يَا أَهْلَ الْكِتَابِ لَا تَغْلُوا فِي دِينِكُمْ وَلَا تَقُولُوا عَلَى اللَّـهِ إِلَّا الْحَقَّ ۚ إِنَّمَا الْمَسِيحُ عِيسَى ابْنُ مَرْيَمَ رَسُولُ اللَّـهِ وَكَلِمَتُهُ أَلْقَاهَا إِلَىٰ مَرْيَمَ وَرُوحٌ مِّنْهُ ۖ فَآمِنُوا بِاللَّـهِ وَرُسُلِهِ ۖ وَلَا تَقُولُوا ثَلَاثَةٌ ۚ انتَهُوا خَيْرًا لَّكُمْ ۚ إِنَّمَا اللَّـهُ إِلَـٰهٌ وَاحِدٌ ۖسُبْحَانَهُ أَن يَكُونَ لَهُ وَلَدٌ ۘ لَّهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ ۗ وَكَفَىٰ بِاللَّـهِ وَكِيلًا﴿١٧١﴾
171. Enyi Ahlal-Kitaabi! Msipindukie mipaka katika dini yenu, wala msiseme juu ya Allaah isipokuwa ukweli. Hakika Al-Masiyh ‘Iysaa mwana wa Maryam ni Rasuli wa Allaah na ni neno Lake (la Kun!) Alompelekea Maryam na Ruwhun (roho Aloumba kwa amrisho) kutoka Kwake. Basi mwaminini Allaah na Rasuli Wake; wala msiseme: ‘watatu’. Komeni, ni kheri kwenu. Hakika Allaah ni Ilaah (Muabudiwa wa haki) Mmoja (Pekee) Subhaanah!
(Utakasifu ni Wake) kuwa ana waladi! Ni Vyake vyote viliyomo mbinguni
na vyote viliyomo ardhini. Na Anatosheleza Allaah kuwa ni Wakiylaa (Mdhamini Anayetegemewa kwa yote).
لَّن يَسْتَنكِفَ الْمَسِيحُ أَن يَكُونَ عَبْدًا لِّلَّـهِ وَلَا الْمَلَائِكَةُ الْمُقَرَّبُونَ ۚ وَمَن يَسْتَنكِفْ عَنْ عِبَادَتِهِ وَيَسْتَكْبِرْ فَسَيَحْشُرُهُمْ إِلَيْهِ جَمِيعًا﴿١٧٢﴾
172. Al-Masiyh hatokuwa na
kiburi kamwe kukataa kuwa mja kwa Allaah, wala Malaika waliokurubishwa
(Kwake). Na atakayekataa (kwa beza au dharau) ‘ibaadah Yake na
kutakabari, basi Atawakusanya wote Kwake (Siku ya Qiyaamah).
فَأَمَّا الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ فَيُوَفِّيهِمْ أُجُورَهُمْ وَيَزِيدُهُم مِّن فَضْلِهِ ۖ
وَأَمَّا الَّذِينَ اسْتَنكَفُوا وَاسْتَكْبَرُوا فَيُعَذِّبُهُمْ
عَذَابًا أَلِيمًا وَلَا يَجِدُونَ لَهُم مِّن دُونِ اللَّـهِ وَلِيًّا
وَلَا نَصِيرًا﴿١٧٣﴾
173. Ama wale walioamini na wakatenda
mema; (Allaah) Atawalipa kwa ukamilifu ujira wao; na Atawazidishia kwa
fadhila Zake. Ama waliokataa kwa kiburi na wakatakabari; Atawaadhibu
adhabu iumizayo; na wala hawatopata pasi na Allaah mlinzi wala mwenye
kunusuru.
يَا أَيُّهَا النَّاسُ قَدْ جَاءَكُم بُرْهَانٌ مِّن رَّبِّكُمْ وَأَنزَلْنَا إِلَيْكُمْ نُورًا مُّبِينًا﴿١٧٤﴾
174. Enyi watu! Kwa yakini imekujieni burhaan (dalili bayana) kutoka kwa Rabb (Mola) wenu na Tumekuteremshieni Nuru bayana.
فَأَمَّا
الَّذِينَ آمَنُوا بِاللَّـهِ وَاعْتَصَمُوا بِهِ فَسَيُدْخِلُهُمْ فِي
رَحْمَةٍ مِّنْهُ وَفَضْلٍ وَيَهْدِيهِمْ إِلَيْهِ صِرَاطًا مُّسْتَقِيمًا﴿١٧٥﴾
175. Ama wale waliomwamini Allaah, na
wakashikamana Naye; Atawaingiza katika Rahmah kutoka Kwake na fadhila,
na Atawaongoza Kwake (katika) njia iliyonyooka.
يَسْتَفْتُونَكَ قُلِ اللَّـهُ يُفْتِيكُمْ فِي الْكَلَالَةِ ۚ إِنِ امْرُؤٌ هَلَكَ لَيْسَ لَهُ وَلَدٌ وَلَهُ أُخْتٌ فَلَهَا نِصْفُ مَا تَرَكَ ۚ وَهُوَ يَرِثُهَا إِن لَّمْ يَكُن لَّهَا وَلَدٌ ۚ فَإِن كَانَتَا اثْنَتَيْنِ فَلَهُمَا الثُّلُثَانِ مِمَّا تَرَكَ ۚ وَإِن كَانُوا إِخْوَةً رِّجَالًا وَنِسَاءً فَلِلذَّكَرِ مِثْلُ حَظِّ الْأُنثَيَيْنِ ۗ يُبَيِّنُ اللَّـهُ لَكُمْ أَن تَضِلُّوا ۗ وَاللَّـهُ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ﴿١٧٦﴾
176. Wanatafuta kwako fatwa. Sema: Allaah Atakufutuni kuhusu al-kalaalah (mkiwa).
Ikiwa mtu amefariki hana waladi lakini ana dada; basi (huyo dada)
atastahiki nusu ya yale (mali) aliyoyaacha (maiti). Na yeye (huyo mtu)
atamrithi (huyo dada) kama hana waladi. Na ikiwa wao (madada) ni wawili;
basi (wote wawili) watastahiki thuluthi mbili ya yale (mali)
aliyoyaacha (maiti). Na wakiwa ni ndugu wanaume na wanawake; basi (kila)
mwanamme atastahiki sehemu iliyo sawa na (sehemu) ya wanawake wawili.
Allaah Anakubainishieni (shariy’ahYake) ili msipotee; na Allaah kwa kila kitu ni ‘Aliym (Mjuzi).
Ukitaka kusoma Sura nyengine Rejeauliko toka
Ukiwa una shauri au maelezo juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii falhaqqiy@gmail.com
Ukiwa una shauri au maelezo juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii falhaqqiy@gmail.com