الْحُجُرَات
Al-Hujuraat: 49
(Imeteremka Madina)
Imeanza
Sura hii kwa kuwakataza Waumini kuhukumia kitu kabla
Mwenyezi Mungu na Mtume wake hawajaamrisha, na pia wasinyanyue sauti zao juu ya
sauti ya Nabii s.a.w. Na imewasifu wale wanao teremsha sauti zao mbele yake. Na
imewalaumu wanao kosa adabu wakampigia kelele Mtume s.a.w. nyuma ya vyumba,
yaani naye yuko ndani nyumbani kwake. Kisha ikawaamrisha Waumini wahakikishe
khabari za wapotovu na wachache wa Imani, na
ikwaamrisha wenye madaraka nini la kutenda wanapo pigana makundi mawili ya
Waumini wenyewe kwa wenyewe. Na imewakataza Waumini wasifanyiane kejeli
wao kwa wao. Na imewakataza wakaazi wa
majangwani kudai kuwa wana Imani kabla haijatua hiyo Imani katika nyoyo zao.
Kisha Sura imebainisha ni nani hao Waumini wa kweli,
na ikakhitimishia mazungumzo kwa kukataza kumsimbulia Mtume wa Mwenyezi Mungu
kwa ajili ya kusilimu kwao. Na ikabainisha kwamba hakika aliye fanya hisani juu
yao ni Mwenyezi Mungu kwa kuwaongoza kwenye Imani,
ikiwa wao ni wasema kweli katika madai yao.
بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تُقَدِّمُوا بَيْنَ يَدَيِ اللَّـهِ وَرَسُولِهِ ۖ وَاتَّقُوا اللَّـهَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ سَمِيعٌ عَلِيمٌ﴿١﴾
1. Enyi mlioamini! Msikadimishe (kuhukumu jambo) mbele ya Allaah na Rasuli Wake. Na mcheni Allaah; hakika Allaah ni Samiy’un-‘Aliym (Mwenye kusikia yote - Mjuzi wa yote).
يَا
أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَرْفَعُوا أَصْوَاتَكُمْ فَوْقَ صَوْتِ
النَّبِيِّ وَلَا تَجْهَرُوا لَهُ بِالْقَوْلِ كَجَهْرِ بَعْضِكُمْ
لِبَعْضٍ أَن تَحْبَطَ أَعْمَالُكُمْ وَأَنتُمْ لَا تَشْعُرُونَ﴿٢﴾
2. Enyi mlioamini! Msipandishe sauti zenu juu ya sauti ya Nabiy, na
wala msiseme naye kwa sauti ya juu, kama mnavyosemezana wenyewe kwa
wenyewe kwa sauti za juu; zisije zikabatilika ‘amali zenu nanyi hamhisi.
إِنَّ
الَّذِينَ يَغُضُّونَ أَصْوَاتَهُمْ عِندَ رَسُولِ اللَّـهِ أُولَـٰئِكَ
الَّذِينَ امْتَحَنَ اللَّـهُ قُلُوبَهُمْ لِلتَّقْوَىٰ ۚ لَهُم مَّغْفِرَةٌ وَأَجْرٌ عَظِيمٌ﴿٣﴾
3. Hakika wale wanaoteremsha sauti zao mbele ya Rasuli wa Allaah, hao
ndio ambao Allaah Amejaribu nyoyo zao kwa ajili ya taqwa. Watapata
maghfirah na ujira adhimu.
إِنَّ الَّذِينَ يُنَادُونَكَ مِن وَرَاءِ الْحُجُرَاتِ أَكْثَرُهُمْ لَا يَعْقِلُونَ﴿٤﴾
4. Hakika wale wanaokuita (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) nyuma ya vyumba, wengi wao hawatii akilini.
وَلَوْ أَنَّهُمْ صَبَرُوا حَتَّىٰ تَخْرُجَ إِلَيْهِمْ لَكَانَ خَيْرًا لَّهُمْ ۚ وَاللَّـهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ﴿٥﴾
5. Na lau kwamba wao wangelisubiri mpaka ukawatokea, bila shaka ingelikuwa ni kheri kwao. Na Allaah ni Ghafuwrur-Rahiym (Mwingi wa kughufuria - Mwenye kurehemu).
يَا
أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِن جَاءَكُمْ فَاسِقٌ بِنَبَإٍ فَتَبَيَّنُوا
أَن تُصِيبُوا قَوْمًا بِجَهَالَةٍ فَتُصْبِحُوا عَلَىٰ مَا فَعَلْتُمْ
نَادِمِينَ﴿٦﴾
6. Enyi mlioamini! Anapokujieni fasiki kwa habari yoyote, basi
(kwanza) pelelezeni, msije mkawasibu (madhara) watu kwa ujahili, mkawa
juu ya ambayo mmeyafanya ni wenye kujuta.
وَاعْلَمُوا أَنَّ فِيكُمْ رَسُولَ اللَّـهِ ۚ
لَوْ يُطِيعُكُمْ فِي كَثِيرٍ مِّنَ الْأَمْرِ لَعَنِتُّمْ وَلَـٰكِنَّ
اللَّـهَ حَبَّبَ إِلَيْكُمُ الْإِيمَانَ وَزَيَّنَهُ فِي قُلُوبِكُمْ
وَكَرَّهَ إِلَيْكُمُ الْكُفْرَ وَالْفُسُوقَ وَالْعِصْيَانَ ۚ أُولَـٰئِكَ هُمُ الرَّاشِدُونَ﴿٧﴾
7. Na jueni kwamba pamoja nanyi yuko Rasuli wa Allaah. Lau kama
atakutiini katika mambo mengi (mnayoyapendelea), bila shaka
mngelitaabika; lakini Allaah Amekupendezesheeni iymaan, na Akaipamba
katika nyoyo zenu; na Akakuchukizisheni kufuru, na ufasiki na uasi. Hao
ndio waliongoka sawasawa.
فَضْلًا مِّنَ اللَّـهِ وَنِعْمَةً ۚ وَاللَّـهُ عَلِيمٌ حَكِيمٌ﴿٨﴾
8. Ni fadhila kutoka kwa Allaah na neema, na Allaah ni ‘Aliymun-Hakiym (Mjuzi wa yote - Mwenye hikmah wa yote).
وَإِن طَائِفَتَانِ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ اقْتَتَلُوا فَأَصْلِحُوا بَيْنَهُمَا ۖ فَإِن بَغَتْ إِحْدَاهُمَا عَلَى الْأُخْرَىٰ فَقَاتِلُوا الَّتِي تَبْغِي حَتَّىٰ تَفِيءَ إِلَىٰ أَمْرِ اللَّـهِ ۚ فَإِن فَاءَتْ فَأَصْلِحُوا بَيْنَهُمَا بِالْعَدْلِ وَأَقْسِطُوا ۖ إِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ الْمُقْسِطِينَ﴿٩﴾
9. Na ikiwa makundi mawili ya Waumini yakipigana, basi suluhisheni
baina yao. Lakini mojawapo likikandamiza jengine, basi piganeni (vita)
na ambalo linakandamiza mpaka lielemee kwenye amri ya Allaah.
Likishaelemea, basi suluhisheni baina yao kwa uadilifu, na timizeni haki
haki. Hakika Allaah Anapenda wanaotimiza haki.
إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ إِخْوَةٌ فَأَصْلِحُوا بَيْنَ أَخَوَيْكُمْ ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ﴿١٠﴾
10. Hakika Waumini ni ndugu, basi suluhisheni baina ya ndugu zenu. Na mcheni Allaah ili mpate kurehemewa.
يَا
أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا يَسْخَرْ قَوْمٌ مِّن قَوْمٍ عَسَىٰ أَن
يَكُونُوا خَيْرًا مِّنْهُمْ وَلَا نِسَاءٌ مِّن نِّسَاءٍ عَسَىٰ أَن
يَكُنَّ خَيْرًا مِّنْهُنَّ ۖ وَلَا تَلْمِزُوا أَنفُسَكُمْ وَلَا تَنَابَزُوا بِالْأَلْقَابِ ۖ بِئْسَ الِاسْمُ الْفُسُوقُ بَعْدَ الْإِيمَانِ ۚ وَمَن لَّمْ يَتُبْ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ﴿١١﴾
11. Enyi mlioamini! Wanaume wasiwafanyie dhihaka na kudharau wanaume
(wengineo) huenda wakawa bora kuliko wao, wala wanawake kwa wanawake
(wengineo), huenda wakawa bora kuliko wao. Na wala msikashifianeni, na
wala msiitane majina (mabaya) ya utani. Ubaya ulioje wa jina la ufasiki
baada ya iymaan. Na yeyote asiyetubu, basi hao ndio madhalimu.
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اجْتَنِبُوا كَثِيرًا مِّنَ الظَّنِّ إِنَّ بَعْضَ الظَّنِّ إِثْمٌ ۖ وَلَا تَجَسَّسُوا وَلَا يَغْتَب بَّعْضُكُم بَعْضًا ۚ أَيُحِبُّ أَحَدُكُمْ أَن يَأْكُلَ لَحْمَ أَخِيهِ مَيْتًا فَكَرِهْتُمُوهُ ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ تَوَّابٌ رَّحِيمٌ﴿١٢﴾
12. Enyi mlioamini! Jieupusheni sana na dhana (mbaya), kwani hakika
baadhi ya dhana ni dhambi. Na wala msifanyiane ujasusi, na wala
wasisengenyane baadhi yenu wengineo. Je, anapenda mmoja wenu kwamba ale
nyama ya nduguye aliyekufa? Basi mmelichukia hilo! Na mcheni Allaah!
Hakika Allaah ni Tawwaabur-Rahiym (Mwingi wa kupokea tawbah - Mwenye kurehemu).
يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِنَّا خَلَقْنَاكُم مِّن ذَكَرٍ وَأُنثَىٰ وَجَعَلْنَاكُمْ شُعُوبًا وَقَبَائِلَ لِتَعَارَفُوا ۚ إِنَّ أَكْرَمَكُمْ عِندَ اللَّـهِ أَتْقَاكُمْ ۚ إِنَّ اللَّـهَ عَلِيمٌ خَبِيرٌ﴿١٣﴾
13. Enyi watu! Hakika Sisi Tumekuumbeni kutokana namwanamme na
mwanamke, na Tukakufanyeni mataifa na makabila (mbali mbali) ili
mtambuane. Hakika aliye mtukufu zaidi miongoni mwenu mbele ya Allaah ni
mwenye taqwa zaidi kati yenu. Hakika Allaah ni ‘Aliymun-Khabiyr (Mjuzi wa yote - Mjuzi wa yaliyodhahiri na yaliyofichikana).
قَالَتِ الْأَعْرَابُ آمَنَّا ۖ قُل لَّمْ تُؤْمِنُوا وَلَـٰكِن قُولُوا أَسْلَمْنَا وَلَمَّا يَدْخُلِ الْإِيمَانُ فِي قُلُوبِكُمْ ۖ وَإِن تُطِيعُوا اللَّـهَ وَرَسُولَهُ لَا يَلِتْكُم مِّنْ أَعْمَالِكُمْ شَيْئًا ۚ إِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ﴿١٤﴾
14. Mabedui walisema: “Tumeamini!” Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم):
“Hamkuamini (bado), lakini semeni: “Tumesilimu.”Kwani iymaan haijaingia
bado nyoyoni mwenu. Na mtakapomtii Allaah na Rasuli Wake,
Hatokupunguzieni katika ‘amali zenu kitu chochote. Hakika Allaah ni Ghafuwrur-Rahiym (Mwingi wa kughufuria - Mwenye kurehemu).
إِنَّمَا
الْمُؤْمِنُونَ الَّذِينَ آمَنُوا بِاللَّـهِ وَرَسُولِهِ ثُمَّ لَمْ
يَرْتَابُوا وَجَاهَدُوا بِأَمْوَالِهِمْ وَأَنفُسِهِمْ فِي سَبِيلِ
اللَّـهِ ۚ أُولَـٰئِكَ هُمُ الصَّادِقُونَ﴿١٥﴾
15. Hakika Waumini ni wale waliomwamini Allaah na Rasuli Wake, kisha
wakawa si wenye shaka, na wakafanya jihaad kwa mali zao na nafsi zao
katika njia ya Allaah. Hao ndio wakweli.
قُلْ أَتُعَلِّمُونَ اللَّـهَ بِدِينِكُمْ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ ۚ وَاللَّـهُ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ﴿١٦﴾
16. Sema (Ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم):
“Je, mnamfundisha Allaah kuhusu Dini yenu, na hali Allaah Anajua yale
yaliyomo mbinguni na yale yaliyomo ardhini? Na Allaah kwa kila kitu ni
‘Aliym (Mjuzi).
يَمُنُّونَ عَلَيْكَ أَنْ أَسْلَمُوا ۖ قُل لَّا تَمُنُّوا عَلَيَّ إِسْلَامَكُم ۖ بَلِ اللَّـهُ يَمُنُّ عَلَيْكُمْ أَنْ هَدَاكُمْ لِلْإِيمَانِ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ﴿١٧﴾
17. Wanadhani wamekufanyia ihsani kwamba wamesilimu? Sema (Ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم):
“Msidhani mmefanya ihsani kwangu kusilimu kwenu. Bali Allaah
Amekufanyieni ihsani kwamba Amekuongozeni kwenye iymaan mkiwa ni
wakweli.”
إِنَّ اللَّـهَ يَعْلَمُ غَيْبَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ وَاللَّـهُ بَصِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ﴿١٨﴾
18. Hakika Allaah Anajua ghayb ya mbingu na ardhi, na Allaah ni Baswiyr (Mwenye kuona yote) yale myatendayo.
Ukitaka kusoma Sura nyengine Rejeauliko toka
Ukiwa una shauri au maelezo juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii falhaqqiy@gmail.com
Ukiwa una shauri au maelezo juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii falhaqqiy@gmail.com