عَنْ ابْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اللَّهُ
عَنْهُمَا عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فِيمَا يَرْوِي عَنْ
رَبِّهِ عَزَّ وَجَلَّ قَال: ((إِنَّ اللَّهَ كَتَبَ الْحَسَنَاتِ وَالسَّيِّئَاتِ
ثُمَّ بَيَّنَ ذَلِكَ فَمَنْ هَمَّ بِحَسَنَةٍ فَلَمْ يَعْمَلْهَا كَتَبَهَا
اللَّهُ لَهُ عِنْدَهُ حَسَنَةً كَامِلَةً فَإِنْ هُوَ هَمَّ بِهَا فَعَمِلَهَا
كَتَبَهَا اللَّهُ لَهُ عِنْدَهُ عَشْرَ حَسَنَاتٍ إِلَى سَبْعِ مِائَةِ ضِعْفٍ
إِلَى أَضْعَافٍ كَثِيرَةٍ وَمَنْ هَمَّ بِسَيِّئَةٍ فَلَمْ يَعْمَلْهَا كَتَبَهَا
اللَّهُ لَهُ عِنْدَهُ حَسَنَةً كَامِلَةً فَإِنْ هُوَ هَمَّ بِهَا فَعَمِلَهَا
كَتَبَهَا اللَّهُ لَهُ سَيِّئَةً وَاحِدَةً)) البخاري و مسلم
Imetoka
kwa Ibn ‘Abbaas رضي الله عنه kutoka kwa Mtume صلى الله عليه وسلم kwamba
katika maneno aliyoyaeleza kutoka kwa Mola wakeعَزَّ وَجَلَّ ni kuwa Amesema:
((Allaah Ameviandika vitendo vyema na vibaya. Kisha Akavieleza (kwa kusema) yule
anayekusudia kufanya kheri na asiifanye, Allaah Anaiandika kuwa ni tendo jema
kamili. Lakini ikiwa aliazimia na akatekeleza, Allaah Anaiandika kuwa ni
vitendo vyema kumi mpaka mara mia saba na ziada. Lakini anapokusudia kitendo
kiovu na asikifanye Allaah Anakiandika kuwa ni jema moja kamili, lakini ikiwa
amekusudia kutenda baya na akalitenda basi Mola anakiandika kama kitendo kimoja
kiovu)) [Al-Bukhaariy
Na Muslim]