Abu ‘Ammaar
Katika
makala hii fupi inshaAllaah tutajaribu kuzitambulisha aina za ndoa na kuweza
kuzijua hukumu zake kisheria pamoja na maelezo kwa
ufupi.
Ndoa ni mkataba unaofungwa na wanandoa kuhalalisha kila mmoja wao
kuweza kustarehe na mwengine kwa mujibu wa sheria
Ndoa ni miongoni mwa alama na miujiza yake Allaah (Subhaanahu
Wata’ala) na ina dalili ya kuthibitika kwake katika Qur’aan na katika Sunnah.
Katika
Qur’aan
Suuratu
Nnisaa/3
وَإِنْ خِفْتُمْ أَلاَّ تُقْسِطُواْ فِي الْيَتَامَى فَانكِحُواْ مَا طَابَ
لَكُم مِّنَ النِّسَاء مَثْنَى وَثُلاَثَ وَرُبَاعَ فَإِنْ خِفْتُمْ أَلاَّ تَعْدِلُواْ
فَوَاحِدَةً أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُكُم
“Na ikiwa mnaogopa kuwa hamtowafanyia mayatima uadilifu, basi
oeni mnao wapenda katika wanawake, wawili au watatu au wane. Na mkiogopa kuwa
hamwezi kufanya uadilifu, basi mmoja tu, au wale ambao mikono yenu ya kulia
imewamiliki.”
Suuratu
Nnuur/32
وَأَنكِحُوا الْأَيَامَى مِنكُمْ وَالصَّالِحِينَ مِنْ عِبَادِكُمْ وَإِمَائِكُم
“Na waozeni wajane miongoni mwenu na wema katika watumwa wenu na
wajakazi wenu.”
Katika
Sunnah
يامعشر الشباب ، من استطاع منكم الباءة فليتزوج فإنه أغض للبصر وأحصن
للفرج ، ومن لم يستطع فعليه بالصوم فإنه له وجاء
أخرجه
البخاري
“Enyi vijana! Mwenye uwezo wa kuisimamia ndoa na aoe kwani huko ni
kuweza kuinamisha macho na kuweza kuzikinga tupu na kama hamna uwezo basi ni
juu yenu kufunga kwani huko ndiko kwenye kinga.” Al-Bukhaariy
Na pia:
النكاح من سنتي ، فمن لم يعمل بسنتي فليس مني
Ndoa ni miongoni mwa Sunnah zangu na mwenye kutenda kinyume na
Sunnah zangu hatokuwa pamoja na mimi. Ibn Maajah
Ili
ndoa ikamilike hupaswa kutimiza nguzo, masharti pamoja na adabu zake vinginevyo inaweza kuwa miongoni mwa ndoa zenye
utata katika uhalali wake.
Ndoa,
kwa mujibu wa Rai za Jamhuur Ulamaa (isipokuwa Abu Haniyfah), zimegawika kwenye
sehemu kuu tatu zifuatazo:
1
Ndoa sahihi
iliyokamilika
Iliyotimiza
nguzo na masharti ya kusihi kwake na kuweza kutekelezwa.
2
Ndoa Sahihi isiyokamilika
Iliyotimiza
nguzo na masharti ya kusihi kwake lakini imeshindwa kutekelezwa.
3
Ndoa batili au
fasidi
Iliyokosekana
moja ya nguzo au masharti ya kusihi kwake.
Yanayopaswa
kuwepo wakati wa kufungwa ndoa (Aqdi)
Ni
yafuatayo
1
Kuwepo mke na mume
(ambao wataweza kuisimamia ndoa na kutokuwepo vizuizi vya kuwazuia
kuoana)-miongoni mwa masharti ya ndoa.
2
Ijaabu (tamko la
kuoa au kuozesha) na Qabuul (tamko la kukubali) - miongoni mwa nguzo za ndoa
3
Awepo walii
-miongoni mwa masharti ya ndoa
4
Wawepo Mashahidi -
miongoni mwa masharti ya ndoa
Yanayopaswa
kuzingatiwa
Ni
yafuatayo
Asiwe
mmoja wa wanandoa ana vizuizi vya kuwafanya wasioane ikiwa ni vya muda au vya
kudumu.
Mkataba
wa ndoa uwe wa kudumu usiwekewe muda maalum.
Ridhaa,
chaguo na uamuzi uwe ni wa wanandoa kusiwepo kulazimishana.
Wasiwe
wanandoa katika hali ya kuhirimia kwa ajili ya Hajj au ’Umrah.
Yawepo
mahari.
Wajulikane
wanaooa au kuolewa.
Kusiwepo
mbinu za kutoitangaza ndoa na kuificha.
Ndoa batili au fasidi
1
|
NDOA
FASIDI/ BATILI
|
Iliyofisidika
kwa kukosekana moja katika nguzo, masharti ya msingi ya kufungika ndoa.
|
Ndoa hutakiwa ikamilike mambo yake yote zikiwemo nguzo masharti
ya kusihi kwake ili iweze kuwa na uhalali kisheria.
|
Haijuzu
|
2
|
NDOA
WAKATI WA IHRAAMU
|
Kuoa/kuolewa
wakati mmeshahirimia ima kwa ibadah ya Hajj au ‘Umrah
|
Kuwepo
katika hali ya Ihraamu ni moja katika mambo yanayamzuia mke/mume kufanya
tendo la ndoa na kuoa au kuwakilishwa ndoa pia ni mambo yasiyofanywa kwa aliye kwenye Ihraamu.
|
Haijuzu
|
3
|
NDOA
BILA YA WALII
|
Kufungwa
ndoa kwa kuwepo mke na mume pamoja na mashahidi lakini Walii amekosekana.
|
Ndoa
haikamiliki bila ya kuwepo kwa Walii na ni mojawapo ya nguzo za ndoa. Walii
ni mwenye haki ya kumuozesha na kusimamia ndoa kwa niaba ya binti.
|
Haijuzu
kwa mujibu wa Jamhuur Ulamaa na inajuzu kwa mwanamke aliye baleghe kujiozesha
kwa mujibu wa rai ya Abu Haniyfah.
|
4
|
NDOA
YA “WALII” ASIYEKUWA NA SIFA
|
Kufungwa
ndoa kwa kutimizwa masharti yote isipokuwa walii ni mama wa binti kwa
kukosekana baba na mfano wake.
|
Moja
katika masharti ya kusihi ndoa ni kuwepo walii mwanamme. Kisheria walii ni
mwanamme na mwanamke si miongoni mwa walii wa binti.
|
Haijuzu
|
5
|
NDOA
BILA YA KUWEPO MASHAHIDI
|
Kufungwa
ndoa wakiwepo mke na mume na walii bila ya kuwepo shahidi kama ilivyo ndoa ya Mut’ah au ndoa ya siri
|
Ni
moja katika masharti ya kusihi ndoa kwamba lazima ishuhudishwe na mashahidi
ili kuondosha dhana ya kuwepo ndoa za siri na kuondosha tuhuma na dhana.
|
Haijuzu
|
Ndoa
zenye utata katika kujuzu kwake
|
NDOA
|
MAELEZO
|
SABABU
|
HUKUMU
|
1
|
NDOA
YA MUT’AH (MUDA MAALUM)
|
Hufungwa kwa muda maalum japo masaa mawili, bila mashahidi wala
walii, ambapo wanandoa kuwa na haki kama wameoana.
|
Imewekewa muda maalum na hakuna kurithiana wala kutalikiana.
|
Haijuzu
|
2
|
NDOA
YA MHALILI (ALIYEACHIKA TALAKA TATU)
|
Kuolewa mke aliyeachika talaka tatu si kwa lengo la ndoa bali
kwa lengo la kuipinda sheria ili ahalalishiwe mume wa mwanzo.
|
Mume
anataka kurudiana na mkewe ambaye kamuacha talaka tatu na hivyo kumtafuta
mume mwengine amuoe mkewe kwa makubaliano lakini pasipatikane tendo la ndoa kisha
amuache.
Kisheria
atatakiwa aolewe na mume mwengine ndoa halisi na papatikane tendo la ndoa.
|
Haijuzu
|
3
|
NDOA
ZAIDI YA WAKE WANE
|
Mume kuoa wake zaidi ya wane kwa wakati mmoja waliokubalika kisheria.
|
Ruhusa
na mipaka tuliyowekewa na sheria ni kuwa na wake
wane tu kwa wakati mmoja. (Na hata kama mke ameachika talaka
rejea na yupo katika eda basi uharamu upo pale pale).
|
Haijuzu
|
4
|
KUOLEWA
NA MUME ZAIDI YA MMOJA WAKATI MMOJA
|
Mke
kuolewa na mume zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja yaani kuwa na waume wawili na
kuendelea.
|
Sheria
inakataza mke kuolewa na waume wengi kwa wakati mmoja kwani ni kunyume na
fitrah- maumbile ya asli (Uislamu).
|
Haijuzu
|
5
|
NDOA
KWENYE EDA
|
Kumuoa au hata kumposa mke aliyeachika na bado yupo katika eda
na hakuwa mke wake kabla.
|
Kuwepo kwenye eda ya aina yoyote kwa mke ni kizuizi
kinachomfunga kutoweza kuolewa mpaka imalizike isipokuwa kwa mtalaka wake tu
kama mke aliachika talaka rejea.
|
Haijuzu
|
6
|
NDOA KWENYE UJA UZITO KWA MWANAMKE HAJAPATA KUOLEWA KABLA
|
Kwa mwanamke ambaye hajaolewa akazini na kupatikana ujauzito na
kutaka kuolewa katika hali hii. Ndoa hizi hufanyika pale mambo
yameshaharibika na kutaka kusitiriana
|
Ujauzito
utakuwa na hukumu sawa kama mwanamke aliye katika eda (Ahmad na Abu Haniyfah). Uja uzito hautokuwa na hukumu sawa kama
mwanamke aliye katika eda (Maalik na ash-Shafi’iy).
|
Haijuzu
kwa rai ya Ahmad na Abu Haniyfah
Inajuzu
kwa rai ya Maalik na ash-Shafi’iy ila tu hatopaswa
kustarehe naye mpaka ajifungue.
|
7
|
NDOA
KWENYE UJA UZITO KWA ALIYEACHIKA
|
Mke
aliyeachika na ni mja mzito na kutaka
kuolewa na mume mwengine asiyekuwa mtaliki
wake.
|
Mke
aliyeachika katika uja uzito yupo katika Eda
na humalizika atakapojifungua na kumaliza muda wake wa Nifasi. Kisheria
Eda inamfunga mke kuolewa mpaka imalizike.
|
Haijuzu
|
8
|
NDOA KWA ASIYEKUWA MUISLAMU WALA HAKUTEREMSHIWA KITABU
|
Kuoa
washirikina na makafiri ambao si miongoni mwa walioteremshiwa vitabu
kama mayahudi na manasara.
|
Moja
katika masharti ya kusihi ndoa ni Uislamu. Hivyo kuoa asiyekuwa Muislamu huifanya ndoa kuwa fasidi.
|
Haijuzu
|
9
|
NDOA
KWA ASIYE MUISLAMU LAKINI NI MIONGONI MWA
WALIOTEREMSHIWA KITABU
|
Walioteremshiwa
vitabu miongoni mwa mayahudi na manasara na wanaowafuata katika mila zao.
|
Uislamu
ni moja ya masharti ya kusihi ndoa ila kwa mujibu wa aya za Qur’aan
wameruhusika kuolewa.
|
Inajuzu
ingawa ni Makruuh - haipendezi
|
10
|
KUOLEWA MUISLAMU NA ASIYEKUWA MUISLAMU
|
Mwanamke wa Kiislamu kuolewa na kafiri, mwenye kumshirikisha
Allaah pamoja na mayahudi na manasara.
|
Ndoa
hulazimisha utiifu wa mke kwa mumewe na hivyo kuwepo khofu ya kuweza
kuathirika na kubadilisha dini na watoto kufuata
dini ya baba.
|
Haijuzu
|
11
|
KUOA/KUOLEWA NA ALIYERTADI
|
Mwanamme au mwanamke aliyekuwa Muislamu kisha akaamua kurtadi –
kutoka katika dini.
|
Kwa kukosekana sharti la msingi la Uislamu na hata kama atakuwa amekwenda katika dini ya
walioteremshiwa vitabu.
|
Haijuzu
|
12
|
KUMUOA BINTI ULIYEZAA NJE YA NDOA
|
Mwanamme
kuoa binti aliyezaa baada kutembea (kuzini)
na mama yake nje ya ndoa.
|
Huyu
ni mtoto wake kwani ni mbegu zake ila tu atakosa baadhi ya haki za kimsingi
kwa kuzaliwa nje ya ndoa.
|
Haijuzu
|
13
|
KUOA BINTI WA KAMBO AMBAYE MLIWAHI KUWA NA MAHUSIANO HARAMU NA
MAMA YAKE
|
Kuoa
binti wa kambo ambaye mliwahi kuwa na uhusiano haramu (zinaa) na mama yake
kabla. Si binti aliyezaa nje ya ndoa bali ni binti wa mama.
|
Kutokana
na kupatikana tendo la haramu la zinaa Maulamaa wametofautiana katika tendo
hili (zinaa) je llitaweza kuharamisha halali (ndoa)? Na kuna Qaaidah-“Haramu
haiwezi kuifanya halali nyengine kuwa haramu”. Kuna Qaaidah nyengine “tendo
la haramu huharamisha halali”.
|
Inajuzu
kwa rai ya ash-Shaafi’iy na Maalik kwa
sababu ya kutokuwepo dalili bayana kuharamisha. Haijuzu kwa rai ya Abu Haniyfah na Ahmad bin Hanbal
kwa sababu ya kuwepo tendo la haramu zinaa.
|
14
|
KUOA BINTI WA KAMBO AMBAYE MLIWAHI KUWA NA MAHUSIANO HALALI NA
MAMA YAKE
|
Kuoa
binti wa kambo ambaye kuliwahi kuwepo
mahusiano ya halali (ndoa) na mama yake mzazi na
binti huyu si miongoni mwa watoto wa mume.
|
kutokana na makatazo katika Qur-aan aayah 23 surah
an-Nisaa) na
Qaaidah – msingi wa kisheria yakipatikana maingiliano kwa mama huharamisha
(kuolewa) binti yake.
|
Haijuzu
|
15
|
KUOA
MAMA AMBAYE ULIWAHI KUOA BINTI YAKE
|
Kumuoa
mama ambaye kabla mliwahi kuwa na uhusiano
wa ndoa na binti yake.
|
Kutokana
na Qaaidah ya kisheria “ikipatikana ndoa kwa mtoto, mama huharamishwa”.
Kinachoangaliwa ni kuwepo kwa ndoa bila ya kujali kama pamepatikana maingiliano(Jimaai).
|
Haijuzu
|
16
|
NDOA
KWA WALIONYONYA ZIWA MOJA
|
Ikiwa
watoto wa kike na wa kiume wametokezea
kunyonya ziwa moja kwa mama mmoja na wakataka kuoana.
|
Moja
katika mambo yanayoharamisha ndoa ni kuoa /kuolewa
na mliyenyonya ziwa moja kwani kitendo hiki tayari kisheria kimeshaunda udugu
baina yao.
|
Haijuzu
|
17
|
NDOA
YA KUBADILISHANA (SHIGHAAR)
|
Mwanamme
kumuozesha binti/dada yake kwa mwanamme mwengine ambaye naye atamuozesha binti/dada yake kwa mwanamme wa
mwanzo kwa mabadilishano.
|
Ndoa
hizi hufanyika pasi na kutajwa mahari kwani mahari ya kila mmoja ni
kumkubalia mwengine kuoa kwake “nipe nikupe” na pasi na kupatikana ridhaa ya
upande mwengine.
|
Rai
yenye nguvu haijuzu kwa kufanyika kinyume na misingi ya ndoa ya Kiislamu.
|
18
|
NDOA
YA BOMANI
|
Ndoa
zinazofungishwa na wakuu wa wilaya au kwenye ofisi za wasajili wa ndoa serikalini.
|
Hufanyika
bila ya kutekelezwa masharti ya kimsingi katika sheria za ndoa za Kiislamu kwani si lazima kuwepo mashahidi au kuwa
wanandoa ni wa dini moja.
|
Haijuzu.
Ikiwa
taratibu za nchi zinahitaji kufungwa ndoa hii itawajibika kwanza kufungwa
ndoa ya Kiislamu.
|
19
|
NDOA
YA MISYAAR
|
Mwanamke
hukubali kuolewa huku akisamehe baadhi ya haki zake za kimsingi katika ndoa
kama mahari, huduma na makaazi au hata katika kugawana siku (kwa wake wenza).
|
Ndoa
hizi hufanyika sana katika Bara Arabu hasa kutokana na ughali wa mahari na
hivyo mke katika kutafuta stara huzisamehe baadhi ya haki zake.
Na
pia kama wenye kuoa Afrika huku wakiwa na mke mwengine na hivyo mke wa Afrika
kusamehe baadhi ya haki zake kama za kugawana siku na nyenginezo kwa kuwa
anapata huduma nyengine kama pesa na kadhalika.
|
Itajuzu
ikiwa imetimiza masharti ya kimsingi – Haitojuzu ikiwa haitotimiza
masharti ya kimsingi kama kufanyika ndoa ya Misyaar bila ya Walii.
|
20
|
NDOA
YA MISFAAR
|
Hufungwa
kwa muda maalum kama wakati wa mapumziko au kwa wafanyakazi, wanafunzi ambao
wako mbali na miji au nchi zao humalizika baada ya kurudi sehemu zao
walikotoka
|
Kimsingi
ndoa yoyote itakayowekewa mkataba/muda maalum kumalizika kwake haikubaliki
kisheria kama ilivyo Mut’ah. Mfano wanandoa wamekubaliana kuoana wakiwa
Uingereza tu lakini wakirudi walipotoka ndoa imemalizika hata bila ya talaka.
|
Haijuzu
kwa rai ya Jamhuur
Licha
ya kutimiza masharti yote ya kimsingi ila kwa kuwepo muwafaka wa kumalizika
kwake ambao ni kinyume na taratibu za ndoa ya kiislamu.
Itajuzu
kwa rai ya Abu Haniyfah ikiwa sharti la kumalizika halitozingatiwa kwani ni
sharti batili.
|
21
|
KUOA
MWANAMKE ALIYEPOSWA KABLA
|
Kuvunja
uchumba uliopo na kuposa kisha kumuoa binti ambaye tayari ameshachumbiwa.
|
Kwenda
kuposa mwanamke aliyeposwa ni haramu kisheria. Kwa mujibu wa Hadithi za Mtume
Salla Allahu ‘Alayhi Wasallam. Ikiwa atakayeposa
anajua taarifa za kuposwa kwa binti kabla basi
mtendaji ni mwenye madhambi na dhimma kwa kukiuka makatazo.
Kama hakujua na kufahamu baadae basi uharamu upo pale pale
|
Ndoa
itajuzu kwa mujibu wa rai ya Jamhuur Ulamaa kwa sababu kilicho haramu
kilitokea kabla ya kufungwa na si katika ndoa kwani khutba si miongoni mwa
mwa masharti ya kusihi ndoa.
Haijuzu
kwa mujibu wa Maalik na kama ndoa itafanyika itabidi ibatilishwe
|
22
|
NDOA
YA KUJIFICHA “SIRI”
|
Kuoana
kwa kukamilisha nguzo na masharti yote ya ndoa ila tu wanandoa na mashahidi
kutakiwa kutoitangaza na kuidhihirsha.
|
Ikiwa
ndoa hii itakamilika katika idara zote ila kilichokosekana ni mashahidi tu
kuitangaza ndoa. Kama kuoa mke wa zaidi ya mmoja bila ya kumtaarifu
mke/wake/watu wengine.
|
Inajuzu
kwa sababu ndoa imekamilika kuwepo mashahidi kumeifanya si siri tena, imeshatangazwa.
Ila ni jambo lisilopendeza kisheria (makruuh)
|
23
|
KUOA
KWA NIA YA KUACHA
|
Mume
kuoa na katika mkataba wa ndoa akashurutisha kwamba atamuacha mke katika muda
fulani au bila ya kushurutisha lakini tayari ameshaweka nia katika nafsi yake
ya kuacha.
|
Kimsingi
ndoa yoyote itakayowekewa mkataba/muda maalum kumalizika kwake haikubaliki
kisheria ikiwa imeshurutishwa au kuwekwa nia kwani inakuwa ndoa ya muda
maalum. Na kuwepo ndani yake hadaa na udanganyifu
|
Haijuzu
kwa rai ya Jamhuur kwa sababu ya kuwekewa muda wa kumalizika na udanganyifu.
Itaweza
kujuzu kwa rai ya Abu Haniyfah ikiwa shurti litabatilishwa na kutenguliwa
|
Ni
muhimu kwa kila muislamu kuzifahamu vyema aina hizi na kuhakikisha ndoa yake
imefungwa katika misingi na taratibu zilizo sahihi. Na kama ni miongoni mwa
watakaosimamia au kuwakilisha katika ndoa wazingatie maelezo haya ili waweze
kuwa na uelevu katika mwenendo mzima wa ndoa kuepuka matatizo na kuepukana na
ndoa zenye utata.
Pia
kuwepo tayari kuusimamia ukweli na haki pale ambapo ndoa iliyofungwa ilifungwa
katika misingi isiyokuwa sahihi au baadhi ya taratibu zake kukiukwa.
Ikiwa
ndoa ni moja katika alama zake Allah Subhaanahu Wata’ala na miujiza yake hatuna
budi waislamu kuhakikisha kuzithibitisha alama hizi kwa kuifunga katika misingi
na taratibu sahihi za kisheria.
Na Allah Ndiye ajuaye zaidi.